Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, December 31, 2013

NEWS ALERT: Wachina wakamatwa na Shehena ya Meno ya Tembo Bandarini Dar

Kuna Wachina wamekamatwa na Shehena Kubwa ya Meno ya tembo Bandarini Dar es Salaam na sasa wamechukuliwa kisiri na "watu flani" ambao hawataki habari hii ijulikane.

Ilikuwa ni meli ya kijeshi ya China ambayo ilikuwa imeegesha gati namba 3 baada ya kuwa nchini katika shughuli za kawaida za ushirikiano katika kudhibiti maharamia (Pirates). Katika kuuficha mzigo kwa kudai magari yamebeba chakula ndipo wakashtukiwa.

Chanzo chetu kinatufahamisha kuwa Wametiwa pingu na wanajeshi wa JWTZ na TISS na wamepelekwa Ukonga na msafara wa magari mawili yakiongozwa na pikipiki za Polisi.

Hata walipo tuna chanzo chetu ambacho kitaendelea kutujuza kinachojiri.

Namna yoyote ya kuzima huu ujangili italeta balaa kubwa si kwa vyombo vya dola tu bali hata kuitia doa serikali kwa ujumla. Msifiche, waanike ili waueleze umma nani yupo nyuma yao!

KUTOKA CHANZO CHETU - WAJARIBU KUHONGA 25 MILLION, WAKUTWA NA TANZANITE PIA!:

Sakata la Wachina na kukutwa na Nyara za Serikali limeendelea kuchukua sura mpya ambapo Wachina wawili walifika bandarini wakitaka kuwasailimia ndugu zao ambao ni Wanajeshi.

Walipofika getini, kwakuwa tayari wanajeshi wa JWTZ waliishaimarisha ulinzi baada ya tukio la jana yake (usiku wa kuamkia leo) na meno ya tembo. Wanajeshi walitaka kuwakagua Wachina hao wakagoma na ndipo wakapekuliwa kwa lazima na kukutwa na madini aina ya Tanzanite. Wakaitwa maofisa wa Nishati na Madini na polisi wakawachukua!

Tukio la awali lilikuwa la jana Jumatatu saa 3 usiku wa kuamkia Jumanne (leo) ambapo gari moja binafsi likisindikizwa na gari la Polisi na mtu mmoja mwenye sare za Polisi lilifika katika lango la bandari eneo la geti namba 2 wakielekea geti namba 3 iliko meli ya kijeshi ya Kichina yenye wanajeshi takribani 600.

Katika gari la kiraia kulikuwa na Wachina watatu; wawili wanajeshi na mmoja raia na dereva Mtanzania.

WACHINA walitaka kuwapa walinzi rushwa ya sh milioni 25 baada ya walinzi kukuta kuna vipande 81 vya meno ya tembo.

Walinzi waligoma na kulazimisha kulikagua gari. Kuona hivyo gari la Polisi na mtu aliyevaa sare za polisi wakatoweka na wale wanajeshi wawili wa Kichina wakatoweka na kukimbilia katika meli yao ya kijeshi na kujichanganya na wenzao.

Ndipo walinzi walipowasiliana na wanajeshi na Polisi na wakaja wanajeshi na maofisa Usalama wa Taifa wa Tanzania ambao waliwachukua Mchina na dereva Mtanzania na kuondoka nao.

Tunaendelea kufuatilia zaidi kuwafahamisha kinachojiri


 Invisible/JF

No comments: