Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, January 14, 2014

Mdee: Mgogoro wa ardhi Mbarali haujamalizika


WAZIRI Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee, amesema mgogoro wa ardhi katika Shamba la Kapunga wilayani Mbarali, mkoani Mbeya bado haujamalizika na kuitaka Serikali ichukue hatua za haraka. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam jana, ilisema kuna dalili za wazi kuwa Serikali imeshindwa kutimiza wajibu wake pamoja na ahadi iliyotoa bungeni ya kuutatua na kuwarudishia wanakijiji eneo lao.

 Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe (CHADEMA), alisema mgogoro huo ambao ni wa muda mrefu, unathibitisha namna ambavyo sera ya kusimamia ardhi ilivyoshindwa kusaidia wananchi.

  “Mgogoro wa Kapunga ambao umedumu kwa miaka mingi sasa, unatokana na athari za kutekeleza sera za uwekezaji na ubinafsishaji bila kuzingatia maslahi ya wananchi, ni mwendelezo wa kushindwa kwa Serikali ya CCM, kusimamia suala nyeti la ardhi na sasa umetudhihirishia pasipo kificho kuwa kuna tatizo kubwa la kiungozi.



“Namshauri Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka asianzishe kitu kipya kinyume na kauli ya Serikali hii ambayo yeye ni waziri. 

Katika taarifa hiyo, Mdee alisema Serikali kupitia kwa Waziri wa Kilimo na Chakula, Mhandisi Christopher Chiza ilitoa ahadi bungeni tangu mwaka 2009 na 2011, ili kumaliza mgogoro wa ardhi katika Shamba la Kapunga, Serikali inamalizia taratibu za kurekebisha hati ili mwekezaji abakie na eneo linalomstahili na wanakijiji warudishiwe eneo lao.

 Mdee, alitoa tahadhari kwa Serikali kuwa makini na migogoro ya ardhi, ambayo katika miaka ya karibuni imeanza kugharimu damu na maisha ya Watanzania.

 “Serikali kupitia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, watuambie wanataka watu wangapi wafe, ili washtuke na kumaliza migogoro katika maeneo mbalimbali nchini? 

Migogoro kama ile ya Kiteto, Kapunga, Mvomero, Mtibwa, Malinyi, Kilombero, ilipaswa kuwashtua watawala na kuhakikisha hatua stahili za kulinda haki za Watanzania katika ardhi zinalindwa.

Source: Mtanzania (Jan. 2014).Mdee: Mgogoro wa ardhi Mbarali haujamalizika. Retrieved from Mtanzania

No comments: