Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Thursday, October 22, 2015

BREAKING NEWS: MBIO ZA UBUNGE: MAFULIKO YAHAMIA MBARALI KWA MWANG'OMBE, AVUNJA REKODI

Liberatus Mwang'ombe "Libe" ameendelea kuvunja rekodi kwa kukusanya watu wengi kuliko mgombea yeyote wa ubunge aliye wahi kutokea jimbo la Mbarali. Mh. Mwang'ombe ambaye amekuwa akiendesha mikutano yake kwa namna ya kipekee kabisa; leo, baada ya kuhutubia aliacha dakika 45 ambapo alisema "nimeomba mdahalo na mgombea wa CCM, Haroon, amekataa; nimeomba mdahalo na mgombea wa ACT, Modestus Kilufi, amekataa; sasa nawaruhusu watu wa Ubaruku mnifanyie mdahalo peke yangu."
Watu wa Ubaruku walimuuliza Mh. Mwang'ombe maswali zaidi ya 10 ambapo walipata majibu stahiki hadi wananchi wakawa wanamwambia Mh. Mwang'ombe inatosha nenda kapumzike. Moja ya maswali aliyo ulizwa Mh. Mwang'ombe ni pamoja na nini atakifanya juu ya huduma ya afya. Mwang'ombe alisema atashirikiana na madiwani, bwana afya wa wilaya na madaktari kuhakikisha wana boresha huduma za afya Mbarali. Zaidi, Mh. Mwang'ombe anaamini kuwa huduma ya afya ni haki ya binadamu; hivyo basi, serikali inawajibu wa kuhakikisha inapeleka vifaa kama, madawa, gloves, nyembe, sindano kwenye vituo vya afya.


 Mh. Mwang'ombe akiendelea kutililika jukwaani

Ni nyomi
 Juu na chini: umati wa watu ulio jitokeza kumsikiliza Mh Liberatus Mwang'ombe



 Mafuliko ya Lowassa yahamia Mbarali






Libe anawaomba wana diaspora na waTanzania wote kumuunga mkono kwa kumchangia fedha ili aweze kutimiza ndoto yake ya kuwa mtunga sheria Tanzania. Msaada wa fedha anaomba utumwe kupitia;

M-PESA- WAVE App number +255 752 494 409

Au, wasiliana na: 
Rehema Sarmet 301 367 9711
Lukresia  240 593 5973
Jabil  240 604 0574 

No comments: