Mbunge wa Nzega Hamis Kigwangalla amesema hawezi kumpa kura yake Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli Mheshimiwa Edward Lowassa endapo jina lake litajitokeza kama mmoja ya wagombea urais, ni kauli ya Kigwangalla akijibu swali aliloulizwa na Mtangazaji Fina Mango katika kipindi cha Makutano kuhusu vuguvugu la urais 2015 linaloendelea ndani ya CCM juu ya mgombea urais ambapo Edward Lowassa ni kati ya wanaotajwa sana kama wagombea hasa katika mitandao ya kijamii.
“Sitompa
kura Mheshimiwa Edward Lowassa kwa sababu za msingi tu, kwamba ninakipenda
chama changu na nina hakika chama changu kikija na mgombea kwenye uchaguzi mkuu
2015 ambaye ana historia ya kuhusishwa na mambo machafu kama yale ya Richmond,
Dowans ambayo unayasema, hapa tunaweza kupata tabu sana kuomba kura kwa
wananchi, lakini pia tutakuwa tumewapa hoja wapinzani wetu ya kusema tunalea
ufisadi, tunaubembeleza ufisadi kwa mikono miwili’ Kigwangalla
Kwenye
sentensi nyingine Kigwangalla amesema Tanzania aihitaji rais asiyeweza
kusimamia ukweli ambapo kuhusu ishu ya dowans amesema haoni tatizo la mitambo
hiyo isipokuwa uamuzi uliotumika katika upatikanaji wake. Kwenye
hii interview, Kigwangalla alitangaza nia ya kugombea urais mwaka 2025 na
kusema 2015 anaona bado ni mapema kwake kwani anaamini watanzania bado
hawajamjua Hamis Kigwangalla ni mtu wa aina gani.
No comments:
Post a Comment