Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, July 6, 2013

UFAFANUZI WA DR. SLAA IKILENGA POST HII - KUTOFAUTIANA KAULI KATI YA MBOWE NA SLAA


Kimsingi hatupaswi kupoteza muda kujibizana na Hamy-D. Wote tunajua hoja zake siku zote ni za upotoshwaji. Hamy Hakushindwa kuuliza a pate ufafanuzi kwa njia ya kawaida. Bila kurejea niliyosema kwenye threads nyingine,

I) akili ya Hammy ndiyo zilikofikia na kuishia. Hata mtoto wa darasa la pili ataona kuwa hakuna kupishana katika kauli ya Mbowe na ya Slaa.

2)Hammy angelikuwa na nia njema alitakiwa aulize mambo ya msingi a) mwaliko wa Mbowe ulifikishwa kwa njia gani, ofisi ya Chama au Ofisi ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ambayo kimsingi ni Ofisi ya Serikali. Kama Serikali ilitaka kumwalika Mbowe Kama Mwenyekiti wa Chama, haifahamu Ofisimya Mbowe Kama Mwenyekiti wa Chadema?

3)Hammy alitakiwa kuuliza Kama mwaliko wa Mbowe ulifikishwa ofisini kwake tarehe ngapi na saa ngapi! Kwa mtu yeyote mwenye akili na busara kabla hujafanya conclusion yeyote lazima ujiridhishe na facts zako na chronological order ya facts zako ili ufanye conclusion objective. Kwa manufaa ya wanaJF mwaliko wa Mgowe ulifikishwa majira ya saa 5 asubuhi siku ya Dinner, kupitia ofisi ya Kambi ya Upinzani.

4) Kama Hammy angelikuwa na dhamira safi hatua ya pili ni kuuliza Kama Mbowe alimshirikisha Dr Slaa kuhusiana na kushiriki kwake. Kama asingelimshirikisha, conclusion ingelikuwa sahihi.

Kwa Taarifa yenu;

mara baada ya kupata mwaliko Mhe. Mbowe alinishirikisha na kushauriana kuhusiana na kushiriki kwake. Tulikubaliana ashiriki kimsingi kwa kuwa kaalikwa Kama KUB, lakini pia hata taarifa yangu ya awali ilisisitiza kuwa hatujapata mwaliko. Busarabya Hammy ingelikuwa kuuliza je, tungelipata tungelienda au la.

Rejea kauli ya Dr Slaa, ambayo haikusema Chadema imesusia Bali "hatujapata mwaliko". Wrong premise produces wrong conclusion, a logical elementary philosophical principle. Lakini kwa kuwa mwaliko wa Mbowe ulifika siku mmoja baada ya Dr.Slaa kuhojiwa na vyombo vya habari, na kutoka kwenye magazeti asubuhi, kabla ya Mbowe kupata mwaliko, dhana ya kupingana inatokana wapi isipokuwa kwenye akili mgando yenye kutaka tu kuwaaminisha Watanzania kuwa Chadema kuna mgawanyiko, kuna kutofautiana.

Kwa vile asubuhi hiyo Mimi sikuhojiwa na gazeti lolote tena, na position ya Chama kimsingi ilibaki hivyo kuwa Chadema Kama Chama, Mtendaji Mkuu Ofisini kwangu sina Mwaliko wala wa Mwenyekiti wa Chama Wala wa Katibu Mkuu, sasa kupishana kunatoka wapi na katika nini. Moja anazungumzia Ng'ombe, mwingine, Punda.Kupishana kunatoka wapuuzi hapo. Unahitaji kwenda shule kugundua kuwa mmoja anaxungumzia ng'ombe na mwingine Punda.

Nadhani ufafanuzi huu unajitosheleza kwa wote wenye nia njema na kutaka kujua nini hasa kilitokea.

Imeandikwa na Dr. Slaa
Katibu mkuu CHADEMA

No comments: