Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, September 3, 2013

‘Acheni itikadi mnapotoa maoni ya Katiba’


WAJUMBE wa baraza la katiba la mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Masasi mkoa wa Mtwara, wameshauriwa kuacha itikadi za kidini na kisiasa, wanapotoa maoni yao kuhusu maudhui yaliyomo kwenye rasimu ya Katiba. Ushauri huo ulitolewa hivi karibuni na Katibu Tawala wa wilaya ya Masasi, Yohana Miwa. Alisema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa siku tatu wa baraza la kujadili rasimu ya Katiba. Akizungumza katika ufunguzi wa baraza hilo, lililoandaliwa na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali wilayani Masasi (Mangonet) kwa ufadhili wa taasisi ya The Foundation For Civil Society, Miwa alisema rasimu hiyo ya Katiba ni ya kitaifa, haipaswi kuchukuliwa ya kidini.
        Alisema wajumbe wakifanikiwa kuweka kando itikadi zao za dini na za kisiasa, watafanikiwa kupata Katiba itakayokidhi maslahi ya Watanzania wote na taifa. Miwa alisema mikutano hiyo ya utoaji wa maoni ya rasimu ya Katiba, inapaswa kutumika kutoa maoni ya msingi yatakayo saidia kupata katiba iliyo bora kwa taifa na kupiga hatua mzuri ya maendeleo bila kuwepo kwa mivutano kuhusu dini ama siasa. Kwa mujibu wa Miwa, lengo la mikutano hiyo ya mabaraza ya utoaji wa maoni ya rasimu ya Katiba ni kutoa ushirikishwaji ili kupata katiba yenye maslahi na haki kwa ajili ya taifa na si chama cha siasa ama tasisi ya dini. Mwenyekiti wa Mangonet, Bernadetha Jumla alisema mkutano huo una lengo la kushirikisha jamii kuweka miundombinu na mifumo ya utawala bora na utawala wa sheria kuwa wa kidemokrasia na shirikishi.
      Alisema washiriki wa mkutano huo ni wawakilishi wa asasi za kiraia na asasi zisizo za kiserikali wilayani Masasi na watu wenye mahitaji maalumu wa jinsia zote na pia mkutano huo, utaongeza ufahamu wa wananchi kuhusu haki zao za msingi na uwajibikaji. “Mkutano huu ni mwanzo wa shughuli kubwa ya kuandika Katiba mpya shirikishi…tunategemea mchakato huu utaongeza idadi ya wananchi ya kujua haki zao za msingi…uwajibikaji…ushiriki wa shughuli za maendeleo hii itapunguza ama kuoandoa migogoro ya majukumu baina ya viongozi na wananchi,”alisema Jumla.
Source: Simba H. (Sep. 2013).‘Acheni itikadi mnapotoa maoni ya Katiba’.Retrieved from HabariLeo

No comments: