Pichani ni mwenyekiti wa CHADEMA,Mh.
Freeman Mbowe akiwa sambamba na Mbunge wa jimbo la Kawe,Halima Mdee wakiwa
wameachiwa na jeshi la polisi akisindikizwa kwenda kupanda chopa katika viwanja
vya mwembetogwa mara baada ya kudaiwa kuzidisha muda kwenye mkutano wao wa
hadhara mkoani Iringa. (picha zote na Denis Mlowe)
Kutoka kushoto, Ms. Mdee, Peter Msigwa na Mbowe wakiwa wanasindikizwa na nguvu ya Umma baada ya kuachiwa na polis
Mh. Mbowe na Peter Msigwa punde baada ya kuachiwa na polis baada ya mahojiano
Na Denis Mlowe,Iringa
MWENYEKITI wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe na Mbunge wa jimbo la
Hai na Mbunge wa Jimbo la Kawe Mhe. Halima Mdee walishikiliwa kwa muda na Jeshi
la Polisi, Kituo Kikuu Iringa, kwa kosa linalosemekana kuzidisha muda wa
mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mgama wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.
Kwa mujibu wa Mhe. Mbowe alisema jeshi la polisi walimshikilia
kwa masaa mawili kwa mahojiano na mkuu wa kituo cha polisi na kisha kumwachia
huru. Akizungumza na wafuasi wa Chadema kabla ya kupanda Helikopta na
kuelekea mkoa wa Pwani akiambatana na Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee aliwataka
wananchama wa Chadema kuungana katika kukijenga chama bila hofu na kuwashukuru
kwa kuwaunga mkono katika harakati za kuikomboa nchi.
Alisema wakati wanajiandaa kuondoka alipata malalamiko kutoka
kwa kamanda wa Polisi wa Wilaya kuwa wamezidisha muda wa kufanya mkutano katika
kijiji hicho.
Mhe. Mbowe alisema kuwa chanzo kingine ni baadhi ya viongozi wa
kijiji kuwadanganya wananchi katika mkutano uliotakiwa kufanyika katika vijiji
vya kata ya Ukumbi kuwa watakuwepo wabunge na mwenyekiti wa chama katika
mkutano kitu kilichosababisha kuwepo na dalili za ugomvi.
“Jeshi la polisi limetuhoji kuhusu mambo hayo na baada ya
kuwaeleza walituachia huru... ila wamesema wakituhitaji watatuita lakini
makamanda naomba sana mjenge chama na nawashukuru sana kwa kutuunga mkono
katika harakati za kuikomboa nchi” Alisema Mhe. Mbowe.
Juu na Chini Mh. Msikwa na Halima Mdee wakiwa na mizigo ya dhambi
No comments:
Post a Comment