Jaji Warioba |
Mh. Membe |
Alisema wizara yake inatambua suala
la uraia wa nchi mbili kuwa ni la msingi, ambalo halikugusiwa katika rasimu ya
katiba iliyopo. “Chimbuko la uraia wa nchi mbili
lilitokana na wingi wa Watanzania walioko nje ya nchi ambao wanatafuta fursa ya
kuwekeza na kuinua maendeleo ya nchi yao,” alisema Waziri Membe. Aliongeza pia, “Ilani ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2005 inawatambua Watanzania hao na kutaka wapewe fursa
ya kuwa na uraia wa nchi mbili katika kuinua maendeleo ya nchi.” Alisema Watanzania hao wamekuwa wakikabiliana
na matatizo kadhaa ambayo yanawanyima haki za msingi, kama vile afya, elimu na
masuala ya ajira. “Kilio chao kimekuwa kero kubwa kwa vile wakati mwingine
wanatibiwa kwa gharama kubwa sana ambazo hazilingani na kipato chao,” alisema
Waziri Membe.
Aidha, alisema changamoto hizo
zimekuwa chanzo kikubwa cha kuwashawishi Watanzania hao kuchukua uraia wa nchi
za kigeni ili kuwawezesha kupata huduma muhimu za kijamii kama vile elimu na
afya. “Hivi sasa sheria yetu haimruhusu
Mtanzania kuchukua uraia wa nchi mbili pasipo kuukana uraia wa nchi yake,”
alisema Membe, na kufafanua kuwa “Ilani ya CCM inamuhamasisha Mtanzania huyo
achangie maendeleo ya nchi yake kupitia uraia wa nchi mbili.” Waziri Membe alisema Watanzania
wakiwa nje wanakosa fursa za kazi zenye kipato kikubwa wasipokuwa na uraia wa
nchi hiyo, jambo linalopelekea maisha magumu na kushindwa kujikimu na kuchangia
kipato chochote kwa ndugu zao walioko nchini.
“Badala yake, unakuta Watanzania
wananaswa na tamaa ya ‘kujiripua’ kwa kubadili uraia wa nchi nyingine
zinazokubali uraia wa nchi mbili na kuachana na uraia wa Tanzania,” alieleza
Waziri Membe. Kwa upande wake, Warioba alisema
maoni hayo ya uraia wa nchi mbili yamekuwa yakijitokeza katika ukusanyaji wa
maoni sehemu mbalimbali na kuongeza kuwa, hofu kubwa ya wananchi ni usalama wa
nchi yao endapo uraia wa nchi mbili utaruhusiwa. Waziri Membe alikuwa ameambatana na
Balozi Gamaha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Balozi Bertha Semu-Somi, Mkurugenzi
wa Idara ya Diaspora na James Lugaganya, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango
katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Kwa upande wa Tume mbali ya
Warioba, pia alikuwepo Jaji Mkuu Mstaafu Agostino Ramadhani, Makamu wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Dk. Salim Ahmed Salim, Mjumbe wa Tume, pamoja na Katibu
Asaa Rashid na Naibu Katibu wa Tume.
Source: Mwakawago T. D., & Salum F. ( August 2013).Membe, Warrioba Wazungumzia Uraia wa Nchi Mbili. retrieved from Magazetini
No comments:
Post a Comment