Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Sunday, December 1, 2013

CHADEMA YAANZA KUZINDUA SERA ZAKE, SAFARI 2015

 UTANGULIZI

Mabadiliko ya tabianchi ni jambo bayana linalotokea kwa dhahiri na kuathiri kila sehemu ya dunia tuishiyo kwa kasi ya ajabu. Nchi yetu ya Tanzania ni mhanga mkubwa tayari imeshaathirika sana na mabadiliko ya tabianchi, kama inavyobainika katika namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukame uliokithiri na wa mara kwa mara ambao una athari kubwa sana kwenye kilimo, usafirishaji, nishati, biashara, na sekta ya uchumi-jamii.  Hivi sasa zaidi ya asilimia 70 ya majanga yote ya asili yanayotokea Tanzania yahahusiana na mabadiliko ya tabianchi vikiwemo ukame na mafuriko.

Wakati wa matukio hayo, kilimo katika maeneo husika hudorora au kusimama kabisa, mifugo mingi na wanyama pori hufa kwa kukosa chakula na maji na wakati mwingine husambazwa na mkondo wa maji yaliyofurika.  Kutokana na ukame wa muda mrefu, Tanzania kwa vipindi tofauti, imekuwa ikiathirika na ukosefu mkubwa wa nishati, ambao umekuwa na athari kubwa kijamii na kiuchumi.  Aidha, matukio ya mafuriko ya mara kwa mara yamekuwa na madhara makubwa kwa binadamu, mali na miundominu.

Kilimo na ufugaji, ambavyo ni shughuli kuu za kiuchumi kwa wananchi wengi wa Tanzania, kwa kiasi kikubwa zinategemea mvua za misimu.  Hii inamaanisha kwamba uchumi wa Tanzania, kwa kiasi kikubwa, unategemea tabianchi.  Kwa hiyo, ingependa kutoa mwongozo katika jambo hilo.  Hivyo, waraka huu ni mwongozo wa Sera ya CHADEMA ya mabadiliko ya tabianchi.

Waraka huu wa Sera unafafanua mpango mzima wa CHADEMA wa namna ya kushughulikia mabadiliko ya tabianchi na masuala mengine husianifu. Inatarajiwa kwamba viongozi wetu wa kisiasa katika ngazi za kanda, mikoa.  Wilaya na kata  wataiweka sera hii katika muktadha wa maeneo yao ili iendane na maeneo husika. Mwisho, ninawashukuru Wajumbe wote wa Kamati Kuu kwa kuona umuhimu wa sera hii na kutoa mawazo ya awali ambayo wataalamu wetu waliyatumia hadi kuwa na mwongozo kamili wa sera. 

Ninamshukuru Bwana Finias Magesa kwa kuratibu mawazo yote mpaka kuandikwa kwa rasimu ya awali ya waraka huu.  Pia ninaishukuru Kamati ya Wataalamu ya CHADEMA inayohusika na Sera kwa ajili ya kuuhariri waraka huu na kuuboresha.  Juhudi zao zinapaswa kuthaminiwa sana kwani wamekifanya CHADEMA kuwa chama tofauti chenye mawazo mbadala na bila shaka cha kwanza kuwa na sera inayotoa mwongozo wa mambo yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi.

Kwa namna ya kipekee kabisa, ninapenda kumshukuru kwa dhati, mshirika wetu muhimu na wa muda mrefu, Konrad Adeneur Stiftung (KAS), kwa kugharamia uzalishaji wa waraka huu.
………………………
Freeman Aikael Mbowe
Mwenyekiti wa Taifa,
CHADEMA



SURA YA KWANZA
UTANGULIZI

1.1        MAELEZO YA AWALI 

Athari na Viashiria vya Mabadiliko ya Tabianchi Tanzania.

Tanzania tayari inaathirika kwa uwepo wa mabadiliko ya tabianchi ikiwemo pamoja na ukame wa muda mrefu unaojirudia rudia ambao unaambatana na athari kubwa katika kilimo, usafirishaji, nishati, biashara na sekta mbalimbali za uchumi wa jamii.  Hivi sasa zaidi ya asilimia 70% ya majanga yote ya asili katika Tanzania yanahusika na mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukame na mafuriko.  Wakati wa majanga hayo, kilimo katika maeneo yanayohusika kinadorora au kusimama, mifugo mingi na wanyama wa porini wanakufa kwa kukosa chakula na maji, na wakati mwingine wanabebwa na mkondo wa maji yaliyofurika. 

Kama matokeo ya ukame wa uda mrefu, Tanzania kwa vipindi tofauti imekuwa ikiathirika na matatizo katika kilimo kinachotegemea mvua na ukosefu mkubwa wa nishati ya kisasa, ikiwemo umeme, ambao unasababisha matatizo makubwa ya kijamii na kiuchumi.  Kwa upande mwingine, mafuriko husababisha hali ya kukatisha tama kwa binadamu na wanyama ikiwemo uharibifu wa mali na miundombinu.

Baadhi ya viashiria vya uwepo wa mabadiliko ya tabianchi katika Tanzania ni pamoja na vifo vya mifugo vilivyokithiri kutokana na ukame uliokithiri katika maeneo ya kaskazini mwa Tanzania kama vile Monduli na Longido. 

Kulingana na takwimu za Wakala wa Hali ya Hewa Tanzania, (TMA), kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita (kutoka 1961 mpaka 2005), hali ya hewa ya Mkoa wa Arusha inaongezeka joto na ukavu.  Wastani wa mwaka wa joto umeongezeka kwa nyuzi moja ya sentigredi na Wastani wa mwaka wa joto umeongezeka kwa nyuzi moja ya sentigreti na Wastani wa mvua wa mwaka umepungua kwa asilimia 25%. 

Utokeaji wa mafuriko unaosababishwa na ongezeko lililokithiri la mvua zisizotabirika katika maeneo makavu yasiyo na mimea inayozuia maji kutiririka na kuzama chini kwa urahisi.  Mifano iko mingi ikiwemo mafuriko yaliyotokea Dar es salaam tarehe 21 mpaka 23 Desemba, 2011 na kuua zaidi ya watu 40, yakiharibu nyumba nyingi na miundo mbinu.  Matukio mengine ya karibuni ya mafuriko ni pamoja na yale yaliyotokea Kilosa, Singida, Kilimanjaro na Mbeya – Mbozi katika miaka kati ya 2006 na 2008.

Aidha, ongezeko la joto duniani linalosababishwa na ongezeko la hewa ukaa angani linasababisha ongezeko hatari na utokeaji wa magonjwa mapya kwa mamilioni ya watu, hasa yale yanayoenezwa na vimelea na bacteria (vectorborn diseases) ikiwemo magonjwa kama malaria katika maeneo yenye baridi na milima ambako kwa asili hayakuwepo.  Maeneo kama hayo ni pamoja na Lushoto na Muheza – Amani (Tanga), Rugwe (Mbeya), Bukoba na Muleba (Kagera), Njombe na Mufindi (Iringa).  Kwa takwimu za Wakala wa Hali ya Hewa Tanzania, Wastani wa Joto kwa mwaka wa Mbeya na Iringa imeongezeka kwa nyuzi joto 2 za sentigredi katika kipindi cha miaka 50 iliyopita (1963 – 2007). 

Takwimu zilizochukuliwa katika hospitali ya wilaya ya Njombe, zinaonesha kuwa wagonjwa wa malaria hospitalini hapo waliongezeka kidogo sana katika miaka ya tisini.  Mwanzoni wagonjwa walikuwa wachache, lakini mwaka 2007, takribani wagonjwa 10,000 walifika hospitalini hapo na 211 walikufa.  Ikumbukwe, Njombe ni moja ya maeneo yaliyokuwa na baridi sana na hivyo kutotoa mazingira mazuri kwa uwepo wa mbu.  Magonjwa mengine ni kipindupindu, kuhara, kichocho, typhoid na ebola katika maeneo mapya ambayo hayakuwa na magonjwa ya aina hiyo awali.

Kwa upande mwingine, ongezeko la joto angani na upungufu wa mvua, vimeendelea kuchangia uyeyukaji wa barafu/theluji katika mlima Kilimanjaro.

Inakadiriwa kuwa tangu 1912 hadi leo, takribani kati ya asilimia 50% hadi 80% ya kiwango cha theluji katika mlima Kilimanjaro tayari imeyeyuka na kupotia.  Ukweli huu unaathiri uendelevu na upatikanaji wa maji katika mkoa wa Kilimanjaro na utalii katika mlima huu mrefu barani Afrika.  Inakadiriwa kuwa, kama hali ya hewa itaendelea kama ilivyo sasa, kiwango cha theluji kilichobaki kitakwisha na kupotea kati ya mwaka 2015 na 2020.

Kwa umuhimu ule ule, kutotabirika kwa viwango na majira ya mvua na kiangazi, tayari vinaathiri uwepo, maisha na uhamaji wa wanyama ikiwemo wanyama mwitu kwenye mbuga za wanyama.  Jambo hili ni wazi katika Mbuga ya Wanyama ya Ziwa Manyara, ambako Ndege maji, hususani aina ya Flamingo, wamepotea.

Kwa upande mwingine, kuongezeka kwa usawa wa kina cha bahari, tayari kunaharibu kuta za kuzuia maji ya bahari na kuingia maeneo ya watu na shughuli mbalimbali katika sehemu za Pangani (Tanga) na Kunduchi Dar es Salaam), ikiwa ni pamoja na kuchafua vyanzo vya maji ya kunywa yasiyo na chumvi chumvi katika eneo la Bagamoyo Mkoa wa Pwani.  Aidha, ongezeko hilo limesababisha uzamaji wa maeneo na baadhi ya visiwa katika bahari ya India kama vile kisiwa cha Maziwe na Fungu la Nyani (Serikali ya Tanzania, 2006), na uharibifu wa maisha katika mfumo wa bahari ikiwemo mimea inayolisha na kutumika kama mazalia ya samaki na viumbe wa baharini.

Utegemezi wa kilimo kwa mvua katika Tanzania unamaanisha kuwa uzalishaji wetu katika kilimo unategemea kwa kiwango kikubwa mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi, kutegemea upatikanaji na mtawanyiko wa mvua na joto.

Athari katika kilimo ni pamoja na kupungua kwa uzalishaji katika kilimo, upungufu wa ardhi yenye rutuba, upungufu wa chakula na mazao ya biashara na hivyo ongezeko la umaskini.

Tafiti mbalimbali zinazohusu mwelekeo wa joto wa muda mrefu katika ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa, zinaonedha ongezeko la joto katika maji ya kina kirefu kati ya nyuzi joto za sentigredi 0.2 mpaka 0.7 kuanzia mwanzoni mwa 1900 (Serikali ya Tanzania 2009).

Mabadiliko ya Tabianchi:

Mabadiliko ya Tabianchi yanahusiana na mabadiliko na tofauti kubwa katika takwimu za ama wastani wa hali ya hewa au tofauti ambazo zinadumu kwa muda mrefu (kuanzia miaka 10 na zaidi).  Maelezo haya ya maana ya mabadiliko ya tabianchi kutokana na IPCC kwenye ripoti yake ya tathmini toleo la tatu, yanaongeza kusema ya kuwa Mabadiliko ya Tabianchi yanaweza kusababishwa na michakato ya ndani ya asili, ya nje isiyo ndani ya michakato yetu, au mabadiliko ya kudumu katika historia ya mchanganyiko wa mada/hewa angani au katika matumizi ya ardhi. 

Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi wa shirika la Umoja wa Mataifa (UNFCCC) kwa upande wa pili unatofautisha maelezo yake ya maana ya Mabadiliko ya Tabianchi “yanayosababishwa na michakato na shughuli za wanadamu” na mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababishwa na kazi za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja za wanadamu, ambazo zinabadilisha mchanganyiko wa viwango vya mada/hewa katika anga la dunia, ambayo pia ni nyongeza kwenye mabadiliko ya asili ya hali ya hewa yaliyotathminiwa na kulinganishwa kwa muda mrefu wa kutosha.

Maelezo ya UNFCCC yanamtambua binadamu kama wakala muhimu wa moja kwa moja anayechangia kwenye mabadiliko ya Tabianchi.

Kwa kuzingatia maelezo ya IPCC, upo ushahidi wa nguvu na wa kutosha kuthibitisha ongezeko la joto katika anga kwa miaka 50 iliyopita limesababishwa na shughuli za binadamu.  Shughuli hizo zimesababisha kwa uchache kutokea kwa madhara makubwa ya kimazingira kama vile kulika na kupungua kwa ukanda wa uozone, kupotea kwa biyoanuai na matukio haribifu ya hali ya hewa kwa mazingira.  Aidha, athari za mabadiliko ya Tabianchi zinasababisha matatizo mbalimbali ikiwemo upungufu na upatikanaji wa chakula, ukuaji duni wa uchumi, uhamiaji, usalama, uchafuzi wa maji ya kunywa yasiyo na chumvi chumvi, ongezeko la umaskini na usambaaji wa magonjwa ya kuambukiza katika maeneo mapya kama vile Ebola, Oma ya Bonde la Ufa, Malaria na mengine mengi.

Sababu Zinazochangia Mabadiliko ya Tabianchi:

Sababu nyingi zinazochangia mabadiliko ya Tabianchi zinatokana na kazi za wanadamu kuanzia matumiazi ya nishati ya mafuta ya petrol kwa aina zake zote, matumizi mabaya ya ardhi, na kuingilia mfumo wa ekolojia ikiwemo uchomaji na ukataji misitu.  Kazi za aina hii zinasababisha ongezeko la uhakika la viwango vya hewa ukaa zinazoongeza joto kama vile carbon dioxide, methane, nitrogen dioxide, na chlorofluorocarbons. 

Uimara na uthibivu wa muda mrefu wa ongezeko la viwango hivi vya hewa ukaa katika anga ni wa muhimu kwa sababu ndivyo vinavyosharabu mionzi inayotoka duniani na kuinasa ili kuongeza joto la dunia mpaka kiwango kinachoruhusu maisha kuendelea.  Kiwango cha sasa cha hewa ukaa angani kinakadiriwa kuwa vipande 390 kwa kila million (ppm) CO2e.  kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa na kuacha viwango vya hewa hiyo angani kata ya vipande 350 – 450 kwa kila million (ppm) CO2e hakuepukiki.

Upunguzaji huo ni wa lazima kwa kila sekta ili kuwezesha uwezo wa mataifa yote kustahimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi.  Ni lazima njia mbalimbali zilizopo za kukabili tatizo hili ambalo linaweza pelekea mabadiliko ya kudumu ya tabianchi kwa sayari yetu dunia haziepukiki.  Mfumo asilia wa ekolojia unatoa fursa muhimu wa kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kwa haraka na kutunza uwezo wa sayari dunia kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Ongezeko kubwa la hewa ukaa angani linasababisha mabadiliko ya tabianchi yenye uwezo wa kudhuru mustakabali wan chi mbalimbali duniani.  Sanyansi inakadiria kuwa kupunguza kiwango cha hewa ukaa angani hadi vipande 350 kwa million CO2E kutasaidia dunia kurudisha nyuma hatari ya maji ya bahari kuwa tindikali na kuyeyuka kwa ncha ya Aktika kunakosababisha kuongezeka kwa kina cha bahari na visiwa kuzama.   Kubakia katika kiwango cha vipande 450 kwa milioni CO2einapendekezwa na sanyansi kuwa ndio kiwango cha juu cha hewa ukaa kinachoruhusiwa angani kama hatuhitaji ongezeko la joto linalozidi nyuzi joto 2 za sentigredi, ambalo litakuwa na matokeo hatarishi na majanga ambayo yatahatarisha uwepo wa sayari dunia yenye uwezo wa kutunza uhai wa binadamu na wanyama na shughuli zao.

Ni muhimu kutambua ya kuwa mfumo wa nishati wa dunia unahusika kwa zaidi ya nusu ya hewa ukaa yote inayozalishwa duniani.  Sehemu kubwa ya hewa joto hizi ni hewa ukaa (CO2) na methane.  Sehemu kubwa ya uzalishaji wa hewa joto hizi unatokana na matumizi ya mafuta ya petrol kwa aina zake zote kama chanzo cha nishati.  Kuongezeka kwa hewa ukaa angani kunasababisha kuongezeka kwa joto la anga ambalo wataalamu wameridhika linahusika na mabadiliko ya tabianchi na madhara makubwa kwa mazingira.

Uchomaji na ukataji wa Misitu kwa ajili ya malisho, makazi na shughuli zingine za kiuchumi ni chanzo kingine kikubwa cha uzalishaji wa hewa ukaa angani, japokuwa imekuwa inapewa uzito mdogo.  Inachangia takribani asilimia 16% ya uzalishaji wa hewa ukaa yote duniani.  Hii ni sawa na hewa ukaa yote inayozalishwa na magari yote duniani, malori, meli, matreni na ndege vikiunganishwa pamoja.

Kulinda ekari moja ya misitu kwenye ukanda wa mvua nyingi ni sawa na kuondoa uchafuzi wa magari 14 kutoka barabarani.  Kwa upande mwingine matumizi bora ya ardhi ni chanzo kingine cha uzalishaji wa hewa ukaa.  Upanuzi wa shughuli za kilimo kwenye maeneo oevu na yenye maji maji, kwenye kingo za mito vimekuwa vikiingilia uwezo wa ekolojia kuzalisha maji (chemic hemi za asili) na malisho ya mifugo kwa nyakati zisizo na mvua.

Wanyama mwitu na mifugo wanaathiriwa na ukame kwa sababu ya upotevu wa vyanzo muhimu vya nyasi na ekolojia.  Kama vile haitoshi, wanadamu wameendelea kubadilisha uso wa dunia kwa njia mbalimbali ikiwemo upanuzi wa miji, uvunaji na ukataji misitu, umwagiliaji wa maeneo kavu na mazao, kutengeneza mabwawa na maziwa, upandaji miti, na matumizi ya ardhi oevu na chemichemi kwa kilimo.  Katika mabara mengine, kama vile Amazon, ubadilishaji wa matumizi ya misitu kwenda miji au shughuli nyingine kunachangia kama chanzo kikuu cha uzalishaji wa hewa ukaa kinachoongoza katika nchi kwa takribani asilimia 70% ya hewa ukaa yote inayozalishwa nchini mwao.

Bila kujali vithibitisho mbalimbali juu ya uhusika wa mwanadamu katika kusababisha mabadiliko ya tabianchi na matokeo yake mabaya kwa jamii, uchumi na maendeleo, jitihada chache zimefanywa na kuinua uelewa wa jamii na kuwaelimisha, hususan vijana kuhusiana na uwepo na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa mustakabali wa maisha yao ya kila siku.  IPCC imeeleza katika ripoti yake ya tathmini ya nne, ya kwamba mabadiliko ya tabianchi ni kitu halisi na tayari yanaendelea kutokea duniani katika spidi kubwa.  Japokuwa siyo rahisi sana kutabiri kitakachotokea baadaye kwa usahihi mkubwa sana, ripoti hii ya nne ya tathmini ya IPCC inaonesha kuwa kuna ujuzi na uelewa wa kutosha kuelezea na kushughulikia athari na hatari za mabadiliko ya tabianchi yanayoendelea kwa sasa (IPCC, 2007).

Juhudi za Kitaifa zilizopo:

Kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Serikali ya Tanzania inatoa elimu ya mazingira kwa wanafunzi.  Elimu hii inatoa uelewa wa awali juu ya masuala mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi, lakini mara nyingi imeshindwa kuunganisha vya kutosha uhusiano wa utaalamu wa juu ya mabadiliko ya tabianchi, vyanzo vyake, mikakati ya kustahimili mabadiliko hayo katika sekta mbalimbali za kiuchumi na maendeleo na njia bora za kushiriki upunguzaji wa uzalishaji wa hewa ukaa nchini. 

Aidha, Idara ya Mazingira katika ofisi ya Makamu wa Rais, imekuwa ikijishughulisha na mikakati mbalimbali ya kustahimili athari za mabadiliko ya tabianchi na kuhamasisha upunguzaji wa uzalishaji wa hewa ukaa nchini kama sehemu ya mkakati wa kitaifa na mchango wa nchi katika agenda za kimataifa.  Hata hivyo kwa kuzingatia uwezo mdogo, raslimali chache, mfumo legevu wa kitaasisi na mpangilio katika kushughulikia masuala ya mabadiliko ya Tabianchi, ufanisi umebakia mdogo na hivyo matokeo si yenye tija sana.  Inatosha kusema kwamba masuala ya tabianchi yamekuwa yakipokea umakini mdogo kutoka kwa serikali yetu ukilinganisha na umuhimu wake.

Sera ya Taifa ya Mazingira (1998), Sheria ya Mazingira (2004) na Mkakati wa Taifa wa Mabadiliko ya Tabianchi na Mpango Kazi ambao unaotayarishwa kwa sasa, havitoshelezi inapokuja kwenye ukamilifu wa muktadha, malengo, na uwepo wa vyombo vya utekelezaji kufikia malengo kusaidiwa.  Kwa upande mwingine, kwa miaka mingi serikali imeendelea kutotoa umuhimu wa kutosha kwa suala la mabadiliko ya Tabianchi, kwa kushindwa kutayarisha hata sera mahususi juu ya suala husika ambalo limebakia muhimu kwenye agenda za kimataifa na hivyo kushindwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na fursa zilizopo.

Ni kwa kuzingatia ukweli huu CHADEMA tunakuja na sera mbadala ya mabadiliko ya Tabianchi ambayo itasaidia Taifa kuingia kwa undani na kivitendo na kimkakati zaidi kuzingatia na kutoa majibu yanayotatua athari na matatizo ya mabadiliko ya Tabianchi,  wakati huo huo sera ikijenga mazingira bora kwa watanzania kunufaika na fursa za kitaifa na kimataifa zinazopatikana katika mabadiliko ya tabianchi ikiwemo biashara ya hewa ukaa.  Sera hii mbadala ya CHADEMA ya mabadiliko ya tabianchi inalenga kuongoza jitihada za CHADEMA kama chama na wadau mbalimbali katika nchi kufanikisha ushiriki wenye tija wa Tanzania katika suala zima la mabadiliko ya tabianchi kitaifa na kimataifa. 

Kimsingi Sera mbadala ya CHADEMA ya mabadiliko ya Tabianchi inalenga kujenga uwezo na ujuzi wa watanzania, kuwapa majukwaa ya kusemea na kushiriki utekelezaji, kuandaa na kusimamia uwepo na upatikanaji wa dhana za utekelezaji wa sera, kuonesha kivitendo katika jamii jinsi jitihada za kupunguza ongezeko la hewa ukaa angani na kujenga uwezo wa kustahimili mabadiliko ya tabianchi ambayo tayari yapo vinavyoweza kuleta tofauti kati maisha ya kawaida ya mtanzania.  Zaidi, ni kuwajengea watanzania wa kada zote uwezo na uelewa wa kushiriki na kunufaika na fursa zilizomo katika mabadiliko ya tabianchi katika ngazi zao zote za jamii ya Kitanzania.

Kwa sababu kazi za kila siku za kijamii na kiuchumi za wanadamu zinachangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya Tabianchi, ufumbuzi wa tatizo la athari za mabadiliko ya tabianchi unapaswa pia kuhusisha uzingatiaji wa madhara na njia bora za kustahimili na kudhibiti uzalishaji na ongezeko la hewa ukaa katika kazi za kila siku za mwanadamu.  Hivyo mikakati inapaswa kuzingatia umuhimu wa kuzingatia masuala ya tabianchi kwa kila mwanadamu kwa kila analolitenda kila siku.  Mfumo rasmi wa elimu na ule usio rasmi wa watanzania, taasisi za kidini na kijamii, za serikali na zisizo za serikali, vyama vya siasa na sekta binafsi, vyote vitumike kueneza na kusambaza taarifa sahihi, ujuzi na uelewa juu ya athari na madhara ya mabadiliko ya tabianchi na namna bora ya kustahimili athari hizo katika ngazi zote za jamii.

Kwa kufanya hayo CHADEMA itakuwa imeshiriki na kuchangia kujenga uwezo na ushiriki wa watanzania na kuingoza jamii katika kutathmini na kutumia njia bora za kuendeleza maisha yao kwa ufanisi katika mazingira ambayo yameathiriwa au yataathiriwa na mabadiliko ya tabianchi hivi karibuni.  Sera hii inawasilisha kwa jamii uwajibikaji wa kiwango cha juu wa CHADEMA katika kushiriki jitihada za kushughulikia na kutatua matatizo na changamoto za kimazingira na mabadiliko ya Tabianchi kwa faida ya kizazi cha sasa na vijavyo.  Sera inazingatia hitaji la sheria za kimataifa za mazingira na inaheshimu kanuni ya maendeleo endelevu ambavyo vimezingatiwa katika malengo ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC).

1.2        Sera za Taifa na Mikakati iliyopo.
Kwa kuzingatia ukweli kwamba Katiba ya sasa ya Tanzania ina udhaifu mbalimbali katika kushughulikia changamoto mbalimbali muhimu za jamii, sera, mikakati na sheria zingine za sekta zilizotungwa chini ya sheria hii mama zimezingatiwa lakini uboreshwaji umefanyika na matumizi ya maeneo yanayolenga ukombozi wa kweli wa mtanzania ndiyo yamezingatiwa zaidi.

Baadhi ya sera za sekta zilizopitiwa kwa uchache na kuzitathmini ni zile za nishati, mazingira, usafirishaji, ardhi, maji, misitu, kilimo, uvuvi, afya, majanga, jinsia na utalii.

1.3        Mikataba ya Kikanda, Kimataifa na Itifaki Mbalimbali

Sera hii pia imezingatia mikataba ya kimataifa, kikanda na itifaki mbali mbali zilizopo bila kuathiri matakwa ya kimaendeleo ya kitaifa.  Sera imezingatia changamoto na ugumu wa maridhiano katika suala la mabadiliko ya Tabianchi baina ya mataifa mbalimbali yaliyoendelea na yanayoendelea yanayojikita katika maslahi binafsi na siasa za kimataifa za nchi mbalimbali.  Japokuwa suala la mabadiliko ya tabinchi ni suala nyeti kwa mataifa yote, siasa za kimataifa na maslahi binafsi yamelifanya kuwa suala gumu kufikia maridhiano mbalimbali ya ushughulikiaji changamoto zilizopo.  Upunguzaji wa hewa ukaa angani na jitihada za kujenga uwezo wa mataifa mbalimbali kustahimili athari za mabadiliko ya tabianchi ni za muhimu sana lakini zimeendelewa kuathiriwa na mfumo na siasa za kimataifa (Einnersting, 2007).

Ukweli kwmba madhara ya mabadiliko ya tabianchi yanaathiri kila mwananchi katika kila nchi, imepelkea uwepo wa maslahi binafsi yanayokinzana kimataifa na hivyo kupelekea suala hilo kuwa gumu kufikia maridhiano katika historia ya dunia.  Masuala ya mabadiliko ya tabianchi yanashughulikiwa kwa kuzingatia sayansi na ujuzi wa masuala ya asili na hali ya hewa.  Hata hivyo IPCC imezishinikiza serikali za mataifa duniani kushughulikia suala hili.  Msukumo na utaratibu huu mpya unatofauti na ule wa asili wa ushirikiano wa kimataifa, na kwa nyakati tofauti umesababisha misuguano baina ya mataifa mbalimbali.

Katika siasa za kimataifa wakati mwingine maslahi binafsi ya taifa na itikadi yake vinakuwa juu ya sababu zingine zozote za kuongoza maamuzi ikiwemo hata ile ya sayansi na utaalamu unavyotaka.

Ni ngumu kuelezea lakini sanyansi huwa inakosa nguvu yake ya kuongoza maamuzi katika siasa za kimataifa, na mara nyingi ukweli unaweza kipindishwa au kutopewa umuhimu stahili.  Hili jambo linaweza kuonekana kirahisi kwa maamuzi na misimamo ya Amerika, China, Kanada, Japan, Brazil, India na nchi zingine ambao ni wachafuzi na wazalishaji wakuu wa hewa ukaa duniani kuamua kutoendelea au kushiriki katika utekelezaji wa matakwa ya Itifaki ya Kyoto ya upunguzaji wa uzalishaji hewa ukaa duniani huku wakijua fika unyeti wa suala husika katika mkutano wa COP 17 Durban Africa ya Kusini.

Mikataba ya Kikanda na Itifaki ambavyo vimezingatiwa katika utayarishaji wa sera hii ni pamoja na Mkataba wa Uanzishaji Jumuiya ya Afrika Mashariki, Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayohusu Mazingira na Maliasili, Sera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu mabadiliko ya Tabianchi, Itifaki ya Maendeleo Endelevu ya Bonde la Ziwa Victoria, na mwongozo wa kufanya upembuzi yakinifu wa athari za kimazingira na ekolojia inayoshirikisha nchi za jumuiya na mkakati wa maendeleo ya Jumuiya ya Afrika mashariki (2011 – 2015).

Mikataba ya kimataifa, Itifaki na sheria za kimazingira za kimataifa zilizopitiwa katika utayarishaji wa sera hii ni pamoja na Mkataba wa shirika la umoja wa mataifa unaohusu mabadiliko ya tabianchi na Itifaki ya Kyoto.  Lengo kuu la mkataba wa umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi ni kufanikisha uthabiti wa mchanganyiko wa hewa ukaa angani katika viwango ambavyo havitasababisha mabadiliko ya kudumu ya tabianchi yatakayoshindwa kuruhusu uendelevu wa uwepo wa uhai katika dunia yetu. 

Kudumisha viwango vya hewa ukaa angani ambavyo vitaruhusu ekolojia asilia kuwa na muda wa kutosha kuhimili mabadiliko ya tabianchi yatokanayo na shughuli za watu na maendeleo, kuhakikisha upatikanaji salama wa chakula na maendeleo endelevu (UNFCCC 2005).  Mikataba mingine ni ile ya Umoja wa Mataifa kudhibiti ongezeko la jangwa (UNCCD); Mkataba wa bayonuai ya kibailojia (CBD); Mkataba wa Biashara ya Kimataifa wa Maliasili zilizo katika hatari ya kupotea duniani (CITIES); Mkataba wa Ramsar kuhusu ardhi Oevu na unyevuunyevu yenye umuhimu wa kimataifa.  

No comments: