Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, January 31, 2014

BREAKING NEWS: KADI Mia mbili (200) za CHADEMA kurudishwa siku ya kuzaliwa CCM Mbeya

KAMBI YA CCM GREEN GUARD, CHIMALA, MBEYA, YAVUJISHA RIRI

Kila kilichokua kinaendelea katika kambi ya CCM Chimala tulikua na watu wetu. Kamanda Beni wa mbeya mjini alifanikiwa kuingiza watu kumi;CHADEMA Chimala iliingiza makachero watatu 3. 

Kuna kadi za CHADEMA 200 ambazo zilitoka kwa Braison Mwasimba aliyefukuzwa CHADEMA ( alikuwa katibu wa tawi CHADEMA Nzovwe, Mbeya) amekabidhi hizo kadi kwa Gunza wa CCM; huyu ni mwalimu wa Wigamba sekondari (Isanga) na alikuwepo pia katika mafunzo ya Green Guard Chimala. Kadi hizo za CHADEMA wanapanga kuwapa watu siku ya maazimisho ya kuzaliwa CCM ili wazirudishe kwa J. Kikwete. Mpango huu mahusui ni kutaka kumuonyesha Kikwete kuwa CCM inakubalika Mbeya. Hii ni miongoni mwa agenda yao CCM.

CCM wamewafukuza watu kumi na tano (15) kutoka kwenye hiyo kambi, ambao nao walikuwa ni “source” wa hii habari baada ya kupigwa chini. Kati ya walio fukuzwa ni kuwa waligundulika wanatoa siri na wengine walifanya mgomo kutokana na kuahidiwa malipo ya Tsh 10,000/= kwa siku na badala yake kuwa wanalipwa 2,000/= kwa siku. 

Mambo yaliendelea kuwa mabaya baada ya chakula kuisha kambini. Ndipo mwenyekiti wa CCM wilaya, Ndg Mathayo Mwangomo alipo amua kumpigia simu mkuu wa magereza wilayani, Rujewa, na kuomba chakula. Mkuu wa magereza ali mgombeza na kumwambia kuwa usirudie kunipigia tena simu kwani shughuri za chama na magereza haziingiliani. Baada ya chakula kuisha ikabidi waanze kutumia pesa ya posho kununua mahindi na viazi. Hapo ndipo yale malipo ya 2,000/= yakakata na kukawa na mtafaruku kambini. 

Green guard walianzisha mgomo na kusema kuwa wanafanya mazoezi magumu hawawezi kurishwa viazi na wanadai fedha zao. Grean gurad waliandamana na kwenda kituo cha polisi Chimala; walikuwa vijana kama 280. Wakaambiwa waje na viongozi. Baada ya viongozi kuja wali ongea na kuyamaliza; kesho yake wakapewa 10,000/= kila mmoja. Kiongozi aliye anzaisha maandamano akapigwa chini, wakati huo vijana sita washafukuzwa.

Makachero wetu wamefanikiwa kurekodi maongozi ya makubaliano ya pesa. Pia wamerekodi walivyo kuwa wanafanya makubariano ya hizo kadi 200 hapo kambini na Ndg Mwasimba. Wamerekodi hadi maongezi ya kijana walivyo kuwa wakimfukuza na kumnyima nauli; huyo kijana anatokea Mbeya. Record tuliyo nayo ni audio ambayo itatolewa muda muafaka utakapo fika.

Kijana mmoja msamalia mwema wa Chimala ambaye anaitwa Rodi; ni kamanda wa CHADEMA aliwaone huruma vijana walio fukuzwa na bila kupewa nauli kwani walifukuzwa usiku na hawakuwa na mahala pa kulala. Alijitolea kuwarudisha mbeya mjini kwa gari lake.

Green Guard imeondoka leo, Jumamosi, February 1, 2014 kuelekea Mbeya mjini kwaajiri ya sherehe za kuzaliwa CCM.

On other note; Mathayo Mwangomo (Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Mbarali) amekuwa akiwatishia watu kuwa yeye ni serikali na atawaweka ndani. Alikutana na mwenyekiti wa CHADEMA Chimala ambaye alimchana na kumwambia yeye ni mwenyekiti wa CCM wilaya na sio serikali.

TAKE AWAY: KUNA KADI ZA CHADEMA 200 ZITARUDISHWA SIKU YA KUZALIWA CCM MBEYA. HIZI NI KADI AMBAZO ALIYE KUWA KATIBU WA CHADEMA, NZOVYWE , MBEYA, ALIKUWA NAZO. KADI HIZO HAKUZIREJESHA BAADA YA KUFUKUZWA UONGOZI


WE REPORT, YOU DECIDE

MBEYA: WAFANYAKAZI WALAZIMISHWA KUSHIRIKI BIRTH DAY YA CCM


Picha: M4C: Operation Pamoja Daima, Mh. mbowe, Ms. Mdee na Msigwa waachiwa na polis



Pichani ni mwenyekiti wa CHADEMA,Mh. Freeman Mbowe akiwa sambamba na Mbunge wa jimbo la Kawe,Halima Mdee wakiwa wameachiwa na jeshi la polisi akisindikizwa kwenda kupanda chopa katika viwanja vya mwembetogwa mara baada ya kudaiwa kuzidisha muda kwenye mkutano wao wa hadhara mkoani Iringa. (picha zote na Denis Mlowe)

Kutoka kushoto, Ms. Mdee, Peter Msigwa na Mbowe wakiwa wanasindikizwa na nguvu ya Umma baada ya kuachiwa na polis

Mh. Mbowe na Peter Msigwa punde baada ya kuachiwa na polis baada ya mahojiano


Na Denis Mlowe,Iringa
MWENYEKITI wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe na Mbunge wa jimbo la Hai na Mbunge wa Jimbo la Kawe Mhe. Halima Mdee walishikiliwa kwa muda na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu Iringa, kwa kosa linalosemekana kuzidisha muda wa mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mgama wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mbowe alisema jeshi la polisi walimshikilia kwa masaa mawili kwa mahojiano na mkuu wa kituo cha polisi na kisha kumwachia huru. Akizungumza na wafuasi wa Chadema kabla ya kupanda Helikopta na kuelekea mkoa wa Pwani akiambatana na Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee aliwataka wananchama wa Chadema kuungana katika kukijenga chama bila hofu na kuwashukuru kwa kuwaunga mkono katika harakati za kuikomboa nchi.

Alisema wakati wanajiandaa kuondoka alipata malalamiko kutoka kwa kamanda wa Polisi wa Wilaya kuwa wamezidisha muda wa kufanya mkutano katika kijiji hicho.

Mhe. Mbowe alisema kuwa chanzo kingine ni baadhi ya viongozi wa kijiji kuwadanganya wananchi katika mkutano uliotakiwa kufanyika katika vijiji vya kata ya Ukumbi kuwa watakuwepo wabunge na mwenyekiti wa chama katika mkutano kitu kilichosababisha kuwepo na dalili za ugomvi.

“Jeshi la polisi limetuhoji kuhusu mambo hayo na baada ya kuwaeleza walituachia huru... ila wamesema wakituhitaji watatuita lakini makamanda naomba sana mjenge chama na nawashukuru sana kwa kutuunga mkono katika harakati za kuikomboa nchi” Alisema Mhe. Mbowe.


Juu na Chini Mh. Msikwa na Halima Mdee wakiwa na mizigo ya dhambi


PICHA; M4C- OPD, kutoka Polisi Iringa hadi kuitikisa Pwani na kujionea 'maajabu' ya elimu Chalinze

 Wananchi wa Kata ya Kibindu, Chalinze, Pwani wakipiga pipooooooz power ya nguvu mkutano uliohutubiwa na Mwenyekiti wa Taifa Mbowe, Makamu wake Said Issa Mohamed, Peter Msigwa na Halima Mdee leo
 Hapa Mwenyekiti Mbowe akisalimina na mke wa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Pela, Khadija Ali, katika Kata ya Kibindu jimbo la Chalinze mkoani Pwani, ambako alitembelea kujionea hali makazi ya mwalimu huyo, leo.

Wananchi wa Kata ya Kibindu, Chalinze, Pwani wakipiga pipooooooz power ya nguvu mkutano uliohutubiwa na Mwenyekiti wa Taifa Mbowe, Makamu wake Said Issa Mohamed, Peter Msigwa na Halima Mdee leo

Chadema yataka Mwekezaji Mtibwa anyang’anywe Kiwanda.

La sivyo kitaongoza maandano ya kumng’oa.

Na Bryceson Mathias, Mtibwa, Mvomero

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka serikali kumnyang’anya  Mwekezaji wa kiwanda cha sukari Mtibwa rasimali hiyo, kwa kuwa ameshindwa kuwalipa wakulima na Wafanyakazi, hivyo kutishia maisha, ustawi, maendeleo, uchumi na afya wananchi zao.

Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata ya Mtibwa, Luka Mwakambaya (CHADEMA), ikiwa ni siku chache baada ya Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka, kusimamisha uzalishaji wa kiwanda hicho hadi wakulima na Wafanyakazi hao watakapolipwa Malipo yao sh.Bil. 1.9/-.

Hatua zote hizo zimekuja baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe,  kumnanga  Mkuu wa Wilaya hiyo Mtaka, kuwa hatua yake ya kukifunga Kiwanda hicho alikurupuka, na kwamba alichostaahili kufanya ni kuhakikisha anapata njia mbadala ya wananchi hao kupata Malipo yao na si siasa.

Akizungumza na gazeti hili jana, Diwani  Mwakambaya, ameiijua juu Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na watendaji wake, kwamba hawana uchungu na maisha ya wananchi wanaonyanyasika ndani ya nchi yao, kutokana na kushindwa kumuadabisha mwekezaji wa Kiwanda hicho.

“Wananchi wanashindwa kulipa matibabu ya ndugu zao Hospitali ya Bwagala, Wanafunzi wameshindwa kupelekwa shule, wanashindwa kuvaa na kujikimu wenyewe kwa mahitaji, kutokana na mwekezaji kuhodhi Malipo ya wakulima wadogo wa miwa na mishahara ya Wafanyakazi.

“Ninafanya upembuzi yakinifu wa majina ya wastaafu zaidi ya 110 waliokufa bila kupata mafao na haki zao stahili, huku wengine wakiwa wamelipwa kati ya Laki 5/- au Mil.1/- ijapokuwa wamefanya kazi zaidi ya miaka 32 na wengine kufukuzwa bila sababu”. Alisema Mwakambaya.

Mwakambaya alisema, katika ahadi aliyoitoa Meneja wa Kiwanda, Hamad Yahaya, siku ya Mkutano wa hadahara baina ya Mkuu wa Wilaya Mtaka na Wakulima na Wafanyakazi, aliahidi kuingiza fedha sh. 1.9/- bilioni kuanzia leo (jana), lakini fedha iliyoingizwa kwenye chama kimoja cha wakulima ni Mil.70/- tu.

Alisema hali hiyo ni dharau na matusi kwa wakulima na Wafanyakazi wanaoteseka na familia zao nchini kwao, kana kwamba wako Somalia, hivyo akadai anasikilizia kikao cha kesho na Mtaka kitakuwaje laa sivyo, wataiomba Polisi iwalinde mlangoni kwa mwekezaji watakakoweka mikeka.

Katika Kikao na Mkuu wa Wilaya (Mtaka) Mwenyekiti wa Halamashauri ya Wilaya ya Mvomero na Diwani wa Kata ya Diongoya, John Van Zealand (CCM), pia alimjia Juu mwekezaji kwa kushindwa kuwalipa wakulima na Wafanyakazi hao, na kudai hata Malipo tu ya Halmashauri halipi, je ya wananchi!

Wanaharakati mbalimbali wa ndani na nje ya Mtibwa, wameuunga mkono kusudi la wakulima na Wafanyakazi ambao hadi tunaenda mitamboni hawako kazini, kufanya maandano ya amani ya kuitaka serikali imnyang’anye mwekezaji huyo kiwanda, maana anakiuka haki za binadamu, na kwamba wako tayari kuongoza maandamano hayo kudai haki hiyo.

Dk. Slaa ataja mwarobaini wa migogoro ya ardhi nchini


Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Willibrod Slaa, amesema migogoro ya wakulima na wafugani haitaisha ikiwa hawatatengewa maeneo yao maalumu. Aliyasema hayo, wakati akihutubia mamia ya wakazi wa mji mdogo wa Mheza uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga. Alisema wakulima na wafugaji mpaka sasa wanaendelea kugombana na hawana amani katika nchi yao kwa sababu ya migogoro inayoendelea kati yao. Alisema kumaliza migogoro ya pande hizo mbili na kuepuka hatari inayoweza kutokea, ni vyema wakatengewa maeneo rasmi kwa ajili ya shughuli zao. Kadhalika, alisema Watanzania wanahitaji kuunganisha nguvu zao ili wapate haki yao ambayo itawaletea amani ya kudumu. “Pasipo na haki hakuna amani, wakulima na wafugaji wanaendelea kugombana kwa sababu ya kila mmoja anatafuta haki, mwingine anatafuta haki yake ya kulima na mwingine haki ya kufuga na ndiyo maana wanagombana,” alisema na kuongeza:

“Hatutaki makundi haya yaendelee kugombana, tunataka migogoro yao itatuliwe  kwa kila pande kupatiwa eneo lake, hii italeta amani kati yao.” Dk. Slaa alisema amani haipatikani kwa mahubiri tu bali katika kutenda haki kwa kila mmoja anayestahili kuipata. Alisema kati ya mikoa ambayo ina wafugaji na wakulima wengi ni mkoa wa Shinyanga, hivyo unapaswa kuangaliwa kwa jicho la upendeleo kwa kuhakikisha unatengewa maeneo ya kutosha kwa wakulima na wafugaji


Zaya E. Ippmedia/Nipashe

Malecela amvaa Edward Lowassa


  Ni mbio za urais 2015
  Amtuhumu kumwaga fedha

Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samuel Malecela, akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya fulana iliyoandikwa Friends of Edward Lowassa (Marafiki wa Edward Lowassa) alizodai kuwa zimesambazwa nchi nzima. Malecela alifanya hivyo wakati akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake mjini Dodoma jana.

Vita ya kusaka urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) inazidi kuchukua sura mpya kila uchao na safari hii Makamu Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho Bara, John Malecela, ameibuka na kuelekeza mashambulizi yake dhidi ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kwa kumtuhumu kuwa anausaka urais kwa kutumia fedha. Mbali na kumtaja Lowassa wazi, pia ameishambulia sekretarieti ya chama hicho kwa kile alichosema inakaa kimya bila kukemea harakati za watu wanaousaka urais kupitia CCM kinyume cha misingi na katiba ya chama. Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake mjini Dodoma jana, Malecela ambaye pia ni Waziri Mkuu na Makamu wa Rais mstaafu, alisema kuwa ingawa sekretarieti ya chama hicho inajua muda wa kuanza mbio za urais bado haujafika, imekaa kimya bila kutoa karipio lolote.


Mbali ya kumtaja Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, akisema kuwa ni miongoni mwa  wanachama walioanza harakati hizo na kwamba amekuwa akikivuruga chama, alisema ana ushahidi wa harakati zake. “Hapa najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu iko wapi? Mpaka tumuachie mtoto (Katibu wa kitengo cha Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM, Paul Makonda) ndiye akemee haya? Je, hapa chama kiko wapi?” alihoji Malecela. Alisema kuwa anamuunga mkono Makonda kwa kitendo chake cha ujasiri cha kumkemea Lowassa bila woga kutokana na anavyokivuruga chama kwa lengo la kutaka urais. “Naomba niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama,” alisema Malecela na kuongeza: “Kinachonisikitisha zaidi ni kuona juhudi za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja na sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana na Katibu Mwenezi, Nape Nnauye, za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga,” alisema.

Alisema vijana ndiyo wamekuwa wakijenga na kuimarisha chama kwa kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. “Je, chama hakioni haya mpaka vijana ndio waone?” alihoji Malecela.Malecela aliishauri sekretarieti ya chama hicho kuchukua hatua mara moja kwani Makonda asingesema hayo yote kama hana ushahidi wa aliyoyasema. “Na tunapozidi kuchelewa suala hili linazidi kuleta mgawanyiko...vijana na wanachama wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndiyo sababu ya baadhi ya wengine kupoteza mwelekeo,” alisema. Alisema wao walikijenga chama kwa tabu sana na kwamba hakuna mwanachama aliyediriki kutumia fedha zake kutafuta madaraka. “Nidhamu, busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndiyo vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na serikalini, ndiyo maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na wenye fedha kutafuta madaraka,” alisema.

Aliongeza: “Mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi pesa wanazotumia wanazipata wapi? Haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya nani huku Watanzania wakiendelea kuwa maskini, sisi Watanzania siasa yetu isimame kwa upande wa maskini.”  Akizungumzia suala la malumbano ndani ya chama, alisema vitendo hivyo havina tija kwa chama. “Hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo vya habari, vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani ya chama kwa muda mrefu,” alisema Malecela bila kuwataja. “Ninaomba sekretariate ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu Makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba kutaleta kutoelewana ndani ya chama kusikokuwa na ulazima,” alisema Malecela.Alipoulizwa na waandishi sababu za kumtaja Lowassa peke yake, Malecela alisema hawajui wengine bali Lowassa.

Baadaye aliingia chumbani na kuchukua fulana mbili na kuwaonyesha waandishi moja ikiwa na rangi nyeusi na kahawia na nyingine rangi nyekundu na nyeupe zikiwa zimeandikwa ‘Friends of Edward Lowassa’ (marafiki wa Lowassa) na kusema kuwa fulana hizo zipo sehemu mbalimbali za nchi. Katika mkutano huo pia alisema siyo busara kutowapongeza Kinana na Nape kwa kujijenga chama na kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama kwa kukemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali.  “Nawaomba waendelee na juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watu wanaowabeza, naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali,” alisema Malecela. NIPASHE lilipomtafuta Lowassa kuzungumzia kauli hizo hakupatikana. Hata hivyo, mmoja wa wasaidizi wake alipoulizwa, alisema hana la kusema.

KAULI ZA MAKONDA

Zitto kuruka kama CHADEMA

CCM yamwandalia chopa kujibu mapigo ya M4C Pamoja Daima

 USHINDANI wa kisiasa kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umefikia hatua mpya baada ya CCM kuibuka na mkakati wa kumtumia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kupambana na CHADEMA waziwazi.

Katika mkakati huo CCM imepanga kukodisha helikopta ya kumpeleka Zitto katika mikoa minne kwa gharama ya sh milioni 50 mara tu baada ya CHADEMA kuhitimisha Operesheni yao ya M4C Pamoja Daima.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vilivyo karibu na Zitto na CCM, yeye na chama hicho sasa wana adui mmoja – CHADEMA; na wameamua kujibu mapigo baada ya kuridhika kwamba kwa vyovyote Zitto amekwisha kupoteza uanachama wake katika CHADEMA.

Nia yao ni kumtumia Zitto kuleta mpasuko katika CHADEMA, na kufunika mjadala wa mgogoro wa CCM, kero za wananchi na mchakato wa Katiba mpya.

Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA – Naibu Katibu Mkuu Bara, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa Baraza Kuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni – anatarajia kutumia helikopta yenye uwezo wa kubeba watu wanne, ambayo inadaiwa kukodishwa na wapinzani wa CHADEMA.

Kwa mujibu wa habari hizo, lengo la ziara ya Zitto ni kujibu mapigo ya CHADEMA, hasa katika maeneo ambayo baadhi ya makada na viongozi wa chama hicho wamepita na kuzungumzia hatima yake kisiasa, hasa walipojibu maswali ya wananchi kuhusu sakata lake kuvuliwa uongozi kwa tuhuma za usaliti, na hatimaye Zitto kwenda mahakamani kuzuia chama kujadili uanachama wake.

Katika kesi ya msingi, Zitto aliyewahi kuwa maarufu akiwa kiongozi wa CHADEMA, anaomba arudishiwe nyadhifa zake zote, na apatiwe nakala za uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ili aweze kukata rufaa Baraza Kuu.

Taarifa zinasema tayari chama kimempatia nyaraka hizo, lakini kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA, Zitto amekwisha kujiondoa kwenye chama hicho kwa kupeleka shauri mahakamani.

Taarifa za Zitto kuanza ziara mikoani zilianza kusikika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mikoa iliyotajwa ni Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Morogoro na Dar es Salaam, ingawa maandalizi yanaendelea na kuna uwezekano wa kubadili baadhi ya mikoa kulingana na mkakati wao.

Kwa hadhi yake ya sasa, CHADEMA imeshasema haitahusika na mikutano yake, na wanachama wake hawatajihusisha nayo. Uratibu wa mikutano yake unafanywa na viongozi waandamizi wa CCM.

Baadhi yao walizungumza na gazeti hili kwa kujitapa kwamba hii ndiyo njia ya kuimaliza CHADEMA, lakini hawakutaka kutajwa majina gazetini.

Iwapo Zitto atakubali ufadhili huo wa CCM na kuendelea na mikutano yake, ni wazi atakuwa amekamilisha ushahidi wa kinachodaiwa na chama chake kwamba amekuwa akikisaliti kwa masilahi ya CCM.

Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa CCM walipoombwa maelezo juu ya urafiki wao na Zitto kiasi cha kumkosanisha na chama kilichomlea kisiasa, CHADEMA, walisema kwamba urafiki uliopo si wa Zitto na CCM, bali Zitto na Rais Jakaya Kikwete.

Gazeti hili linafahamu kwamba wakati fulani mwaka juzi Zitto alipobanwa na wabunge wenzake kuhusu tabia zake za kuwasaliti kwa Rais Kikwete, alisisitiza kuwa Rais Kikwete ni rafiki yake binafsi, kwa hiyo wamwelewe.

Vilevile, wapo wanaohoji nia ya ziara hii wakati kwa muda mrefu amekuwa akikwepa kuambatana na viongozi wenzake katika ziara na operesheni nyingi za kichama.

Wanasema kwa kuwa operesheni ya sasa ya CHADEMA imepewa jina la M4C Pamoja Daima, kitendo cha CCM kuandaa ziara ya Zitto na kumkodishia helikopta, ni uthibitisho kuwa Zitto hayuko pamoja na CHADEMA tena.

Wameongeza pia kuwa kama hilo litafanyika, litakuwa limemwingiza Zitto katika orodha ya makada kadhaa wa upinzani waliotumikia CCM baada ya kufukuzwa au kunyimwa fursa za uongozi katika CHADEMA, kama Tambwe Hiza, Dk. Aman Walid Kabourou na Dk. Masumbuko Lamwai.

Alipotafutwa athibitishe kuhusu ziara hii na kama ni kweli inafadhiliwa na CCM, Zitto hakuweza kupatikana.

Mbowe kuwania tena uenyekiti

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema kuwa kamwe hatakiacha chama hicho katika uchanga wa harakati za kulikomboa taifa kama kiongozi wake wa juu.

Akihutubia katika mikutano ya Operesheni M4C Pamoja Daima katika sehemu mbalimbali mkoani Morogoro jana, mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa, bado atagombea nafasi ya uenyekiti kwa lengo la kuendeleza harakati za ukombozi wa pili wa taifa hili.

Bila kutaja jina, Mbowe alionya kuwa wenye fikra za kuachiwa chama hicho kikiwa katikati ya ukombozi huo hawatapata nafasi, kwa sababu hawana nia thabiti ya kukiendeleza, bali wana nia ya kukibomoa kwa kutumiwa na wapinzani wa CHADEMA.

“Makamanda, kumbukeni kuwa chama hiki na sisi viongozi wake tumepita katika majaribu makubwa na hata kukoswakoswa kuuawa. Mimi nimekoswakoswa kuuawa kwa bomu huko Arusha, lakini pia kuna watu wamepoteza maisha, wamefungwa jela, wengine wamekuwa vilema, halafu watu wengine wanatusaliti kwa kupewa visenti ili wakivuruge chama na wanataka tuwape chama. Huu ni uendawazimu,” alisema.

Mwenyekiti huyo alisema CCM imekuwa ikifanya jitihada za kuihujumu CHADEMA kwa mbinu mbalimbali, zikiwemo za kupandikiza migogoro, jambo ambalo limeshindwa kufanikiwa kwani Mungu ameweka mkono wake ili kisisambaratike.

“Harakati hizi tunazofanya za kuwakomboa Watanzania mjue tunahatarisha maisha yetu, tumejaribiwa kushawishiwa ndani na nje ya Bunge ili tuwe kondoo, tumekataa. CCM wamekuja na mbinu za kupandikiza migogoro wameshindwa na sasa wanaomba nife wakifikiri nikifa na CHADEMA itakufa. Nawaambia CHADEMA haifi kwa kuwa tumezalisha makamanda wengi, watakiendeleza,” aliongeza Mbowe.

Akielezea kwa mara ya kwanza kwa undani zaidi kuhusu mauaji ya Arusha, mwenyekiti huyo alisema wana ushahidi wa kutosha kwamba polisi walihusika na mauaji hayo na kuongeza kuwa waliohusika ni polisi wa kutoka mkoani Morogoro.

“Kwa mara ya kwanza niliseme hili, mauaji ya Arusha yaliyofanyika kwa kurusha bomu katika mkutano wa kampeni za CHADEMA, yalifanywa na polisi ambao walitoka mkoani Morogoro. Ndiyo maana tunaendelea kumwambia Rais Jakaya Kikwete aunde tume ya kimahakama ili kupata ukweli wa jambo hili,” alisema.

Kuhusu Katiba

Akizungumzia msimamo wa CHADEMA kuhusu muungano, Mbowe alisema chama hicho kinaunga mkono maoni yaliyokusanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, ya serikali tatu.

Alisema hata tafiti mbalimbali zilizofanyika, zikiwemo za wanasheria na wachumi zinaonyesha kuwa Muungano utaimalika zaidi chini ya muundo wa serikali tatu.

“Nawaonya Wana CCM wasijaribu kuingilia mjadala wa Bunge la Katiba na kama wanataka nchi ichimbike, basi walazimishe serikali mbili,” alisema Mbowe.

“Zipo tetesi za CCM kutaka kupitisha hoja zao kwa nguvu kutokana na idadi yao ndani ya wabunge zaidi ya 600, wakiwemo 356 wa Bunge la Tanzania Bara, 84 kutoka Zanzibar na 201 kutoka makundi mbalimbali watakaokwenda kwenye bunge hilo. Wasidanganyike kwamba wanaweza kutumia wingi wao kubadilisha maoni ya Watanzania kuhusu serikali tatu,” alisisitiza Mbowe.

Halima Mdee anguruma

Naye Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, ambaye yuko katika msafara wa mwenyekiti huyo, alisema vijana wengi wanaochipukia katika siasa kupitia chama hicho, wamelelewa na Mbowe, ambao leo wamekuwa chachu ya mabadiliko nchini.

“Ukweli ni kwamba kamanda huyu wa anga (Mbowe), ndiye ametulea vijana wengi nikiwemo mimi, tena wengine hatukuwa na ujasiri tulionao sasa, asiwadanganye mtu, hasa sisi vijana kwamba tuliingia CHADEMA na umaarufu, hawapo hao, tumelelewa na huyo kamanda,” alisisitiza huku akipigiwa makofi.

Tanznia Daima