Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, August 20, 2013

CCM Inaweza “Kujivua Gamba”?

    Na Ashakh (Kiongozi)
Ikumbukwe miaka miwili nyuma ndani ya chama tawala CCM kuliibuka kundi lenye mzozo na kundi jengine kuputia dhana na kauli mbiu ya “Kujiva Gamba”. Kauli hii ilitokana na lile kundi la viongozi waliojiona kuwa ni wasafi mbele ya kundi la viongozi walioshukiwa kujihusisha na mambo rushwa. Uhasama ukajengeka miongoni mwao hivyo kutakiwa wale wote wanaojihusha na vitendo vya ufisadi kujchukuliwa hatua ya kuvuliwa nyadhifa za uongozi na kufukuzwa uanachama.

       Kama vile unayebeba kilo 100 za usufi, dhana ya kujivua gamba ndani ya CCm haikuweza kutekelezwa. Licha ya kuonekana wepesi wake, ugumu ulikuwa umezidi na kuumiza migogo ya viongozi na wale wote walizaa dhana hii. Leo hii fununu zimetanda kutaka utekelezaji wa dhana ile, kwa baadhi ya viongozi wa CCM Zanzibar kupendekeza baadhi ya wananchama wao wavuliwe gamba. Tofauti kidogo sababu kuu ya kuvuliwa gamba na pale mwanzo. Mara hii ni kwa wale wanachama waliotumia fursa ya kuwataka Watanzania wote washiriki na watowe maoni yao katika upatikanaji wa katiba mpya ya Tanzania.

       Hii ni aibu, kwani kama mwananchi wa Tanzania bila ya kujali itikadi ya chama, kutoa maoni ni haki ya kila mtu kwa mujibu wa sheria. Vipi leo kuwe na fukutu la kufukuzwa uanachama kwasababu tu mawazo yako yako kinyume na mawazo ya wengine. Hivi kweli CCM inaweza kujivua gamba? Vipi kwa wale wengine waliokuwa na mawazo sawa na wanachama wanaofukuzwa uanachama. Tukichukulia mifano kama vile Jaji Joseph Warioba, Dr Salim Ahmed Salim, Mzee Hassan Nassor Moyo, na wengineo wote hawa ni CCM nao hawakubaliani na Ilani ya CCM kupatikana katiba mya, jee na wao watafukuzwa uanachama?

Yataka ujasiri “Kujivua Gamba”


No comments: