Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Wednesday, October 9, 2013

Dr. Slaa ndani ya Indianapolis Radio


Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Dr. Wilbrod Slaa, katibu mkuu wa Chadema amefanya mahojiano na radio ya Indianapolis ambayo ndiyo moja ya radio kubwa nchini marekani akisikilizwa na watu zaidi ya millioni 9 huku wengine wakishiriki kwenye mjadala kupitia mitandao ya jamii na simu moja kwa moja.

Kwa asilimia kubwa, wengi wamemkubali na kumuona kama mkombozi, siyo tu wa Tanzania, bali wa bara la Afrika kutokana na jinsi alivyojielezea na pia kuzungumzia mada mbalimbali hasa mikakati yake na chama chake Chadema kumuokoa mtanzania kutokana na ukoloni mamboleo ya CCM. Dr. Slaa amezungumzia kuhusu elimu, kilimo, afya, uwekezaji na fursa nchi zilizopo Tanzania.

Baadae mchana, Dr. Slaa atahojiwa na radio ya jijini Washington DC. Stay tuned...

Dr. Slaa akiongozwa

Dr. Slaa akijadiliana na Minority leader wa bunge la Indiana

Dr. Slaa akifurahia jambop ndani ya studio

Mchana huu atakuwa hapa;...

Dr. Slaa interview na Washington, D.C., U. S. A. Pacifica station WPFW 89.3 FM., Jumatano, Oct 9, 2013


Dr. Wilbroad Slaa amealikwa kwa mahojiano na WPFW Radio ya Washington, D.C., U.S.A. siku ya jumatano October 9, 2013. Saa saba mchana kwa saa za Amerika ya mashariki (1pm U.S Eastern time)/ Saa mbili usiku saa za Afrika mashariki (8pm East Africa time).

    Kumefanyika jitihada za kuushirikisha ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kushiriki mahojiano haya bila kuwa na mafanikio. Bado jitihada za kuushirikisha ubalozi zinafanyika mpaka hivi sasa.

Baadhi ya mambo yatakayo jadiliwa ni hali ya siasa Tanzania, hali ya kijamii, hali ya kiuchumi, amani na usalama wa Tanzania na mengineo.

Bofya hapa kusikiliza WPFW radio live WPFW Radio 

No comments: