Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, March 29, 2013

Viongozi watano wa CHADEMA washtakiwa kwa kufanya fujo


Viongozi watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kata ya Ulemo wilayani Iramba, wamefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Kiomboi kujibu shitaka la kufanya fujo mkutanoni. Viongozi hao ni Mwenyekiti wa kata wa chama hicho, John Wilfred (22), Katibu wa vijana wa kata, Kitila Gabriel (20), Mwenyekiti wa kata, Emmanuel Reuben (27), Katibu mwenezi, Christopher Edso Shilla (33) na mwanachama Kephasi Cyprian (35). Mlalamikaji katika kesi hiyo ni Mwenyekiti wa kijiji cha Ulemo, Milton Nazael.

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, washtakiwa wanadaiwa kufanya kosa hilo Machi 8, mwaka huu saa 5:15 asubuhi katika kijiji cha Ulemo wilayani Iramba. Ilidaiwa kuwa siku hiyo ya tukio, washtakiwa kwa pamoja, wakati mkutano uliokuwa ukiongozwa na Mwenyekiti huyo wa kijiji, bila halali na kwa makusudi, walifanya fujo na kusababisha mkutano huo ushindwe kuendelea kama ulivyopangwa.

Hata hivyo, washtakiwa hao walikana mashitaka hayo na wapo nje kwa dhamana ya Sh. 200,000 kila mmoja za maandishi hadi Aprili 4, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Source:  Ismailly j. (March 2013). Viongozi watano wa Chadema washtakiwa kwa kufanya fujo. Retrieved from Ippmedia/Nipashe

No comments: