Aliyekuwa mwakilishi wa
jimbo la kiembesamaki ndugu mansour yussuf himid ccm kwa tiketi ya ccm amesema
anamshukuru m/mungu kutokana nakufukuzwa kuwa mwanachama wa CCM. akizungumza na
idhaa yakiswahili ya sauti ya ujerumani amesema bado ni mapema kuzungumza lolote
kuhusu kufukuzwa kwake kuwa mwanachama wa CCM. Amesema ataendelea kutoa maoni
yake kupitia mchakato wa katiba unaondelea hapa nchini kama alivyotoa huko
nyuma. Hata hivyo ndugu mansour amefafanua kuwa haiwezekani kuwa na katiba
iwapo hakuna uhuru wakujieleza.
Aidha kiongozi huyo wa
zamani wa jimbo la kiembesamaki ameshauri kuzingatiwa maamuzi ya wengi katika
kupatikana katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Wakati huo huo jumuiya
ya umoja wa vijana waccm wilaya ya dimani kichama jimbo lakiembesamaki imesema
kuwa inaunga mkono uamuzi wakumvua uanachama uliotolewa huko dodoma na
halmashauri kuu ya taifa ya CCM kwa aliyekuwa mwakilishi wao ndugu mansour
yussuf himidi.
Taarifa iliyotolewa kwa
vyombo vya khabari na jumuiya hiyo nakusainiwa na katibu wake ndugu yussu
ramadhani imesema kuwa wanachama wake wamefarijika kutokana na chama chao
kumchukulia hatua zakinidhamu ili kukabiliana na vurugu zilizokuwa zikifanywa
na mwakilishi huyo kwa kutumia ukumbi wa baraza la wawakilishi Zanzibar
kukishambulia,kukipaka matope na kuigawa ccm mbele ya wananchi. Aidha
jumuiya hiyo imeshauri kuwa uamuzi huo usimalizie kwa mansour pekee bali kwa
mwakilishi,mbunge na kiongozi yoyote anayekwenda kinyume na sera za CCM.
Source: Harith (August 2013).Mansour amshukuru mungu kwa kufukuzwa CCM. Retrieved from Mzalendo net
No comments:
Post a Comment