Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Wednesday, July 1, 2015

CUF YALAANI KUVAMIWA COCONUT FM



Chama Cha Wananchi (CUF), kimelaani vikali kitendo cha kuvamiwa kituo cha redio cha Coconut FM mjii Unguja na kumtisha mwandishi wa khabari Ali Mohammed wa kituo hicho.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya khabari ambayo Swahilivilla imeipata nakala yake, CUF imesema kuwa kikundi cha watu wapatao 20 wanaosadikiwa kuwa ni askari wa vikosi vya SMZ kilivamia kituo cha Coconut FM kilichoko katika mtaa wa Kilimani mjini Unguja mnamo tarehe 29 Juni, 2015 na kumtisha mwandishi Ali Mohammed kwa sababu ya kuandaa kipindi maalum kilichokuwa kinajadili hali ya vitisho inayoendelea katika uandikishaji wa wapiga kura.

Katika taarifa hiyo iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano na Umma Bwana Ismail Jussa, CUF imesema kuwa tukio hili ambalo limefanywa na askari hao wakiwa wamejifunika nyuso zao  huku wakiwa na silaha za bunduki za SMG, mapanga, marungu, na msumeno wa kukatia miti  wakitumia gari zenye namba za vikosi vya SMZ ni muendelezo wa vitendo vya kukamata, vitisho vya aina mbalimbali na udhalilishaji dhidi ya wananchi  ambavyo vilianza pale uandikishaji wa wapiga kura ulipoanza katika kisiwa cha Unguja.

"Kitendo cha kuvamia COCONUT FM na kumtisha mwandishi Ali Mohamed na wafanyakazi wengine ni kitendo kinacholenga kuvinyamazisha vyombo vya habari na waandishi wa habari ili waogope kuanika uovu unaofanywa na vikundi hivyo katika jamii", ilisema taarifa hiyo na kuongeza kuwa kitendo hicho kinapaswa kulaaniwa na wapenda amani wote, watetezi wa haki za binadamu na kila anayeamini katika Utawala bora.

Katika taarifa yake hiyo, CUF imeelezea masikitiko yake kwa Jeshi la Polisi kwa kushindwa kuchukua hatua yoyote ya kuzuia vitendo hivyo vya uonevu, na kusema kuwa chombo hicho chenye jukumu la kuhakikisha usalama wa raia na mali zao kimekuwa kikikimbia majukumu yake.

"Hali hii imeleta taharuki kwa wananchi wa Zanzibar ambao wengi wao wakiwa ni Waislamu wanaendelea na mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani huku wakiwa wanakosa amani na utulivu hata wa kufanya ibada zao", ilmeeleza taarifa ya CUF na kuendelea kusema kuwa haikutegeme fujo hizi kutokea baada ya Maridhiano  ya mwaka 2009 amabyo yalileta maelewano ya kisiasa visiwani Zanzibar.

Kufuatia hujuma hizo, CUF imewataka Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed  Shein na Rais wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete kuchukuwa hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa hali ya utulivu na usalama vinarejea Zanziba kama ilivyoachwa na Rais mstaafu wa Zanzibar Dk Amani Karume mwaka 2010. Aidha, imewaataka viongozi hao kuhakikisha kuwa wale wote waliohusika katika vitendo hivyo vya uvunjaji amani, wanawajibishwa akiwemo Waziri anayehusika na Vikozi Vya SMZ Bwana Haji Omar Kheri.


Chama Cha Wananchi, pia kimetoa wito wa kuundwa Tume huru ya uchunguzi juu ya vitendo hvyo vya uvunjaji wa amani itakayoyashirikisha mashirika ya Kimataifa, na kuitaka Jumuiya ya Kimataifa kufuatilia kwa karibu mwenendo wa matukio Visiwani Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

No comments: