Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Monday, September 16, 2013

Tafakari ya Ya yaliyojiri Jumamosi Star TV: Ndugai Vs Mnyika


Pamoja na kwamba kumekuwa na mijadala mingi kuhusu kipindi kilichooneshwa Juzi Jumamosi Stat TV, bado naomba na mimi nichukue nafasi hii kuendeleza mjadala huu, kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo:

1. Hoja kwamba mitafaruku na migongano mingi hutokea bungeni na sio katika kamati. Ndugai alijenga hoja kwamba hii ni kwa sababu kuna Kamera bungeni wakati katika kamati hakuna kamera. hoja yake ni kuwa wapinzani, hasa CHADEMA, wanatumia nafasi hiyo ya kuonekana kwenye kamera, kufanya "vituko". Jibu la Mnyika: Kamati siyo chombo cha maamuzi ya mwisho. chombo cha maamuzi ya mwisho ni bunge. kwa mantiki hiyo, lazima kuwe na mtifuano katika hatua ya bunge kwa kuwa hapo ndipo muhimu zaidi. na kwa hiyo hata kama kusingekuwa na kamera, mtifuano ungetokea. kwa mawazo yangu, Hoja ya mnyika ni logical and sensible, hasa ukizingatia kwamba kuna maamuzi mengi ambayo inaonekana yanatetewa na wabunge wa CCM kufuta "pressure" kutoka CCM, na ambayo yanapingana na maslahi ya taifa kwa ujumla. mfano dhahiri ni huo muswada wa mabadiliko ya sheria ya katiba mpya ulioleta mzozo hivi karibuni.

2. Hoja kwamba inakuwaje mitafaruku mingi na vurugu hutokea anapokuwepo Mh. Ndugai. Hoja ya Ndugai hapa ilikuwa pengine watu wanamuona kuwa yeye nidhaifu, ndio maana wanafanya vurugu. Jibu la Mnyika: hapa Mnyika alishangilia kwa furaha kwamba hatimaye amepata jibu la swali ambalo limemsumbua siku nyingi. kumbe Mh. Ndugai ana tatizo la INFERIORITY COMPLEX! Hapo Ndugai alikuja juu sana na kufoka kwamba Mnyika amemtukana kumwambia kwamba ana INFERIORITY COMLPLEX!! Kwa maoni yangu, Ndugai hawezi kumlaumu Mnyika kwa kujenga hoja hii, kwa sababu "opening" aliitoa mwenyewe, Mnyika akapenyeza ngumi ikatua usoni. ngumi hiyo ni halali kabisa.

3. Hoja ya umri. Ndugai alirejea hoja hii mara kadhaa. katika taharuki yake pale Mnyika alipomwambia kwamba kwa kuwa amekiri kwamba ni dhaifu, basi ana INFERIORITY COMPLEX (inaleta maana hasa ukizingatia kwamba mara nyingi katika midahalo Ndugai hupandwa hasira. rejea kipindi cha ITV cha Kipima joto, Ndugai Vs Lissu), Ndugai alitoa kigezo kimoja cha umri, kwamba Mnyika anatakiwa kumheshimu Ndugai kwa kuwa amemzidi umri. na kuna wakati alikuwa anamjadili nadhani Mbowe, akasema kwamba ni mtu mzima wana rika moja. Mnyika hakutoa jibu la hoja hii moja kwa moja, lakini nitachangia. kwa kawaida hoja ya mantiki inatakiwa ijibiwe kwa hoja ya mantiki. tayari Ndugai alishafanya kosa la kuzungumzia uwezekano wa yeye kuonekana dhaifu. inawezekana subconscious yake ilikuwa ina-struggle kusema tu ukweli wake unaomsumbua muda mrefu. alipotapika ukweli huo mbele ya dogo Mnyika, na mbele ya hadhara ya ulimwengu mzima uliokuwa unamtazama, hapo hapakuwa na njia tena. hapo alitakiwa aoneshe umahiri wake wa kupindisha mwelekeo wa mjadala, kitu kigumu lakini inawezekana. kutumia kigezo cha umri ni hoja dhaifu sana katika mazingira yale, inaonesha kushindwa hoja.

4. Hoja ya Ndugai vs. Mbowe. kuhusu hili, hoja kubwa ya Ndugai ilikuwa kwamba kwa kuwa Mbowe aliposimama, Naibu Spika pia alisimama, kumwashiria Mbowe aketi, Mbowe alikiuka kanuni kwa kuendelea kusimama. Hii ni hoja nzito, imejikita kwenye kanuni. lakini najiuliza hivi: kanuni zimewekwa ili kuwezesha bunge lifanye kazi zake vizuri, kwa njia bora na inayohakikisha matokeo bora kwa maslahi ya taifa. Kanuni zinaweza kutumiwa kufunika au kukwamisha yale ambayo zimeundwa kuyalinda. kwa uzito wa mjadala ule, na kwa uzito wa Mh. Mbowe, Mh. Naibu Spika angeweza kabisa kuamua kumpa nafasi Mbowe azungumze. yeye aliamua kutompa nafasi hiyo. Ni nani analinda maslahi ya taifa hapo? Mantiki inatuelekeza kwamba katika suala la Katiba, kinachohitajika ni maridhiano zaidi kuliko ushindi wa walio wengi, busara na hekima zaidi kuliko kutimiza kanuni au kutumia fimbo ya kanuni. inaonekana hapa Ndugai ametumia fimbo ya kanuni kukidhi mahitaji ya kundi fulani katika jamii.

Hatima:

Kwa ujumla, Mnyika alijitokeza kama mpambanaji wa hali ya juu, anayetumia akili, na hekima zaidi kuliko umri wake, na hivyo kumzidi Ndugai ambaye alitaka kujenga hoja kwamba akili na hekima zikipungua, ongezea na idadi ya miaka ili uwe na akili na hekima nyingi zaidi!!

Mnyika, kwa wale ambao walikuwa wanasikitika kwamba LISSU hayupo, basi Ndugai leo anaserereka tu - wapi! dogo kamkomalia mpaka povu likamtoka Ndugai wa watu jamani! huruma?

Mindi/Jamii Forums

No comments: