Muda huu kwenye Kata ya Itamboleo kijiji cha Kapunga/Mbarali kuna mpambano mkali sana kati ya polisi na Umma. Wananchi wamechoma ofisi ya kijiji, duka la mtendaji wa kijiji pamoja na nyumba yake.

Hii ni baada ya polis kuchukua masanduku ya kura kwa kushindwa kuhesabiwa kutokana na kura kuchanganywa kwenye mabox. Hadi hivi sasa hali ni tete na polis wameita back up kutoka mbeya mjini.