Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, September 3, 2013

Wazanzibari wataka Zanzibar ijitegemee karibu kwa kila kitu


     “Kila nchi mshirika (Zanzibar na Tanganyika), ibakie na uraia wake na mtu kuwa na uraia wa nchi mshirika ndiko kumpe uhalali wa kuwa raia wa shirikisho,” alisema. Pia kamati imependekeza Rais wa muungano ambaye atakuwa na madaraka ya juu katika shirikisho lote kwa mambo yote ya Muungano, hivyo nchi washirika zinapaswa kuwa na haki sawa katika kutoa watu wa kushikilia Baraza la Mawaziri la Muungano, Bunge na Mahakama. Alisema rasimu inatakiwa itamke wazi kwamba urais wa Muungano utashikwa kwa zamu na kwa kupokezana baina ya nchi washirika yaani Tanganyika na Zanzibar na kwamba Rais atangazwe mshindi baada ya kupata kura zaidi ya asilimia 50 kutoka Tanganyika na Zanzibar.
Mambo ya kuondolewa
       Alisema uchumi si suala la Muungano hata katika Katiba ya sasa na kwamba nyenzo za kuendeshea na kusimamia uchumi wa nchi kwa maana ya sera za fedha na uchumi zimeendelea kudhibitiwa kupitia Serikali ya Muungano. “Vyombo vikuu vinavyosimamia sera hizo ambavyo ni Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha ya Serikali ya Muungano vimekuwa vikifanya uamuzi na kuyatekeleza bila ya kuzingatia kuwa Zanzibar inategemea uchumi wa utoaji huduma na haiwezi kuwa sawa na uchumi wa Tanganyika ambao unategemea rasilimali,” alisema. Akizungumzia usajili wa vyama vya siasa alisema Rasimu ya Katiba haipaswi kujumuisha suala la vyama vya siasa katika mambo ya Muungano na kwamba Zanzibar na Tanganyika zinatakiwa kuandikisha vyama vyake vya siasa. Alisema badala ya kuendeleza mfumo uliopo sasa wa Makamu wa Rais kupatikana kutokana na mgombea mwenza, marais wa nchi washirika (Zanzibar na Tanganyika) moja kwa moja wawe makamu wa kwanza na makamu wa pili wa Rais wa Muungano.

Source: Wamtambwe (Sept. 2013).Wazanzibari wataka Zanzibar ijitegemee karibu kwa kila kitu. Zanzibar. Retrieved from Mzalendonet

No comments: