MAELEZO KWA WANAHABARI KUHUSU MAAMUZI
YA MKUTANO MAALUM WA BARAZA KUU LA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) ULIOFANYIKA TAREHE 28 JANUARI 2013
KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE JIJINI DAR ES SALAAM
Baraza
Kuu la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) limefanya mkutano wake
maalum tarehe 28 Januari 2013 katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es
salaam ambao ulikuwa na ajenda zifuatazo: Maoni na Mapendekezo kuhusu Maudhui
na mchakato wa katiba mpya; Mapendekezo ya Haja ya kufanya marekebisho katika
kanuni za chama na kutunga muongozo; Mpango Kazi, Mkakati na mwendelezo wa
Operesheni ya M4C na Bajeti ya chama kwa mwaka 2013 na mengineyo.
Baraza
kuu limefanya maamuzi mbalimbali; katika hatua ya sasa tunatoa taarifa kwa umma
kuhusu maazimio yafuatayo:
Maoni na Mapendekezo kuhusu Maudhui na
mchakato wa katiba mpya
Baraza
Kuu limepokea na kuridhia taarifa ya kamati kuu kuhusu maoni na mapendekezo ya
chama kuhusu maudhui na mchakato wa katiba mpya. Baraza Kuu limezingatia kuwa
katika mpya bora ni nyezo muhimu ya ufumbuzi wa matatizo ya kiongozi na
migogoro inayolikabili taifa ikiwemo kuhusu rasilimali za nchi. Taarifa ya
maamuzi ya Baraza Kuu kuu juu ya hatua zitazochukuliwa kuhusu maudhui na
mchakato wa katiba mpya itatolewa kwa umma.
Kwa
sasa umma ufahamu kwamba kati ya maamuzi hayo ni pamoja na kuridhia kwamba
katika ya masuala ambayo CHADEMA itahamasisha umma kuikataa katiba mpya iwapo
hayataingizwa ni pamoja na Katiba kutambua kwamba Wananchi ndio wamiliki wa
rasilimali asilia za maeneo wanakoishi Kama vile ardhi, madini, mafuta, gesi
asilia, misitu/wanyama pori na rasilimali uvuvi na kwamba jukumu la Serikali ni
kuwezesha Wananchi wa maeneo husika kunufaika na umilikaji huo wa rasilimali
asilia.
CHADEMA
imetaka katiba mpya iwe na vifungu vya kuhakisha kuwa wananchi
hawatanyang'anywa rasilimali zao asilia na mamlaka za Serikali matumizi na watu
au taasisi nyingine ya rasilimali asilia za Wananchi bila kwanza Wananchi
watakaoathiriwa na unyang'anyi au matumizi hayo kutoa ridhaa yao baada ya kupatiwa
taarifa zote na kamili zinazohusu matumizi yanayotarajiwa ya rasilimali hizo na
athari za matumizi hayo kwa mazingira, kiuchumi na kijamii (the right of prior
informed consent).
Katiba mpya ihakikishe wananchi, Kama wamiliki wa msingi wa rasilimali asilia, watakuwa na haki ya kulipwa mrahaba kwa ajili ya matumizi ya watu au taasisi nyingine ya rasilimali asilia za Wananchi, wakati mamlaka za Serikali za mitaa, Majimbo na Serikali Kuu zitakuwa na haki ya kutoza kodi mapato yatakayotokana na matumizi ya rasilimali hizo.
Baraza Kuu limezingatia kuwa katiba ya sasa inatambua haki ya kumiliki mali na hifadhi ya mali hiyo na inakataza unyang'anyi wa mali kwa lengo la kuitaifisha au kwa malengo mengine, haki za wananchi kumiliki rasilimali zao za asilia kama ardhi, madini, mafuta, gesi asilia, misitu na wanyama pori, uvuvi, n.k., zimekuwa haziheshimiwi na mamlaka za kiserikali kwa hoja kwamba rasilimali asilia hizo ni mali ya umma.
Baraza Kuu limeelezwa kwamba dhana ya mali ya umma ni dhana yenye asili yake katika ukoloni. Ni dola ya kikoloni ya Kijerumani ndio ilikuwa ya kwanza kutangaza kwamba mali asilia zote katika koloni lao la Tanganyika ni mali ya Mfalme wa Kijerumani. Baada ya Wajerumani kushindwa Vita ya Kwanza ya Dunia na kunyang'anywa makoloni yao ya Afrika, dola ya kikoloni ya Waingereza iliyokabidhiwa Tanganyika, walitangaza kwamba rasilimali asilia zote ni mali ya umma chini ya mamlaka na udhibiti wa Gavana wa kikoloni. Dhana hii ilipokelewa bila mabadiliko yoyote ya msingi baada ya uhuru na ndio imekuwa msingi mkuu wa sera za rasilimali asilia za nchi yetu chini ya utawala wa Serikali inayoongozwa na CCM na kusababisha migogoro katika maeneo mengi nchini na kama ilivyo sasa huko Mtwara.
Kwa
kuzingatia misingi hiyo, Baraza Kuu limeridhia msimamo wa Kamati Kuu kuhusu
mgogoro wa gesi Mtwara kwamba tunataka wananchi wasikilizwe na serikali
isimamishe mchakato wa kuvuna gesi ya Mtwara hadi itakapokuwa imetekeleza
yafuatao: Iweke wazi mikataba yote ya utafutaji na uvunaji wa gesi ili wananchi
wajue kama mikataba hiyo inalinda maslahi yao (ifahamike kwamba viongozi wa CCM
na CCM kama chama kijinufaisha moja kwa moja na sehemu ya mikataba hiyo) ;
waone jinsi wanavyonufaika na raslimali hiyo; Iweke wazi mikataba yote ya
ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, ili wananchi wajue
gesi hiyo inapelekwa wapi na kwa madhumuni gani; Ieleze kwanini haitaki kujenga
vinu vya vya kufua umeme kwa kutumia gesi pale Mnazi Bay Mtwara, na kuingiza
umeme wa 300 MW katika gridi ya taifa (CCM ijieleze kwa kushindwa kutekeleza
ilani yake kuhusu ahadi hii) ; Iseme kwanini haiwezi kujenga mitambo ya kufua
gesi Mtwara, na badala yake inang’ang’ania kujenga mabomba ya kupeleka gesi
Bagamoyo na Dar es Salaam; na ieleze wananchi wa Mtwara na mikoa ya Kusini
watafaidikaje na bomba linalopeleka gesi Bagamoyo.
Mapendekezo ya Haja ya kufanya
marekebisho katika kanuni za chama na kutunga muongozo:
Baraza
Kuu limefanya kwa mujibu wa mamlaka yake ya ibara ya 7.7.13 (i) ya kupokea
mapendekezo na kuridhia haja ya kufanyia marekebisho ya kanuni za chama na
kutunga muongozo.
Kati
ya maeneo ya kanuni yaliyopendekezwa kufanyiwa marekebisho ni pamoja kuweka
utaratibu wa wajibu na mipaka ya mbunge wa viti maalum kuondoa migongano na
wabunge wa majimbo, kuweka utaratibu wa kuchukua hatua za kinadhamu mapema
katika masuala yenye kuhitaji hatua za haraka kwa maslahi ya chama na
taifa, na mipaka ya wenza wa viongozi
kwenye ushiriki wao katika shughuli za chama na nidhamu kuhusu muda wa
mikutano.
Aidha,
Baraza kuu limeridhia kuandaliwa kwa muongozo kuhusu utaratibu wa kutangaza
kusudio la kugombea nafasi za uongozi kwenye chama na katika chaguzi za
kiserikali kuanzia ngazi za kitongoji, kijiji/mtaa, udiwani, ubunge na urais.
Mpango Kazi, mwendelezo wa Operesheni
ya M4C, ratiba ya uchaguzi na Bajeti ya chama ya 2013:
Baraza
Kuu limepitisha Mpango Kazi, Mwendelezo wa Operesheni ya M4C, ratiba ya
uchaguzi wa ndani wa chama na bajeti ya chama kwa mwaka 2013.
Baraza
Kuu limezingatia kwamba matatizo yanayoikabili nchi kwa sasa ikiwemo migogoro
mbalimbali na matokeo ya sera mbovu na udhaifu wa kiuongozi wa CCM na Serikali
yake; hivyo CHADEMA kwa itaendelea kuwaongoza wananchi kuiwajibisha Serikali
mwaka 2013, kueneza sera sahihi za CHADEMA na kuwaunganisha wananchi kuiondoa
CCM madarakani katika chaguzi zinazokuja mwaka 2014 na 2015.
Kwa
kuzingatia Ibara ya 3.A ya Katiba ya chama, Baraza Kuu limesisitiza falsafa ya
chama ya “nguvu ya umma” katika kuongoza utekelezaji wa Mpango kazi kwa mwaka
2013 ya kwamba umma ndiyo wenye mamlaka ya mwanzo na mwisho katika kuamua hatma
ya taifa na katika kumiliki na kuendeleza mawazo, maamuzi, rasilimali, uchumi
na siasa za nchi.
Baraza
Kuu limepitisha utaratibu wa mfumo wa utendaji wa kanda kwa kuzingatia misingi
ya ‘sera ya majimbo’ na kwa kurejea katiba ya chama ibara ya 7.6 ili kugatua
(decentralize) mfumo wa upangaji na utekelezaji wa shughuli za ujenzi wa chama
kupitia operesheni za M4C.
Baraza
Kuu limepitisha ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama ifuatayo: Uchaguzi wa
misingi, matawi, majimbo na wilaya (Aprili mpaka Septemba 2013 kupitia
Operesheni za M4C kwa kila kanda); Chaguzi za Mikoa (Novemba 2013); Uchaguzi ngazi ya taifa ( Desemba 2013, Tarehe 11
BAWACHA, 12 BAVICHA na Wazee, 13 Kamati Kuu, 14 Baraza Kuu, 15 Mkutano Mkuu, 16
Baraza Kuu Jipya, 17 Kamati Kuu Mpya).
Imetolewa
tarehe 29 Januari 2013 na:
John
Mnyika (Mb)
Mkurugenzi
wa Habari na Uenezi
No comments:
Post a Comment