CHADEMA
YAZUNGUMZIA KUKAMATWA KWA LWAKATWARE
Katibu Mkuu
wa CHADEMA, Dk Slaa amezungumza na wanahabari (video imepachikwa hapo chini)
kuhusiana na tukio la jana la kiongozi mmoja wa chama hicho, Wilfred Lwakatware
kuwekwa chini ya ulinzi wa Polisi tokea jana kwa ajili ya mahojiano ya
kiuchunguzi. Slaa akasema CHADEMA inalitaka jeshi la polisi kufanya
uchunguzi wake kuhusiana na suala hilo bila kufuata mrengo wa kisiasa. Slaa pia
amesema CHADEMA inashangazwa na hatua iliyochukuliwa na Jeshi hilo
kumkamata Lwakatare kwa kuona video il hali zikiwapo taarifa nyingi za
uchochezi ambazo wasemaji wake hawajachukuliwa hatua. Akasema haamini kama
Lwakatare anaweza kupanga mipango ya kufanya uvunjifu wa amani. Pia
amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakipeleka malalamiko yao na vielelezo
mbalimbali polisi kuhusu kuhujumiwa lakini hadi sasa hakuna uchunguzi
uliofanywa na Jeshi hilo.
Source: Wavuti. (March 14, 2013). CHADEMA yazungumzia kukamatwa kwa Lwakatware. Retrieved from Wavuti
No comments:
Post a Comment