Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Thursday, July 11, 2013

Tumpuuze Mwigulu Nchemba na Mwenyekiti Wake(Picha), Tuimarishe haraka Red Brigade




Ninaunga mkono maazimio ya kamati kuu ya CHADEMA ya kuanzisha mafunzo ya ukakamavu kwa vijana kwa ajili ya kujilinda,kulinda viongozi na mali za chama chao.Binafsi nimefurahia sana jinsi mwitikio ulivyokua mkubwa,vijana wamehamasika,ari yao ipo juu.Tusonge mbele tena tufanye haraka
  
Ni jambo la ajabu kuwa tunae Rais asiyejua kuelekeza hasira na kauli zake sehemu sahihi.Rais Kikwete alinukuliwa na shirika la utangazaji la BBC akilaani hatua hii ya CHADEMA alipokua katika zoezi la kufunga kongamano la amani lililoitishwa na TCD. Kongamano la amani bila amani halina mantiki,ni kongamano nje ya mantiki.Unapokua na kongamano la Amani ambalo linashindwa kukemea kauli za kichochezi zilizotolewa na Waziri mkuu, basi moja kwa moja dhana nzima inabadilika na sasa linakua ‘kongamano la unafiki’

Naomba nikope busara za Rais kupitia kauli yake maarufu ‘Akili za kuambiwa,changanya na zako” kwa kumkumbusha Rais kikwete yafuatayo

Mosi, Katiba ya CHADEMA ambayo ilipelekwa kwa msajili wa vyama vya siasa ipo wazi kuhusu suala la kuwa na kikundi cha ulinzi kulingana na ibara hii,naomba kuinukuu‘

’7:7:5 Kutakua na mfumo wa ulinzi na usalama wa mali,viongozi na maslahi ya chama utakaotambulika kama brigedia nyekundu(Red Brigade)’’

Hii ni katiba ya CHADEMA ambayo haijawahi kupigiwa kelele na haijavunja sheria wala katiba ya nchi maana kama ingekiuka sheria basi ofisi ya msajili wa vyama vya siasa pamoja na wanasheria wakuu walitakiwa wakamatwe mara moja na hata Rais atakua ameshiriki kuvunja katiba mana siku zote ilikuwepo.Kinachofanyika sasa hivi ni kuwa Red Brigade inaimarishwa zaidi na vijana kupata mafunzo ya ukakamavu zaidi.Rais alitakiwa kutafakari na pengine kuomba ushauri kabla hajaibuka na kauli hii inayoweza kumvunjia heshima na kutufanya sisi vijana tuwe wepesi wa kuhoji weledi wake nap engine katika hatua mbaya zaidi kuishia kudharaulika

Pili,Rais Kikwete alitakiwa amlaani waziri mkuu wake aliyemteua.Kauli ya Pinda ya kutaka jeshi la polisi kupiga Raia ni kauli ya ovyo kutolewa na kiongozi mwenye busara na Rais alitakiwa amfukuze kazi mara moja badala ya kuwalaani Raia wanaojilinda.Hapa ndipo nilipoona konagamano lile ni mkusanyiko wa wanafiki na wasaliti wakubwa wa Taifa hili.Nami natumia fursa hii sasa kuwalaani.

Pinda alivunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoapa kuilinda na kuitetea.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 13(2) inasema: “Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweka sharti lolote ambalo ni la kibaguzi ama wa dhahiri au taathira yake.”

Kifungu cha nne cha ibara hiyo hiyo kinasema:

“Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa shughuli yoyote ya mamlaka ya nchi.” Pinda alitoa kauli hiyo akiwa anatekeleza kazi yake kama Kiongozi wa Serikali Bungeni.

Katiba Ibara ya 13 (6) (e) inaonya kuwa: “Ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazomtweza au kumdhalilisha, pia Ibara ya 16 ya Katiba inasema: “Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi ya nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na pia heshima na hifadhi ya maskani na mawasiliano yake binafsi.”

Waziri mkuu amevunja katiba na Rais kwa kulinyamazia hilo, ameshiriki kuvunja katiba ya nchi.

Tatu,Sotetunatambua kuwa Katiba yaJamuhuri ya muungano ya Tanzania inakataza mtu, chama au taasisi yoyote kuunda jeshi au chombo chenye muelekeo wa kijeshi “Para-millitary groups” ispokuwa serikali yenyewe. Kwa mfano; Katika sura ya tisa ya Katiba; Ibara ya 147 (1) inaeleza :

“Ni marufuku kwa mtu yeyote au shirika
lolote au kikundi chochote cha watu, isipokuwa Serikali kuunda au kuweka Tanzania jeshi la aina yoyote”. Sasa pamoja na kifungu hiki cha katiba; CCM(Green Guard), CUF(Blue Guard) na sasa CHADEMA(Brigedia nyekundu kwa ajili ya kujilinda) wana vikosi vya ulinzi ndani ya chama. Je ina maana ni ukiukaji wa katiba?

Nne,Mwenyekiti hiuyu wa CCM Ndugu Jakaya Kikwete alitakiwa atangaze maslahi katika laana zake alizotoa maana inajulikana kwamba Chama chake kinachomiliki vikundi vya green Guard wakati huo huo wakisaidiwa na polisi kama alivyokiri kwenye mkutano wa NEC mwaka jana ndicho kinachohatarisha amani

Pia nimeona maelezo ya naibu katibu mkuu wake Mwigulu Nchemba yaliyojaa upotoshaji na au pengine ni mgumu kuelewa na pengine lugha ya kiingereza inamtatiza hasa pale alipotumia maneno ya kiingereza yasiondana na dhana maarufu ya misamiati husika.Kikosi cha Green Guard hapa chini hakifanyi mazoezi ya kawaida maana wanafanya hadi mazoezi ya silaha na pia wameanza kufanya mazoezi hayo kwa kutumia vijana wadogo wenye umri chini ya miaka 18 na kuwalea kwa viapo.Maelezo ya mwigulu ni ya uongo na upotoshaji

















RED BRIGADE ya Italy ilikua Political Group ambayo ilikua na itikadi kinzani dhidi ya umoja wa kujihami wan chi za Magharibi NATO.Ilitambulika kama Brigate Rosse yaani BR.Ilikua na mrengo wa kiitikadi unaoendana na Leninism au Marxism ukiongozwa na Mario Morreti.Hapo ni lazima tuweke historia sawa
Mathalani CCM wanaogopa kivuli chao kwa maovu wanayotekeleza kupitia Green Guard ambayo ina muundo kama wa The green Armies ya Russia ya chama cha Kisoshalisti cha mapinduzi na walikua wakifanya kazi ya kuteka na kushambulia wafuasi wa vyama vingine.Red guard ambayo baadae ilikuaja kugeuka kuwa red army ilipambana na wafuasi hao .CHADEMA hakipambani,kinachukua hatua ya kujilinda maana wafuasi na viongozi wetu wanashambuliwa huku polisi wakiwa kimya


Nampa Mwenyekiti wa CCM ndugu Jakaya kikwete na Mwigulu Nchemba changamoto.Wasome Ripoti ya Amnesty International ya Mwaka 2001 juu ya kikundi cha kihuni cha Ghaddafi kilivyokua kikiwafanyia wananchi wa Libya.Kikundi hicho kilikua kikifanya hayohayo Mwigulu Nchemba aliyosema
Ripoti ina kichwa cha habari

‘Libya: Existence of the Green Revolutionary Guard; origin, composition and activities; whether this organisation is involved in kidnappings and torture; possible threats against returned asylum seekers by the Revolutionary Guard or other groups ‘  Pia muundo wa Green Guard hauna tofauti na muundo wa Red Guard ya China ambayo ilikua ikitesa,kuteka na kushambulia Raia miaka ya 1960.Ilikua Political movement group ya vijana iliyoratibiwa na baadhi ya makada waliokua wakimuunga mkono Chairman Mao

RED NA GREEN ni Rangi tu ila dhamira na vitendo vinatofautiana. Picha hizo hapo juu zinatoa taswira halisi na watanzania sasa waamue



















Katika Picha: Kushoto ni Mbunge wa Ilemela (CHADEMA) Highnes Kiwia aliyeshambuliwa na wafuasi wa CCM tarehe 31 Machi,2012 baada ya kufunga kampeni ya uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya Kirumba-Mwanza.Polisi hadi leo wapo kimya,kongamano la Amani lipo kimya na msemaji wa Jeshi la polisi hana majibu


Pichani Kulia:Mzee Nyaulingo Lunyiliko ambaye ni mwenyekiti wa wazee wa wilaya ya kilolo akivuja damu baada ya kushambuliwa na Green Guard wakati wa kampeni za ichaguzi mdogo uliofanyika Juni16,2013



Maiti ya kada na Mwenyekiti wa CHADEMA USA RIVER aliyeuawa kinyama.Miongoni mwa watuhumiwa ni viongozi wa Kitongoji cha Mgadini wa CCM Davis Mkumba na Mathias Nathan ambao walitoroka Oktoba 4,2012 wakiwa chini ya ulinzi wa polisi walipokua wakipelekwa mahakamini.Marehemu aliacha mjane na watoto wadogo

Hapa Chini ni kada wa CCM aliyekua akipewa mafunzo tofauti na uongo alioueleza Mwigulu Nchemba,sasa Laana za Mwenyekiti wa CCM Ndugu Jakaya Kikwete azielekeze huku.Jeshi la polisi lilikua wapi.Sikiliza hiii na baada ya hapo Rais achague moja Green Guard ifutwe ama TUIMARISHE RED BRIGADE. Hakuna compronise!!


Source: Saanane B. (July 2013).Tumpuuze Mwigulu Nchemba na Mwenyekiti Wake(Picha), Tuimarishe haraka Red Brigade. Retrieved from Jamii Forums

No comments: