Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Thursday, August 15, 2013

Maelefu ya wananchi wa Kahama kwenye Mabaraza ya rasimu ya katiba mpya


Maelefu ya wananchi wa mji wa Kahama na vitongoji vyake, wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Mabaraza ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya, wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, uliofanyika mjini Kahama jana (kwa ajili ya kuripoti ni juzi)


 Mbowe kuwasili Shy 1 na 2;


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, alipowasili mjini Shinyanga, akiongozana na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ambako walifanya mkutano wa Mabaraza ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya juzi.



Mnyika kuhutubia Kahama;

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, akiwahutubia wananchi wa mji wa Kahama, katika mkutano wa Mabara ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya juzi.



Kada wa CCM;

Aliyekuwa Kada wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Kahama, Malimi Ng'wanabulanhwa, akipkea kadi ya uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutoka kwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, mara baada ya mkutano wa hadhara wa mabaraza ya wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya, ulioanyika mjini Kahama juzi.



Mbowe, Mnyika helkopta;

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika, wakiwasili katika moja ya mikutano yao ya Mabaraza ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya juzi.



Mbowe kuhutubia Malya;

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Malya, wilayani Kwimba, Mwanza, katika mkutano wa hadhara wa Mabaraza ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya juzi.



Mbowe, Mnyika kuwasili Bariadi;

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika, wakilakiwa na wananchi wa mji wa Bariadi mkoani Simiyu, walipowasili kufanya mkutano wa Mabaraza ya Wazi ya kujadili rasimu ya katiba mpya juzi.


Makamanda wa CHADEMA wakiwapokea Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika kwenye mkutano wa hazara baraza la katiba Kahama.

No comments: