LIPUMBA ASEMA MBOWE AMEDHALILISHWA BUNGENI
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), tukio
la Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani kuondolewa bungeni mjini Dodoma kwa agizo
la Naibu Spika, Bw. Job Ndugai, lilipangwa na Serikali ili kuhakikisha Muswada
wa sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba mwaka 2013, unapitishwa
bungeni ili kulinda masilahi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mkurugenzi wa
Habari na Uenezi CHADEMA, Bw. John Mnyika, ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo,
aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema Serikali ilipanga kupitisha muswada huo bungeni ndio maana hata Bw.
Mbowe kama Kiongozi wa Upinzani bungeni, aliposimama kutaka kuzungumza,
hakupewa nafasi hiyo badala yake alitakiwa akae na alipokataa Bw. Ndugai
aliagiza atolewa nje jambo ambalo hawakuliunga mkono.
Aliongeza kuwa, Serikali inafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wabunge
wa CCM wanakuwa wengi katika Bunge la Katiba ili kupitisha mambo
wanayoyataka."Kilichopitishwa bungeni na wabunge wa CCM ni kibaya kuliko
ilivyokuwa awali...wameharibu zaidi, CHADEMA imepinga kwa masilahi ya makundi
mengine ya kijamii ili yaweze kupata uwakilishi katika bunge hilo," alisema. Bw.
Mnyika alisema CHADEMA walipendekeza Bunge la Katiba lipunguze uwakilishi wa
chama kimoja ambapo katika kipengele cha wajumbe 166 wanaoteuliwa na rais,
iongozwe na kufikia wajumbe 359 lakini Serikali imekataa."Lengo letu ni
kutoa nafasi kwa makundi mengine ya kijamii kama wakulima, wafanyabiashara,
wafanyakazi na taasisi nyinginezo kutoa wawakilishi wao kwenye bunge
hili," alisema.
Alisema upande wa Zanzibar, hakukuwa na wawakilishi waliotoa maoni yao
juu ya nafasi ya Zanzibar katika bunge hilo na kilichosemwa na Serikali ni
uongo."Serikali baada ya kushindwa kuchakachua Mabaraza ya Katiba, sasa
imeona njia pekee ya kufanya hivyo ni kuhakikisha kwenye Bunge la Katiba
wabunge wa CCM wanakuwa wengi," alisema. Akizungumzia uamuzi wa Bw.
Ndugai kumtoa nje Bw. Mbowe, alisema Naibu Spika amevunja kanuni ya 76 ya Bunge
kwani hana nguvu ya kuita askari ambapo kwa mujibu wa kanuni ya 20, alitakiwa
kuhairisha shughuli za Bunge."Ndugai amefanya kosa la kuwaingiza watu
wasiohusika bungeni na kuruhusu vitendo vya uhalifu vitokee ili kupitisha
muswada walioutaka na kulinda masilahi ya chama kimoja.
"Sekretarieti ya CHADEMA itakutana kesho (leo) ili kujadili kwa
undani suala hili na kulishughulikia, pia tutatumia nguvu ya umma (wananchi)
kuhakikisha katiba haivurugwi, tutakutana na vyama vingine vya upinzani,"
alisema.Alisema chama hicho hakioni sababu ya kuharakisha katiba badala yake
kama wanataka katiba hiyo itumike katika Uchaguzi Mkuu 2015 ni vyema
ikaandaliwa ya mpito. Aliongeza kuwea, katika Bunge lijalo Sheria ya Kura
za Maoniambayo itajadiliwa ni ya hatari zaidi kuliko Bunge la Katiba na
isipofanyiwa marekebisho, itazusha mgogoro mkubwa zaidi.Katika hatua nyingine,
Chama cha Wananchi (CUF), kimepinga kitendo cha askari wa Bunge, kumtoa nje
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Bw. Freeman Mbowe, baada ya kuzuiwa
kuzungumza. Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba,
aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa
habari.Alisema kitendo cha Naibu Spika wa Bunge, Bw. Job Ndugai, kuwaagiza
askari wa Bunge wamtoe nje Bw. Mbowe, hakiwezi kukubalika, bali ni unyanyasaji
na udhalilishaji mkubwa.
"Ni kitendo cha aibu na hakikupaswa kufanywa na Naibu Spika
(Ndugai), CUF tunajiuliza angesimama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kutaka
kuzungumza angemnyima?" alihoji.Alisema Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba mwaka 2013, ulikuwa na utata mkubwa kwani Serikali imeubadili kwa
kuondoa maoni muhimu ya wadau ambapo Wazanzibari hawakushirikishwa
ipasavyo. "CUF tunataka muswada huu urejeshwe kwa wananchi ili
ujadiliwe upya, mbali ya Mbunge wa Singida Mashariki (Tundu Lissu- (CHADEMA) na
Naibu Katibu Mkuu wa CUF upande wa Zanzibar (Hamadi Masoud), kuthibitisha kuwa
Zanzibar haikushirikishwa, wabunge wetu hawana taarifa kama wananchi wao
walishirikishwa.
"Kuupitisha muswada huu ni njama za wazi za Serikali na kiti
cha Spika kutelekeza maoni ya wananchi na kuyapatia kipaumbele ya CCM, hivyo
kuondoa uhalali wa Bunge na kiti cha Spika katika kusimamia mchakato wa kutafuta
Katiba Mpya," alisema.Katika hatua nyingine, Prof. Lipumba muswada huo
unampa Rais Jakaya Kikwete, mamlaka ya kuteua watu anaowataka kuwa wajumbe wa
Bunge la kutunga sheria. Aliongeza kuwa, hivi sasa kila taasisi itapaswa
kuteua majina tisa na kumpa Rais ambaye atateua jina moja au asiteue kabisa,CCM
na Serikali wanajua hujuma wanazofanya katika mchakato huu ili kupata katiba
wanayoitaka wao si wananchi," alisema.Alisema upo umuhimu wa wananchi
kuunga mkono msimamo wa wabunge wa upinzani na kudai kuwa, watendaji wa
Serikali wakiwemo Mawaziri na Naibu Spika, wanamhujumu Rais Kikwete
asifanikishe mchakatato wakupata Katiba Mpya. Alisema muswada wa kwanza wa
Mabadiliko ya Katiba ulikuwa mbovu ambapo Rais Kikwete alilazimika kuzungumza
na wapinzani ili kuurekebishaWakati huo huo, CUF imedai kusikitishwa na kitendo
cha kupigwa na kutupwa nje ya lango la Bunge Mbunge wa Mbeya Mjini, Bw. Joseph
Mbilinyi (CHADEMA), na kuvuliwa hijab kwa Mbunge wa Viti Maalum, Bi. Mozza
Abeid (CUF) na kudai huo ni udhalilisha usiokubalika.
Source: Balama R., & Said D. (Sept. 2013).
CHADEMA: NDUGAI ALITUMWA. Retrieved from Majira
No comments:
Post a Comment