Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Sunday, October 13, 2013

Breaking News: Wamerakani Wamvulia Kofia Dr. Slaa. Wamuona kama Mkombozi Wa Bara La Afrika


Akielekea ukingoni mwa safari yake, Katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbrod Slaa ameacha historia nchini Marekani kwa kuonyesha kukubalika kwa kiwango kikubwa miongoni mwa viongozi wa ngazi mbali mbali nchini humo. Kutokana na msimamo wake dhidi ya ufisadi, busara, sera zake na chama chake, Dr. Slaa ameidhiirisha siyo umma wa Kitanzania na Kimarekani, bali dunia kwa ujumla ya kwamba ni kiongozi ambaye yuko Tayari kuliokoa taifa la Tanzania na bara la Afrika.

Gavana wa Jimbo la Indiana katika Kipindi chake cha Radio Jijini Indianapolis , amesema kwamba ili Afrika iondokane na maradhi, ujinga, na umasikini, viongozi kama Dr. Slaa ndio dawa. “ I was amazed and humbled to meet such a visionary man. My huts off to him. He is a brilliant and a visionary fellow whose time has come. He is a hero of our time. I can’t imagine how difficult it must have been for him to campaign under police horrific bombings” alisema governor Pence.

Dr. Slaa ameonyesha kiu ya maendeleo, na sisi kama taifa inayoipa elimu kipaumbele, ni lazima tuwe tayari kumpa huyu kiongozi wa kipeke mkono ili atayarishe nguvu kazi ya kesho. Ni aibu kiongozi kama huyu mzalendo kubughudhiwa na vyombo vya dola kwa sababu tu ni mpinzani wa chama iliyopo madarakani.

Viongozi wengi barani Afrika wamesahau kwamba elimu ndiyo ukombozi wao. Dr. Slaa ameonyesha njia ya kulikomboa nchi yake aliongeza gavana Pence. Kadhalika wachangiaji mbali mbali walioshiriki katika kipindi hicho, walionekana kumkubali Dr. Slaa mpaka kumfananisha na Nelson Mandela pamoja na Kwame Nkurumah

Katika kipindi kifupi akizunguka katika majimbo tofauti nchini marekani, Dr. Slaa ameonyesha uchungu na nchi yake. Kadhalika ameonyesha umahiri mkubwa kusimama na kupigania haki, licha ya kufanya hivyo katika mazingira magumu na kandamizi.

Ameweka wazi msimamo wake, kwamba kamwe Afrika lazima ijiondoe katika biashara kandamizi na pia kuweka wazi msimamo wake wa kutokukukubali misaada ya kigeni isipokuwa biashara itakayo wanaufaisha wananchi wake na sawa na mwekezake. Siyo biashara inayoegemea upande mmoja.

2 comments:

Anonymous said...

Nabii hatambuliki kwao.....

Computer Link Developments said...

Dr. Slaa kama tusipo ku support tayari Mungu amekukubali na endeleza kupigania haki za taifa, Tanzania ni Nchi kama zingine na mabadiliko haya epukiki