Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Wednesday, December 11, 2013

CCM wamhujumu Dk. Slaa

    JESHI la Polisi mjini Kasulu jana lililazimika kupiga mabomu ya machozi, kuwatawanya vijana takriban 15 ambao wanadaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), walioanza kuwarushia mawe polisi na wananchi waliokuwa wakisikiliza mkutano huo. Kitendo cha vijana hao kuwarushia mawe polisi na wananchi kilizua mtafaruku ambapo polisi waliamua kupiga mabomu ya machozi, wakati Dk. Slaa akiwataka vijana waliokuwa na mabango waende mbele ya mkutano awasikilize. CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimedai kubaini mkakati mzima unaoandaliwa kwa ajili ya kuvuruga na hatimaye ikiwezekana kufanya jambo baya la kudhuru au kuua, ili kuharibu ziara ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa inayoendelea mkoani Kigoma kwa sasa.
       Wakati chama hicho kikibaini njama hizo, Dk. Slaa ametoa kauli nzito akisema kuwa atazunguka nchi nzima kama ambavyo amefanya kwa kwenda kila mahali tangu mwaka 2011, kwa sababu Katiba ya nchi inampatia uhuru huo bila kutegemea hisani ya mtu. Aliyasema hayo jana alipokuwa akihutubia wananchi wa kijiji cha Malumba, jimbo la Kasulu Mjini, ambapo wananchi walimsubiri kwa muda mrefu kisha kuvumilia mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha katika maeneo hayo, wakati wakisikiliza hotuba yake. “Naona ofisa wangu hapa Waitara anazungumza kwa kusita, mwisho atawatia hofu wananchi wangu bure. “Kwanza sipendi sana kujibizana na hao anaowasema Waitara, hao si saizi yangu.
      “Ninachoweza kuongezea katika maneno yake hayo ni kwamba Dk. Slaa hajawahi kuogopa, Dk. Slaa si mtu wa hofu, Dk. Slaa hajawahi kutishika. “Nilisema baada tu ya uchaguzi wa 2010 kwa sababu sijaenda Ikulu, kazi yangu itakuwa ni kujenga chama, hiyo ndiyo kazi ya katibu mkuu. “Katika hilo tena kiongozi wa kisiasa sina mipaka. Nitakwenda kila mahali katika nchi hii kama ambavyo nimepita kila jimbo, kila kijiji tangu 2011. “Hakuna mtu mwenye hatimiliki na eneo lolote la nchi hii. Kwangu mimi si mara ya kwanza kutishiwa maisha. “Nimetishiwa mno. Sitaacha kuzunguka na kutetea wananchi wangu wanyonge hawa sababu ya upuuzi fulani tu hivi. “Wanapoteza muda wao. Mlinzi wangu ni Mwenyezi Mungu pekee,” alisema Dk. Slaa huku akishangiliwa na wananchi wa Malumba.
       Mapema mratibu wa ziara hiyo, Waitara Mwita, alidai kuwa wamebaini mikakati inayopangwa na watu aliosema kuwa ni makada na viongozi wa CCM wakishirikiana na baadhi ya wanachama wa CHADEMA wasiokuwa watiifu au ambao wamewahi kuadhibiwa na chama, kuhujumu ziara ya Dk. Slaa. “Tunajua mikakati iliyopo. Walianza na kuleta vijana walevi kwenye mikutano wakiwa na mabango wameshindwa, sasa wanapanga kufanya fujo ili mikutano isifanyike kabisa. Lakini mkakati mkubwa ni ule unaopanga kufanyika Kigoma mjini kuzuia na ikibidi kudhuru watu kwenye mkutano huo. “Mkakati huo unaandaliwa na CCM kwa kushirikiana na watu wanaojiita ni CHADEMA.
      “Kuna vijana wanapewa mafunzo pale ofisi ya mkoa na mtu anayejulikana kwa jina la Hamis, mtu huyo na wenzake ndiyo waliotumika kwenye tukio la kukata mapanga wabunge wetu Machemli na Kiwia pale Mwanza. “Tunajua kuna kundi la watu walitoka jana Mwanza kwenda Kigoma mjini kwa ajili ya kufanya vurugu, wako kwenye magari kadhaa, wanafikia idadi ya watu 60 hivi, wanaongozwa na mabaunsa wa Matata aliyefukuzwa unachama wa CHADEMA lakini CCM wakampatia umeya,” alisema Waitara. Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma na Meya wa Ilemela aliyeenguliwa CHADEMA, Matata, ndiye anayeongoza kufanya hujuma hizo. 
Source: Senga J. (Dec. 2013). CCM wamhujumu Dk. Slaa. Retrieved from Tanznia Daima

No comments: