Lwakatare akiwa hospitalini leo |
Tangu Jana Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Kamanda
Alfred Lwakatare amelazwa hospitali ya Muhimbili(Pichani).Nanukuu maelezo yake
hapa
‘’Mkirejea
tatizo la kiafya nililolipata nikiwa Central Police baada ya kukamatwa; la
kuumwa sana na mgongo/mkono na baadaye nikiwa gerezani
Segerea nilipelekwa Muhimbili Moi na baada ya vipimo (M.R.I) wakabaini kuna
ulazima wa kufanyiwa upasuaji. Tatizo hili limeendelea na hata baada ya kutoka
Segerea na nimekuwa nikiwaona madaktari kwa ukaribu. Jana mchana,imelazimu
kulazwa hospitali ya Muhimbili ward ya Sewahaji NO.18,chumba No.024 kwa
uchunguzi na matibabu zaidi.
Kama
ilivyo kawaida yetu; Tunaanza na Mungu,Tunaendelea na Mungu na kumaliza na
Mungu.
Tuzidi
kuombeana na yote tumkabidhi Mungu.
Nawapenda
sana!’’
Ofisi ya Katibu Mkuu imetuma timu kutoka makao makuu muda mfupi
uliopita wakiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Katibu Mkuu Mzee Victor
Kimesera ambayo ilienda kumjulia hali.Taarifa Rasmi itatolewa na msemaji wa
chama
Kipindi chote alichoshikiliwa kwa makosa ya kubambikiza
kimechochea tatizo kubwa alilokua nalo kiafya.
Tunaomba tuungane tena katika hili kama tulivyoungana katika
kipindi chote cha kesi
No comments:
Post a Comment