Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, October 7, 2014

CHADEMA: UKATILI WA CCM WAMREJESHA KIWIA HOSPITALINI INDIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UKATILI WA CCM WAMREJESHA KIWIA HOSPITALINI INDIA

Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa hali ya Mbunge wa CHADEMA Jimbo la Ilemela, Highness Kiwia ambaye amekuwa akihudhuria matibabu ndani na nje ya nchi tangu alipovamiwa, kushambuliwa, kupigwa kwa visu na mashoka na vijana wa ulinzi wa CCM (Green Guard), usiku wa kuamkia Aprili Mosi, 2012, imebadilika hivyo ameshauriwa kurejea kwa haraka tena nchini India kwa ajili ya matibabu.

Madaktari wa Hospitali ya Doctor’s Plaza ambao wamekuwa wakimuuguza kwa kipindi sasa baada ya matibabu aliyopewa nchini India mara baada ya tukio hilo la kutisha, wamemshauri Kiwia arejee nchini India baada ya kuona bado hali yake haijatengemaa na anahitaji uangalizi wa hospitali ya Apollo iliyomtibu awali.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam siku ya Jumanne Septemba 30, muda mfupi kabla ya kuondoka kuelekea India, Kiwia ameelezea masikitiko yake kwamba pamoja na kwamba yeye bado yuko kwenye kipindi kigumu cha maumivu makali, miaka miwili tangu baada ya tukio lile alilosema lilikuwa la tishio kubwa la uhai wake, hadi leo hakuna hatua yoyote imewahi kuchukuliwa kwa watuhumiwa aliosema wanajulikana kwa majina na sura.

“Nimelazimika kuondoka kwa dharura kwenda India tena kwa ajili ya matibabu. Nimeshauriwa hivyo na madaktari wa Doctor’s Plaza ambao wamekuwa wakinihudumia kwa muda sasa. Baada ya kunichukua vipimo, wameaniambia niende India kule kule nilikotibiwa awali baada ya lile tukio la kutisha ambalo adi leo sijui niliponaje.

“Ni jambo linaloumiza na kusikitisha sana. Kwamba haki inaweza kutolewa kwa double standards kwa kiwango hiki. Kwamba wale watu waliotushambulia tukiwa na wenzangu akiwemo Mbunge Machemli (Sylvester), kwa marungu, mapanga na mashoka kwa nia ya kutuua wapo, wanajulikana kwa majina na sura, lakini hakuna hatua yoyote imewahi kuchukuliwa dhidi yao.

“Inauma na kusikitisha zaidi kuwa tukio lile lilitokea mbele ya askari polisi wenye bunduki. Vijana wale wa CCM walifanya tukio lile zima la kinyama, kututeka na kutaka kutuua mbele ya askari polisi ambao tulikuwa tukiwaomba msaada. Lakini walikuwa wakiangalia kama vile ni sinema au maigizo ya kutoa uhai wa watu. It was terrible and horrific. Hivi kweli kitendo hiki angekuwa amefanyiwa mbunge wa CCM haki ingetolewa kwa double standards namna hii inavyofanyika kwetu,” amesema Kiwia kwa masikitiko.

Mbali ya kuwaambia wananchi wa Jimbo la Ilemela kuwa atarejea kutoka India na kuendelea kuwatumikia, amesema kuwa atakaporejea kutoka kwenye matibabu anakusudia kulishughulikia tukio hilo kwa namna aliyosema itakuwa ni tofauti na ambayo imekuwa ikitumika sasa katika kusaka haki na hatua dhidi ya wahusika.

“Bunge huwa wanatoa wiki moja kwa ajili ya safari ya matibabu. Lakini mwisho wa siku watakaoamua nirejee lini ni madaktari wa Apollo. Nina matumaini nitarudi nikiwa na afya njema kuendelea kuwatumikia wananchi wa Ilemela,” amesema Kiwia huku akiugulia maumivu makali katika mfumo wa hewa, kichwani (alikokatwa mapanga, shoka na kupigwa marungu) na moyo, huku pia akisema ile hali ya kupatwa na ganzi iliyokuwa ikimwandama siku za awali baada ya tukio lile, imekuwa ikimrejea.  

Imetolewa leo Jumanne, Septemba 30, 2014 na;
Idara ya Habari ya CHADEMA


No comments: