Pamoja
na Kamanda Kova kuongea jambo ambalo halieleweki la kuzuia Maandamano ya Kesho
tarehe 21September 2013. Viongozi wa Vyama vya Upinzani wamesisitiza Maandamano
yako palepale na hakuna wa kuyazuia wala sababu ya kuyazuia haipo.
Kama
ujio wa Obama wa siku moja tu ulifunga barabara kwa siku tatu sembuse Katiba
yetu sisi Watanzania!!? Je Oboma ni bora zaidi kuliko Katiba yetu??
Kova
na wenzako mkumbuke popote mlipojaribu kuingilia mambo ya kisiasa nchini mliua
au mliwaacha watu vilema au yote mawili kwa pamoja. Tumieni busara ila uminyaji
huu wa demokrasia hauwezi kukubalika hata kidogo wala damu ya Watanzania
haiwezi kuchezewa kwa ulevi tu wa madaraka na ukosefu wa busara na hekima wa
viongozi wa Jeshi la Polisi.
Maandamano
yataanzia kwenye vituo viwili ambavyo ni Tazara na Ubungo kuelekea Jangwani
yakiongozwa na viongozi wakuu wa vyama vyote vya Upinzani ambapo kutakuwa na
Mkutano Mkubwa ambao haujawahi kufanyika katika historia ya siasa za nchi hii.
Taasis
mbalimbali hapa nchini zitashiriki katika Mkutano huo ambazo ni pamoja na
Jukwaa la Katiba, Shura ya Maimau, CCT,TEC, SHIVYAWATA, TGNP, Vyama vyote vya
Upinzani vyenye usajili hapa nchini n.k
Maandamano
yataanza saa tatu kamili asubuhi
NGUVU YA MAJESHI HAIJAWAHI KUSHINDA
NGUVU YA UMMA
No comments:
Post a Comment