Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Sunday, July 21, 2013

Wafanyabiashara `machinga` kuondolewa kuanzia kesho



         Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik, amesema zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama 'wamachinga' na ombaomba mitaani, litaanza kesho. 
Alisema wafanyabiashara hao ni pamoja na wale wenye ulemavu wa viungo na kwamba zoezi lina lengo la kuendeleza Jiji la Dar es Salaam kuwa katika hali ya usafi. Aidha, alisema ombaomba wote waliozagaa katikati ya mitaa ya Jiji watakusanywa na kurudishwa makwao. Sadik aliliambia gazeti hili jana kuwa uchunguzi uliofanywa na ofisi yake, umegundua kuwa ombaomba asilimia 90 wanatoka nje ya mkoa wa Dar es Saalam na asilimia 10 ni wa jijini ambao wanandugu wenye uwezo.

      “Tumeamua kuwarudisha ombaomba wote vijijini kwao," alisema. Aliongeza kuwa wamachinga wanaofanyabiashara katika maeneo yasiyo rasmi watapelekwa kwenye masoko rasmi waliyopangiwa. Alisema magari kwa ajili ya kuwasambaza wamachinga wanaofanyabiashara za vyakula na mbogamboga barabarani watapelekwa kwenye masoko ya vyakula, na wale wa bidhaa za madukani watatakiwa kukodisha fremu. Alisema ofisi yake imeandaa kikosi cha askari wa jiji na magari yatakayobeba bidhaa za machinga hao kwenye masoko waliyopangiwa. Sadik alisema kuwa lengo la zoezi hilo ni kuliweka jiji la Dar es Salaam katika hali ya usafi na kufanana na majiji mengine duniani yaliyokaa kibiashara.

        Alisema wageni kutoka nje ya nchi wana nia yakuja kuwekeza jijini na fursa hizo zipo kwa lengo la kuwanufaisha wananchi wote. Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umegundua kuwa baada ya ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama, Jiji la Dar es Salaam liliendelea kuwa katika hali yake ya uchafu baada ya wafanyabiashara hao kurudi kwa staili ya kuweka meza ndogo na kuuza vitu vidogovidogo, wakati wanaouza nguo huanza kazi yao majira ya saa 11 jioni. Maeneo ambayo NIPASHE ilishuhudia biashara hizo zikiendelea kama kawaida ni Mwenge, Mabibo Posta na Ubungo.

Source: Lusonzo M. (July 2013). Wafanyabiashara `machinga` kuondolewa kuanzia kesho Ippmedia/Nipashe

No comments: