Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Monday, September 16, 2013

Pinda aweka pingamizi kesi dhidi yake

   Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amewasilisha katika Mahakama Kuu ya Tanzania, pingamizi kuhusu kesi ya kikatiba dhidi yake. Kesi hiyo imefunguliwa kwa ushirikiano wa Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS). Katika kesi hiyo, taasisi hizo mbili zinadai kuwa Pinda alivunja Katiba kwa madai kuwa aliamuru vyombo vya dola kuwapiga wananchi pale wanapokaidi amri ya polisi na kufanya virugu. Mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni, Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
       Jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Kiongozi, Fakihi Jundu, akisaidiana na Jaji Dk Fauz Twaib na Jaji Augustine Mwarija, limepanga kusikiliza kesi hiyo ilyotajwa kwa mara ya kwanza jana. Upande wa walalamikaji uliowakilishwa na mawakili wanne kati ya saba waliotajwa. Mawakili hao ni, Fulgence Massawe na Harold Sungusia wanaomwakilisha mdai wa kwanza (LHRC), Rais wa TLS, Francis Stola, Makamu wa Rais wa TLS, Peter Kibatala, Mpale Mpoki na Jeremiah Mtobesya wanaomwakilisha mdai wa pili (TLS).
      Upande wa wadaiwa Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, uliwakilishwa na mawakili wakuu watatu wa Serikali. Mawakili hao ni, Nickson Mtingwa, Sarah Mlipana na Alesia Mbuya. Hata hivyo upande wa madai uliomba siku 21 kuwasilisha majibu ya majibu ya wadaiwa.
Source: Magai J. ( Sept 2013).Pinda aweka pingamizi kesi dhidi yake. Retrieved from Mwananchi

No comments: