Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, June 18, 2013

Breaking news: Arusha kimenuka

Breaking news: Polisi waamua kutumia mabomu ya machozi na kupiga raia


Polisi wamelipua mabomu mengi ya machozi muda huu kuwatanya Wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Soweto ili kwenda kuaga miili ya marehemu wanaosafirishwa leo.

Polisi wameanza kupiga mabomu wakati wabunge wa CHADEMA walipoanza kuhutubia maelfu kwa maelfu ya wafuasi wake. Hali ni mbaya sana hata watu wametelekeza magari na pikipiki zao, wabunge wote nao wamekimbia na mbaya zaidi wanapiga mabomu kila mahali.

Hali ni tete, mabomu yanarindima sana hali ni tete magari ya mevunjwa gari la Lissu laharibiwa, pikipiki zinavunjwa na polisi bila sababu.

Wametumia risasi za moto kupiga watu, gari la Tundu Lissu limevunjwa vioo na jeshi la polisi. Wameumiza watu wengi sana! Hali ni mbaya sana!

Kufuatana na mgogoro wa serikali na wananchi wa Arusha, barabara inayounganisha kalolen na polisi central mpaka pale benki kuu arusha pamefungwa na inaonekana kuna pilikapilika nyingi central zinazoashiria hali si shwari Huku upande walipo wanaCHADEMA kukirindima mabomu

Kwa kweli hali ni ya hatari na wabunge kadhaa wa Chadema wameshikiliwa, polisi wanatumia nguvu kubwa kupita kiasi. Baadhi ya vyombo vya usafiri vilivyoachwa eneo la tukio polisi wanaviharibu kadiri wawezavyo. Usafiri wa abiria katika barabara ya Moshi-Arusha umesitishwa na hakuna gari zinazopita latika barabara hiyo. Majeruhi ni wengi na wamepelekwa hospitali.

Mabomu yalilipuliwa baada ya naibu mwenyekiti kuhitimisha kwa kuwaomba wananchi waliojikusanya eneo la Soweto waende ktk hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya kwenda kuwaaga marehemu. Awali palitokea mabishano kati ya polisi na viongozi wa Chadema kuhusu mkusanyiko uliokuwapo hapo. Polisi walisema AICC wamekataa uwanja wao wa Soweto usitumike ktk shughuli yoyote. Bado vyombo vilivyoachwa uwanjani na wananchi vinaendelea kuharibiwa na polisi na baadhi ya wananchi wamejificha ktk fensi na baadhi ya nyumba zilizopo ktk uwanja huu.

Tutawaletea taarifa zaidi. Poleni Makamanda wote.

No comments: