Salim Ahmed Salim |
Aidha Dk Salim aliongeza kuwa wizara hiyo ina nafasi nzuri zaidi ya kuchambua na kushauri jinsi ya kutumia vizuri rasilimali za nchi kuendana na uzoefu walioupata kutokana na kufuatilia na kutembelea nchi nyingine duniani. Akizungumzia suala la Muungano, alisema wizara hiyo ipo katika nafasi nzuri ya kuchangia katika suala la katiba gani inahitajika kwani moja ya dukuduku kubwa la Wazanzibari ni kwamba Muungano kwa ulivyo sasa hauwapi nafasi ya kutambulika, na kupata ushirikiano katika medani ya kimataifa hasa kwa yale mambo ambayo si ya Muungano. “Muundo wa Muungano umekuwa ni jambo ambalo limejadiliwa sana na kuonyesha tofauti kubwa kwa wachangiaji mbalimbali, kutokana na uzoefu wenu wa mambo ya nchi za nje na mchango wenu kama wizara inayotetea maslahi ya Tanzania kwa ujumla, na uzoefu uliopatikana mpaka sasa mnaweza mkachangia vizuri pia katika suala la Muungano,” alisema.
Source: Fridolin S. (August 2013).Dk. Salim: Suala la uraia wa nchi mbili litatuliwe. Retrieved from Ippmedia/Nipashe
No comments:
Post a Comment