Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, September 28, 2013

Ukweli wa Handeni kuhusu wanachama waliokihama CHADEMA


Taarifa zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na baadhi ya magezeti (Uhuru, Jambo leo, na Majira). Kuhusu kuhama kwa viongozi na wanachama wa chadema na hivyo kupelekea kufungwa kwa ofisi ya Chadema wilaya ya Handeni sio za kweli bali za kupikwa.

Mtakumbuka kuwa imekuwa kawaida ya ccm kusema na kuzusha uongo ili kuendelea kuhadaa watu kwa manufaa ya siasa nyepesi ili kukwepa kujibu au kutatua mambo mazito yanayo kabili jamii na taifa kwa ujumla.

UKWELI NI UPI

1. Shabani Ngido aliyetajwa kama katibu hakuwa katibu wala mwanachama wa Chadema, katibu halali wa Chadema wa wilaya ya Handeni anaitwa Ramia Ibrahimu Kisalazo anaishi Mkata umbali wa zaidi ya kilometa 20 kutoka Handeni mjini. Huyo Shabani Ngido alikuwa mwanachama wa ADC hakuwahi kuwa mwanachama wa Chadema.

2. Ni kweli mwenyekiti wa wilaya Bwana Lucas Elisa Selemani amehamia ccm kwa sababu anazojijua yeye moja kubwa ikiwa ni pamoja na kutishiwa kuchomewa tena nyumba. Alisha chomewa nyumba mara ya kwanza na wafuasi wa CCM.

3. Idadi ya wanachama zaidi ya 300 iliyo tolewa kuwa wamehama Chadema sio ya kweli na imejaa takwimu za uwongo. Wanachama walio kihama Chadema na kuhamia ccm haizidi 10, miongoni mwa hao kuna aliyetajwa kuwa alikuwa mwenyekiti wa Kabuku, hakuwa mwenyekiti bali mwanachama wa kawaida.

4. Baadhi ya wanachama wa ccm walipewa kadi bandia ili watakapo zirudisha ijenge taswira kuwa wanahandeni wameanza kuikataa Chadema, hili limefanyika kwenye ziara nyingi za mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ya ccm. Mfano ukiwa wilaya ya Hai ambako kadi na walioitwa wanachama wa Chadema zaidi 300 walitajwa kuwa wamerudisha kadi na kurejea ccm wakati ilikuwa ni uwongo.

5. Ccm walidiriki kununua bendera za chadema kati ya shilingi 20000 na 30000 ili zisipepe kwenye maeneo ambayo Bulembo alikuwa anapita au kwenda kufanya mikutano na kushindwa kujali na kutatua shida ya maji inayo ikumbuka wilaya ya Handeni kwa zaidi ya miaka 50 sasa.

Mwisho

CCM waache kufanya siasa nyepesi zenye ghiriba na kuhadaa wananchi, ni wakati wa wanahandeni kuungana pamoja kuendelea kufanya mabadiliko ya kukataa chama chenye serikali iliyoshindwa kuleta ya huduma ya maji.

Imetolewa na Mashuve Aroni

Mwenyekiti wa BAVICHA TANGA

0756 923 945

Source: Mtoi M. (Sept. 2013). Ukweli wa Handeni kuhusu wanachama waliokihama CHADEMA. Retrieved from Jamii Forums

No comments: