Mhadhiri wa Chuo Kikukuu cha Dar es Salaam, Profesa Chris Maina |
Profesa Maina alisema katika Bunge hilo, wabunge wote 357 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ambao idadi yao ni 81 watakuwa wajumbe wa bunge hilo huku wananchi wa kawaida wakiwa ni 166 tu. Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba, amewataka wabunge na wawakilishi wanaotaka kuingia katika Bunge Maalumu la Katiba, wajiuzulu kwanza ubunge. Kibamba alisema kimsingi wananchi wengi hawataki kuona mbunge yeyote aliyopo Dodoma au Baraza la Wawakilishi anakwenda kushiriki kwenye mkutano wa Bunge la Katiba kwa sababu siyo kazi yake ambayo alitumwa na wapiga kura wake. Kwa upande wake, Kamishina wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi, alisema Tume haitahusika katika suala la Bunge Maalumu la Katiba kwa sababu kazi yake itakuwa imekoma.
Source: Mwanakatwe T. ( Sept. 2013). Profesa atahadharisha mchakato Katiba mpya. Retrieved from Ippmedia/Nipashe
Source: Mwanakatwe T. ( Sept. 2013). Profesa atahadharisha mchakato Katiba mpya. Retrieved from Ippmedia/Nipashe
No comments:
Post a Comment