Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, November 9, 2013

DKT SLAA NJE YA NCHI NA MIKAKATI MIZITO YA KUBORESHA AFYA

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa yuko Ulaya, nchini Ujerumani kwa ziara ya kikazi ya siku mbili, kuanzia Novemba 7, mwaka huu, katika mji wa Bensheim, Makao Makuu ya Shirika la Kimataifa la Kimataifa la CBMI Mshirika mkuu wa Taasisi ya CCBRT ambayo yeye Dkt. Slaa ni mwanzilishi na Mwenyekiti wake. 

Ni kwamba CCBRT kwa ajili ya kuboresha huduma zake, ipo kwenye mpango mkubwa wa upanuzi, kwa kuanzia na 

Baobab Hospital, mother and Child yenye vitanda 200 itakayokuwa na huduma zote za kisasa,
Ujenzi wa Private Clinic ambayo unaweza kuanza wakati wowote, na; Staff Housing na Hostel. Kutakuwa na jumla ya majengo sita hivi yenye ghorofa nne kila moja. Mambo hayo yote yanakisiwa kugharimu zaidi ya Euro 150 million.

Hivyo Bodi ya CCBRT na Bodi ya CBMI watakuwa na mkutano wa siku mbili katika mji wa Bensheim, dk 45 kutoka jiji la Frankfurt, Ujerumani. 

Lengo kuu la mkutano huo ni pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ya pande hizo mbili na kutengeneza mpango mkakati wa pamoja katika upanuzi huo mkubwa ambao unalenga kubadilisha sura ya huduma kwa mama na mtoto katika jiji la Dar Es Salaam.

No comments: