Tangu mapema
sana asubuhi, tumepokea simu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, watu tofauti,
wakionesha concerns zao juu ya taarifa kuwa ofisa mmoja wa Jeshi la Polisi
ameonekana kwenye picha 'akimdhibiti' Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willbroad
Slaa. Picha na
maelezo yake (caption) yameonekana kuwasononesha na kuwatisha watu wengi. Ili kusaidia
jamii na kuepusha madhara makubwa yanayoweza kutokea, iwapo usahihi wa tukio
hilo hautaelezwa, tumeona ni vyema kwa nafasi yetu kuweka kumbukumbu sawa.
USAHIHI;
Kama ilivyo ada ya misafara ya CHADEMA, hasa inapohusisha viongozi wakuu,
viongozi (watendaji waandamizi) wengine wa kitaifa, wabunge na viongozi wengine
wa chama katika maeneo husika, huwa ina hamasa, shamrashamra na mapokezi
makubwa kila mahali kunapofanyika mikutano au shughuli ya kichama.
Katibu Mkuu,
Dkt. Slaa na timu yake walipotua Mpwapwa kwa helkopta siku ya Agosti 18, mwaka
huu, alilakiwa na umati mkubwa wa watu, wakitaka kumsalimia na kumkumbatia.
Wakifurahia ujio wa mmoja wa viongozi wakuu wa chama katika eneo lao, kwa ajili
ya kuendesha Mabaraza Huru ya Rasimu ya Katiba Mpya, katike eneo hilo.
Katika hali
kama hiyo, walinzi, wakiwemo askari polisi, walikuwa 'concerned' na hali ya
usalama, maana 'lolote' laweza kutokea. Ofisa wa Polisi anayeonekana kwenye
picha, alikuwa akiwaelekeza watu wasogee pembeni kwanza, akimwambia Daktari
asubiri kidogo watengeneze njia 'vizuri' apite, maana watu wote wale kumfuata
na kumkumbatia ingeweza kuwa hatari.
Kama
anavyoonekana, Dkt. Slaa naye alikuwa akijaribu kumwambia yule askari kuwa
awasaidie wale watu bila kuharibu utaratibu wa yeye kusalimiana na wananchi
wake, ambao hujaa kumlaki kwa nia njema, bila kukodiwa wala kusombwa. Hivyo ndivyo
ilivyokuwa. Hakukuwa na 'kudhibitiana', bali kulikuwa na kuongozana.
Timu ya
Katibu Mkuu, kama ilivyo kwa Mwenyekiti Freeman Mbowe, kwa kutumia usafiri wa
chopa, inaendelea na ratiba ya kuendesha Mabaraza Huru ya Rasimu ya Katiba
Mpya, ambapo muda huu timu ya Mwenyekiti imeshaingia Mkoa wa Katavi, kutokea
Tabora na timu ya Dkt. Slaa iko Morogoro! Maelfu ya
Watanzania wanaendelea kupata fursa ya kushiriki moja kwa moja, kutoa maoni yao
kwenye mabaraza hayo, yanayoendeshwa kwa njia ya wazi kwenye mikutano ya
hadhara.
Nawe unaweza
kuungana na maelfu hao wanaotumia fursa ya mikutano, kwa kutoa maoni yako ya
katiba, kwenye Mabaraza Huru ya Rasimu ya Katiba Mpya, kupitia ujumbe mfupi
kwenye namba
0789 248224
email;
chademamaoni@gmail.com
Asanteni.
No comments:
Post a Comment