Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, September 20, 2013

Balozi wa China: CCM inahusika, msajili wa vyama kimyaa!


Mkataba wa kimataifa wa Vienna wa mwaka 1961 unakataza Wanadiplomasia kujihusisha na mambo ya ndani ya nchi au taasisi wanazowakilisha. Sheria ya Tanzania ya mwaka 1986 ina akisi vienna kama chanzo chake. Balozi wa China amejihusisha na mambo ya ndani ya Tanzania na siasa za chama tawala akiwa katika vazi rasmi na kutoa kauli za kukiunga mkono Chama hicho katika mikutano ya hadhara. Balozi aliambatana na katibu mkuu wa CCM bwana Kinana na katibu wa uenezi wa CCM bw Nape Nnauye.

'Kelele' zilipopigwa Nape alitoka kwa mtindo wa kupotosha umma akisema Balozi alikuwa akifuatilia uwekezaji wa Pamba.  Nape,mwenyeji wa Balozi alipaswa kuwa kiongozi wa serikali na si chama na wala balozi hakupaswa kuvaa vazi la chama. Hakuna habari za serikali kumkaribisha balozi.Nape ni kijana wa kumpuuza kwasababu yupo tayari kwa tumbo lake hata kama kufanya hivyo ni dhalili kwake na maafa kwa taifa. Nape ni mfano mbovu wa vijana kupewa uongozi na vijana wa nchi hii wanapaswa kumlaani kila anpotokea hata kabla ya kunena. Mheshimiwa kinana haonekani kutumia uzoefu katika kulisaidia taifa. Jambo hili halipaswi kufanywa na mtu wa kiwango chake. Pengine ni hofu ya chama kufia mikononi ndiyo inamsukuma kufanya madudu haya ya aibu.

Waziri Membe amethibitisha balozi kukiuka taratibu za kimataifa na kitaifa.  Taarifa ya Membe ni ya ndumilakuwili kwani mwisho amemsifu kwa kazi nzuri ili kufunika uvunjaji sheria. Hatutegemei Membe kuchukua hatua nyingine zaidi ya taarifa hii ya kupooza hasira za Watanzania. Yote yametokea baada ya wananchi kuonyesha kutoridhika na ukikukwaji wa sheria za nchi na wakuu wa chama tawala kinachounda serikali iliyopo madarakani na inayopaswa kulinda sheria za nchi. Pamoja na harakati za kuutarifu ulimwengu kuna eneo muhimu linalohusika katika sakata hili.

CCM kimehusika kama chama cha kisiasa tena kwa uongozi wa juu wa chama. Tulitegemea msajili wa vyama vya siasa alione tatizo hili na kuchukua hatua stahiki. Hadi sasa pengine bado anatafakari.  Tunachukua fursa hii kumkukubusha kuwa kuna dalili za chama tawala kukiuka taratibu za vyama vya kisiasa kwa kumburuza balozi katika mikutano ya kisiasa huku CCM ikijua hilo ni kosa la kimataifa na kitaifa kwa sheria za nchi yetu. Upo uwezekano hakuna sheria ya msajili iliyokiuka. Muhimu ni kumtaka ajitokeza kufafanua kama kilichotokea kipo katika taratibu za uendeshaji wa vyama vya siasa au la.  Ufafanuzi ni muhimu na hana sababu zozote za kujificha kwasababu anaongozwa na sheria. 

Hili tunadhani ni muhimu kwa wakati huu na kwa uzito wa tatizo kiserikali na kichama. Endapo msajili atakaa kimya bila kutoa ufafanuzi basi tutamuomba aendelee kukaa kimya pale Alshabaab watakapokuwa na tawi na uhusianio na vyama vya siasa au taifa lingine litakapokuwa katika uhusiano wa kisiasa wa mambo ya ndani ya nchi na chama kingine. Tutamataka akae kimya na kuacha kila chama kitafute njia zake hata kama kufanya hivyo ni kuliangamiza taifa.

Nguruvi3/Jamii Forums




No comments: