Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, February 7, 2014

CCM washambulia mwandishi wa habari vibaya, amri ya Nape? IGP Mangu here is the test

Na Tumain makene
Nimelazimika kukatisha safari baada ya kusikia taarifa za CCM kuanza kutekeleza agizo alilolitoa Nape Nnauye leo mjini Mwanza kwamba Green Guard waanze kufanya kazi yao. Kweli wameanza. Muda mfupi uliopita, Mwandishi wa Habari Christopher Maregesi amepewa kipigo kikali na CCM, huko Bunda. Ilikuwa ni baada ya kitu kinachodaiwa au kuonekana kuwa nimtego kumnasa, kisha watu wa Green Guard, wanaopewa mafunzo kwenye makambi ya CCM yanayoanzishwa kila wakati wa uchaguzi, wakafanya kazi yao.

Taarifa zinasema, waandishi wa habari waliitwa kwenda Ofisi ya CCM ambako eti ilikuwa watoe taarifa kwa vyombo vya habari. Hakukuwa na taarifa yoyote wala kitu cha namna hiyo. Mara baadhi ya waandishi wakaanza kuondoka mmoja baada ya mwingine. Mmoja wa waandishi aliyeondoka ni kiongozi wa CCM. Akabakia Maregesi peke yake. Watu wa CCM wakatekeleza maagizo ya kiongozi wao. Wakamshushia kipigo. Baada ya kipigo, wamempeleka kituo cha polisi ambako hawajafungua kesi yoyote. This is very sad and unbecoming.

Kitendo hiki kimetokea muda mfupi baada ya Nape Nnauye kutoa kauli akiwa mjini Mwanza kuwataka Green Guard, lile jeshi la CCM, waanze kazi. Taarifa zilizopo ni kwamba baada ya press conference kiongozi huyo wa CCM aliekea Bunda. Huko alikopigwa mwandishi. Baada ya tukio Nape amekimbilia Mwanza. Wakati Nape anakimbilia Mwanza baada ya tukio hilo, Waziri Wassira ameonekana kuchanganyikiwa. Alipotafutwa na waandishi amesikika akisema kuwa majukwaani CCM wanajitahidi kuwarubuni wananchi kuwa wanaopiga watu ni CHADEMA, punde inadhihirika kinyume chake. Kumbe CCM ndiyo wanafanya vitendo hivyo. Yeye anadaiwa kusema kuwa hiyo ni aibu.

Tunamwambia Wassira hiyo si aibu. Ni dhambi. Umwagaji wa damu wanaoufanya kulazimisha ushindi au kuwatisha wapiga kura, kisha wanatumia ngao ya vyombo vya dola kulinda uhalifu wao dhidi ya Watanzania wanaowakataa, itawawinda na kuwaondoa madarakani. Pamoja na kuwa msibani, nimefuatilia kwa ukaribu sana press conference ya Nape Mwanza. Amechochea kuni za kutosha. Tukio hilo la Bunda jioni hii limedhihirisha nilichowaambia baadhi ya waandishi walionipigia simu kutaka ufafanuzi wa upande wa pili.


Chama gani kinaweza kufanya vitendo vya ugaidi zaidi ya kile kinachoweka vijana makambini, wakifundishwa matumizi ya silaha, mafunzo ya kijeshi, wakifundishwa namna ya kupiga, kuteka, kutesa na hata kuua? Nikawaambia, hakuna waandishi wenye uzoefu na unyama wa CCM kama walioko Kanda ya Ziwa. Nikawakumbusha vitu vitatu. Kwanza tukio la kuvamiwa, kukatwa mapanga na mashoka wabunge wa CHADEMA, Kiwia na Machemli. Kazi iliyofanywa na vijana wa CCM wanaojulikana kwa sura na majina, mbele ya askari polisi wenye silaha. Si tu kwamba polisi hao hawakuzuia uhalifu wala kuwakamata wahalifu, hadi leo hakuna hatua imechukuliwa dhidi ya watu hao. Kama ni ugaidi unataka zaidi ya huo?

Nikawakumbusha namna ambavyo Green Guards waliwahi kumshushia kipigo cha mbwa mwizi mmoja wa waandishi wa habari, tena mbele ya umati wa watu waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kampeni za mgombea wa chama hicho, ambaye leo ni mbunge, Ndugu Ndassa. Tatu, nimekumbusha kwamba wao wanajua vizuri kuliko hata sie wengine kwamba kama kuna mahali CCM wanafanya siasa za kihuni, completley thug politics ni Kanda ya Ziwa. Jiko lake liko Mwanza. Zinapikwa kweli kweli. Matokeo yake ndiyo hayo yaliyodhihirika tena leo kwa maagizo ya kiongozi mwandamizi wa CCM.

Imekuwa kawaida sasa kwa CCM kuweka vijana wao kwenye makambi kila kinapokuwa na uchaguzi. Wanawapatia mafunzo ya kijeshi, ikiwemo matumizi ya silaha, mbinu za kupiga, kuteka, kutesana hata kuua. Taarifa hizi Jeshi la Polisi linazo. Zimeripotiwa kwao na viongozi wa CHADEMA karibu kila uchaguzi. Dhahiri imekuwa wakati wa chaguzi ndogo; Taja zote; kuanzia Tarime, Biharamulo, Busanda, Kiteto, Igunga, Arumeru, zote. Wanaowekwa makambini hutumika mahali ambapo CCM inaona kuna ukinzani mkubwa na ushindi haupo. Wanaweza kutembea na silaha kama mapanga, wakionesha shari hadharani kabisa.

Katika uchaguzi huu utakaofanyika keshokutwa, moja ya makambi hayo lilikuwa huko Mbarali, Mbeya. Tayari wamefanya kazi yao huko. Wamepiga na kujeruhi watu vibaya kwenye kata inayofanya uchaguzi, Njombe mjini.Mmoja amevunjika taya. Taarifa za uwepo wa kambi hiyo zilitolewa mapema kwa polisi mkoani Mbeya. Maana awali walipanga wafanye fujo kwenye mkutano wa Dt. Slaa alipofika Chimala kwenye M4C-OPD. Mpango ukashindikana baada ya taarifa kunaswa na CHADEMA. Ilitarajiwa kuwa polisi wangechukua hatua ya kuzuia na kuwakamata! Si hivyo ilivyotokea.

Sasa matokeo ya mafunzo ya makambini yameendelea kudhihirika leo, tena kwa amri iliyotolewa hadharani kweupe. Kama ilivyodhihirika Igunga kw akifo cha Mbwana Masoud. Mfano mmoja kati ya mingi ya 'kazi' za vijana wanaowekwa makambini kwa kazi maalum. Kitu alichokifanya leo Nape ni kile ambacho wamekuwa wakiagiza kwa maficho usiku. Polisi wanataka ushahidi zaidi upi? Uchaguzi wa kata 27 unaoendelea nchini utakaohitimishwa Jumapili kwa upigaji w akura ni JARIBIO la kwanza la aina yake kwa IGP Ernest Mangu, kwamba chini ya uongozi wake mpya, tunaweza kuwa na jeshi lisilotumika kubeba chama fulani ambacho kwa sababu ya kuishiwa ushawishi na kukataliwa na watu, kinatumia mbinu hizo za msituni.

IGP Mangu tunataka kuona Jeshi la Polisi linalofanya kazi yake ipasavyo likifuata weledi na maadili, likizingatia sheria kwa ajili ya kutenda haki, si kukimbia kutekeleza maelekezo ya kisiasa ya wanasiasa walioko madarakani leo, kwa manufaa ya kisiasa ya CCM. Tunataka kuona chini yake, CCM kama wanavyofanya Arusha mjini na mahali pengine, hawatumii tena majambazi kupiga watu. Tunataka kuona dismantling ya hizo kambi na vijana hao wakifikishwa mahali panapowastahili, badala ya polisi kuwageuzia kibao viongozi, wabunge, wanachama, wafuasi na wapenzi wa CHADEMA, wakati watendaji wa matukio wakiachwa kutamba mitaani.

Hakuna Jeshi la Polisi linaweza kujijengea imani kwa wananchi iwapo double standards za wazi kabisa zitaendelea kama inavyofanyika hivi sasa, kwa makusudi ya kushughulikia CHADEMA au wananchi wanaopinga CCM! IGP Mangu this is the test...matukio yaliyotokea au yanayotokea katika uchaguzi huu wa marudio katika kata 27, yataonesha Watanzania pasi na shaka mwelekeo wa jeshi unalotaka kuliongoza huko tunakokwenda hasa katika kukabiliana na changamoto za kisiasa zinazohusisha matukio ya kikatili na kinyama kama yanayofanywa na Green Guards, kwa usimamizi wa walioko madarakani, huku polisi wako wakionekana 'kushikwa' mikono katika kuchukua hatua stahili. Zaidi ya hapo, yatawaonesha Watanzania utakuwa IGP wa namna gani katika hali ambayo ni dhahiri kuwa CCM iko ukingoni na anguko lake ni wazi mno, tena kupitia sanduku la kura.

Tumain Makene


No comments: