Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, June 15, 2013

FACEBOOK WALL: Mbunge Joshua Nassar afunguka, anusurika kutekwa


"Whats going on in Tanzania? Jana usiku nilikoswakoswa kutekwa na ccm, nikajiokoa na nikawakamtisha polisi watekaji kwa msaada wa ocd wa monduli afande Okinda na ocs wa makuyuni. Watekaji wakashikwa wakiwa wameniblock usiku wakakutwa na madawa ya kulevya mirungi kwenye gari dogo aina ya mark II. Maelezo yapo polisi makuyuni lakini watekaji waliachiliwa huru pamoja na kukutwa na madawa na kukutwa wameniblock." Mh. Nassar

 "Leo  ndo inekuwa mbaya zaidi, gari langu aina ya L/C GX ikiwa imebeba mawakala kuwapeleka kulala kusikojulikana lakini nje ya makuyuni limezuiliwa na ·agari matatu likiwemo lile la jana barabarani katikati ya pori kabla ya kufika mto wa mbu, dereva akafanikiwa kugeuzia porini na kutoroka wakarudi makuyuni, na mimi nikiendesha mwenyewe ford ranger ya chama kama kuelekea tarangire junction/babati wakanifuata lakini wakashindwa kuifukuza gari yangu nikawaacha, niliendesha kasi ya km 180 ambayo sijawahi before. Nimeingia kwenye lodge moja hifadhini tarangire ikawa pona yangu kwa usiku wa leo. Ni siku ya pili watawala wanataka kuniteka, wanausalama wanajua lakini bado hawajachukua hatua." Mh. Nasssar


"Kwenye picha, kushoto ni mdogo wake na aliyekuwa diwani wa makuyuni msomali, katikati ni dereva wangu, kulia ni mkuu wa kituo cha makuyuni monduli OCS na ameshika madawa (mirungi) iliyokutwa kwenye gari yenye wasomali watatu waliotaka kuniteka kwa maelekezo ya Lowassa". Mh. Nassar

"Ccm hoy makuyuni. Lowasa kabeba watu toka mto wa mbu, lokisale, monduli juu chini na kati, duka bovu, babati, longido etc. Tutarusha picha. Wameleta watu mpaka kwa semi-trela kama zile zinazobeba ng'ombe toka usukumani. Hakika na tumewabana. Wafanyakazi kadhaa wa halmashauri ya monduli ambaye pia nasimamia uchaguzi wameniambia hawajawahi kuona hii monduli kwa miaka yote waliyosimamia chaguzi ndogo na kuu." Mh. Nassar


"Gari iliyotumiwa kujaribu kuniteka, Mbunge Joshua Nassar,  jana usiku ikiwa kituo cha polisi cha makuyuni wilayani monduli. Hata hivyo watekaji ambao pia gari yao ilikutwa na mirungi na wao wakila mirungi waliachiwa na gari yao pia.

Walikuwemo wanaume watatu wenye asili ya kisomali. Leo tena mawakala wetu wamekoswakoswa kutekwa between makuyuni na mto wa mbu.mimi nimewatoroka watekaji wengine eneo la mswakini karibu na minjingu, nikaingia kwenye hoteli ya kitalii hifadhini tarangire. Hii ni saa chache baada ya bomu la Soweto Arusha" Mbunge Joshua Nassar

No comments: