Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Monday, October 14, 2013

Wenje awachokonoa Mkapa, Chenge


Wenje
   MBUNGE wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA), amemshukia vikali Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, akisema sera yake ya ubinafsishaji ilikuwa mbovu. 
Wenje aliongeza kuwa Mkapa ndiye aliyeleta umaskini kwa Watanzania na kusababisha uchumi wa nchi kuyumba. Mbunge huyo alitoa madai hayo juzi wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Igoma Stendi jijini Mwanza na kufungua matawi ya CHADEMA. Alisema licha ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kutounga mkono sera hiyo, lakini Mkapa alibinafsisha viwanda vya umma kwa wawekezaji, ambapo kwa sasa vingi vimekufa. Kwa mujibu wa Wenje, ubinafsishaji na kufa kwa viwanda vingi nchini umechangia kiwango kikubwa wananchi kukosa ajira, hivyo kujikuta wakiangukia kwenye biashara za uchuuzi na uendeshaji wa pikipiki zinazoua vijana wengi nchini.
Chenge

       “Sera ya Mkapa ya kubinafsisha viwanda imesababisha wananchi wengi kukosa ajira na nchi kuyumba kiuchumi. Maana viwanda vingi vilivyochukuliwa wa wawekezaji vimekufa na kubaki magodauni ya kutunzia mali za wawekezaji hao. “Kutokana na ukweli huo, ndiyo maana vijana wengi sana kwa sasa hivi wametumbukia kwenye biashara ya umachinga na kuendesha bodaboda. Na CHADEMA tunaomba mtupe nchi mwaka 2015 ili tuwakomboe na lindi la umaskini uliopo sasa,” alisema. Kuhusu fedha za rada, Wenje alimtuhumu pia aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), kwa madai kwamba ndiye aliyeliingizia taifa hasara kubwa kutokana na manunuzi ya kifisadi juu ya chombo hicho. Alisema kwamba manunuzi hayo ya kifisadi yalishtukiwa na Serikali ya Uingereza, hivyo kuamuru fedha zilizozidi zirudishwe nchini kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo, lakini fedha hizo hazijulikani zilipo kwa sasa.

     “Chenge na serikali ya CCM walifanya manunuzi ya kifisadi kuhusu rada. Yaani manunuzi hayo yaliishtua hadi Serikali ya Uingereza na kuhoji kwa nini Tanzania nchi maskini inunue rada kwa bei kubwa hivyo?”alihoji. Aidha, aliwaomba wananchi wa Nyamagana kujiandaa kuiangusha CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani, pamoja na uchaguzi mkuu 2015, kwani imeshindwa kuwaletea maendeleo wananchi wake. Hata hivyo, mbunge huyo Wenje aliwaahidi wananchi wa Kishili, Kata ya Igoma kushughulikia suala la umeme ili waweze kupata nishati hiyo kwa ajili ya maendeleo yao.

Source: Suma S. (Oct. 2013).Wenje awachokonoa Mkapa, Chenge. Retrieved from Tanzania Daima

No comments: