Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, January 31, 2014

Picha: M4C: Operation Pamoja Daima, Mh. mbowe, Ms. Mdee na Msigwa waachiwa na polis



Pichani ni mwenyekiti wa CHADEMA,Mh. Freeman Mbowe akiwa sambamba na Mbunge wa jimbo la Kawe,Halima Mdee wakiwa wameachiwa na jeshi la polisi akisindikizwa kwenda kupanda chopa katika viwanja vya mwembetogwa mara baada ya kudaiwa kuzidisha muda kwenye mkutano wao wa hadhara mkoani Iringa. (picha zote na Denis Mlowe)

Kutoka kushoto, Ms. Mdee, Peter Msigwa na Mbowe wakiwa wanasindikizwa na nguvu ya Umma baada ya kuachiwa na polis

Mh. Mbowe na Peter Msigwa punde baada ya kuachiwa na polis baada ya mahojiano


Na Denis Mlowe,Iringa
MWENYEKITI wa Chadema Mhe. Freeman Mbowe na Mbunge wa jimbo la Hai na Mbunge wa Jimbo la Kawe Mhe. Halima Mdee walishikiliwa kwa muda na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu Iringa, kwa kosa linalosemekana kuzidisha muda wa mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mgama wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mbowe alisema jeshi la polisi walimshikilia kwa masaa mawili kwa mahojiano na mkuu wa kituo cha polisi na kisha kumwachia huru. Akizungumza na wafuasi wa Chadema kabla ya kupanda Helikopta na kuelekea mkoa wa Pwani akiambatana na Mbunge wa Kawe Mhe. Halima Mdee aliwataka wananchama wa Chadema kuungana katika kukijenga chama bila hofu na kuwashukuru kwa kuwaunga mkono katika harakati za kuikomboa nchi.

Alisema wakati wanajiandaa kuondoka alipata malalamiko kutoka kwa kamanda wa Polisi wa Wilaya kuwa wamezidisha muda wa kufanya mkutano katika kijiji hicho.

Mhe. Mbowe alisema kuwa chanzo kingine ni baadhi ya viongozi wa kijiji kuwadanganya wananchi katika mkutano uliotakiwa kufanyika katika vijiji vya kata ya Ukumbi kuwa watakuwepo wabunge na mwenyekiti wa chama katika mkutano kitu kilichosababisha kuwepo na dalili za ugomvi.

“Jeshi la polisi limetuhoji kuhusu mambo hayo na baada ya kuwaeleza walituachia huru... ila wamesema wakituhitaji watatuita lakini makamanda naomba sana mjenge chama na nawashukuru sana kwa kutuunga mkono katika harakati za kuikomboa nchi” Alisema Mhe. Mbowe.


Juu na Chini Mh. Msikwa na Halima Mdee wakiwa na mizigo ya dhambi


No comments: