Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, October 8, 2013

Ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi Wilayani Sikonge, Tabora


Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetupeleka Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora.

 Nikiwa (Zitto Kabwe) na Wenyeviti wa chama wa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora pia Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi Ndg. Mambo tumefanya mikutano 4.



Kero ya Wakulima wa Tumbaku

Kero ya wakulima wa Tumbaku bado ni kubwa sana na tumekuwa tunaelezwa kila tunapokwenda. Hapa Sikonge mwaka 2012/13 Chama Kikuu cha Ushirika kimewakata wananchi fedha za mbolea ambayo wananchi hawakupata. Wananchi wanakaa msimu mpaka msimu kupata fedha za mauzo ya Tumbaku. Makato ni mengi na kufanya mkulima ashindwe kuvunja mzunguko wa umasikini.



Nimetoa mawazo ya kisera kwamba imefikia wakati wakulima kupitia vyama vya msingi wajiunge na mifuko ya hifadhi ya jamii ili kuweza kwanza kuweka akiba, pili kupata mikopo nafuu kupitia vyama vyao vya kuweka na kukopa na hivyo kuweza kuwalipa wakulima pindi wauzapo tumbaku.

Nimetoa wito kwa SSRA waangalie uwezekano wa kuanzisha scheme maalumu ya hifadhi ya jamii kwa wakulima ambapo Serikali ishiriki kwa kuchangia kiwango maalumu katika kila michango ya wakulima. Hii itawezesha wakulima kupata mafao kama bima ya afya, bima ya mazao, mikopo midogo midogo, tofauti za bei na hata elimu kwa watoto wategemezi.


Hili ni wazo jipya lakini linapaswa kutazamwa ni kuinua wakulima wa Tanzania. Tusiendelee kuwasahau wakulima. Watanzania wapo Vijijini, tusiwasahau. Umasikini wa Tanzania unaonekana vijijini (rural phenomenon), tutokomeze umasikini kwa kuwekeza kwa mkulima.

No comments: