Jeshi la
Polisi mkoani Dar es Salaam kanda ya Kinondoni limekataza maandamano yaliyokuwa
yamepangwa kufanyika tarehe 16 Machi 2013 yaliyokuwa yameiratibiwa na
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika yaliyolenga kufika katika Wizara ya Maji ili
kufikisha ujumbe kwa Waziri wa Maji, Prof Maghembe kuhusu kero ya maji katika
jimbo hilo ambayo haijatatuliwa wala kupatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu. Kamanda
wa Polisi wa kanda hiyo ACP, Charles Kenyela amesema endapo maandamano hayo
yatafanyika:
1.
Upo wasiwasi wa kutokea kwa vurugu pale watakaposhindwa
kufikia muafaka kuhusu hoja zao.
2.
Amewasiliana na Ofisi ya Waziri husika na kufahamishwa
kuwa haina taarifa rasmi za ujio wa maandamano hayo.
3.
Barabara yatakakopita maandamano hayo ipo katika ujenzi
na hivyo maandamano hayo yatazuia shughuli za mkandarasi kukamilisha kazi yake
kwa wakati na kuisababishia Serikali hasara.
4.
Eneo ambamo maandamano hayo yanakusudiwa kutamatia ni dogo
na hivyo itasababisha usumbufu mkubwa.
Source: Wavuti. (March 14, 2013). Polisi yazuia maandamano ya maji Ubungo. Retrieved from Wavuti
No comments:
Post a Comment