Kutoka Kushoto, Mwanafunzi wa Kitanzania, Dr. Slaa, mwanajeshi mtafiti pamoja na Mwenzie ambaye ndiye kiongozi wa utafiti |
Katibu mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Dr. Wilibrod
Slaa akiendelea na ziara yake iliyopewa jina la “Vision Tanzania” leo
ametembelea chuo kikuu cha Indiana ambako ametembelea kitivo cha utafiti wa
nishati mbadala “Center for Renewable Energy” ambako alilakiwa na Vice
Chancellor wa Chuo hicho. Dr. Slaa amependezwa kuona jinsi wanafunzi na wanajeshi
wanavyoshirikishwa katika utafiti kwa manufaa ya nchi. Dr. Slaa alijionea
mashine ya ndogo ya aina yake inayotumia takataka na hata majani kutengeneza
umeme pamoja na gesi ya hydrogen kwa wakati mmoja, mtambo uliogunduliwa kwa
ushirikiano kati ya chuo kikuu cha Indiana na Jeshi la Marekani.
Bahati mbaya wanafunzi kama hawa nchini kwetu serikali
imewanyima nafasi ya kukuza vipaji vyao na kutusaidia kwenye maswala ya
utafiti. Wanajeshi wetu waadilifu, wachapakazi na wazalendo wamekatishwa tamaa.
Gari la nyumbu walilotengeneza linaoza na mradi mzima umekufa. Wastaafu
wametelekezwa hadi malipo yao wanadhulumiwa na serikali dhalimu ya CCM. Hiyo
ndiyo CCM. Kwa miaka zaidi ya 50, serikali ya CCM imekuwa ikitoa ahadi
za kumaliza tatizo la umeme. Mpaka sasa, CCM bado wanaendelea na ahadi zao kana
kwamba watanzania bado wamelala. Ni swala la fedheha na aibu kubwa kwa nchi
kama Tanzania kuzunguka kuomba misaada wakati tunacho kila tunachohitaji
kujitengenezea umeme wa kutosha alisema Dr. Slaa
Tanesco ambayo ingekuwa inatutengenezea umeme wa kutosha kwa
matumizi yetu na kuuza nje ya nchi umeme wa ziada, imegeuka kuwa shamba la bibi
na kichaka cha mafisadi. Wizara nayo imekuwa makao makuu ya matusi kwa
wawekezaji na watanzania. Waziri muhongo badala ya kutafuta suluhisho ya
matatizo yeye amekuwa mtambo wa matusi. Anawaambia watanzania wakawekeze kwenye
juice na matunda. Hii ndio maana tunasema kwamba CCM ni janga la mtanzania. Tunachotaka kujua ni Uhusiano wa Symbion na serikali ya CCM.
Tunataka kujua hii kampuni ya Symbion inamilikiwa na nani . Kwa sababu ni hii
Symbion ndiyo ilitokana na Dowans ambayo ilizaliwa na Richmond. Makampuni
ambayo yanatafuna kodi zetu hadi wa leo. Wanatudanganya watawashtaki mafisadi
wa Tanesco, tunawaomba waanze na mafisadi papa wa EPA na Richmond
Rais Kikwete na CCM wamekuwa janga. Leo Kikwete anaagiza
shule zote za kata ziwekewe umeme. Umeme gani wanaozungumzia na utatoka wapi
wakati wameshindwa katika kipindi cha miaka zaidi ya hamsini. Watanzania
wamechoshwa na usanii. CCM wamebaki kugawana vyeo kindugu na kirafiki. Hawana
uchungu na nchi, wanachojali ni kiasi gani wataweza kuiba. Inabidi watanzania
wajitayarishe kuin’goa CCM madarakani kupitia sanduku la kura alisema Dr. Slaa.
Viongozi wa chuo kwenye picha ya pamoja na Dr. Slaa |
Dr. Slaa Akutana na viongozi wakuu wa mashirika ya Nishati
Meya pamoja na mkuu wa polisi nao walikuja kumuona Dr. Slaa na kumkaribisha kwenye jiji lao |
No comments:
Post a Comment