Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Thursday, December 5, 2013

DKT. Slaa ziarani; mikutano ya Desemba 5, Kakonko, Kigoma



Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa ameendelea na ziara yake, ambapo Desemba 5 aliingia Mkoa wa Kigoma akianzia wilayani Kakonko, moja ya wilaya mpya zilizoanzishwa hivi karibuni, kwa kufanya mikutano miwili, kijijini Muhange, Kata ya Muhange, kisha akamalizia Kakonko mjini Uwanja wa Mwenge.

Katibu Mkuu Dkt. Slaa amendelea kupata mapokezi yenye ukarimu mkubwa kutoka kwa wenyeji ambao wengi wao wamekuwa na hamu ya ugeni mzito wa chama. Wilaya ya Kakonko kwa mwaka huu pekee imekuwa na bahati njema kweli kweli kwa kupokea ugeni mzito wa kitaifa mara mbili.

Timu ya Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe, akiwa na Mwanasheria Mkuu wa Chama Tundu Lissu na Mkurugenzi wa Mawasiliano John John Mnyika ilifanya mkutano wa mabaraza ya wazi ya maoni ya rasimu ya katiba mpya mwaka huu. Halikadhalika wakati wa kampeni za mwaka 2010 aliyekuwa mgombea urais, Dkt. Slaa alitua katika eneo ambalo leo ndiyo makao makuu ya wilaya hiyo mpya.

Katika mkutano wake wa kwanza Kijiji cha Muhange, Kata ya Muhange (ambayo inaongozwa na diwani wa CHADEMA), Dkt. Slaa alizungumzia baadhi ya kero zinazowasumbua wananchi wa maeneo hayo, hususan wakulima wa kahawa, walioathirika na operesheni za kuondoa wahamiaji haramu na tokomeza ujangili, ambako watu wameteswa sana na vyombo vya dola.

Alisema kuwa kwa muda mrefu sasa ofisini kwake kuna malalamiko mengi kutoka kwa viongozi wake wa chama, hususan kutoka wilaya za Kasulu na Kibondo dhidi ya kero za wananchi hususan kuteswa na vyombo vya dola na watendaji wa serikali.

Hali hiyo ndiyo ilimlazimu kupanga kufanya ziara mkoani Kigoma kuwasikiliza wananchi yeye mwenyewe, ingawa alilazimika kuahirisha ziara hiyo mara tatu tangu Julai mwaka huu, kutokana na majukumu ya kiofisi ndani na nje ya nchi.

Hapa ni kijijini Muhange...tutaanza na mkutano huu kisha tutatoa maelezo na kuweka picha za mkutano wa pili Kakonko mjini. Wenyeji au watu wanaofahamu maeneo haya, wanajua namna gani kulivyo na miundombinu hafifu ya mawasiliano, hususan internet. Tunashukuru kwa kutuvumilia.

Kurugenzi ya habari CHADEMA

No comments: