Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, April 20, 2013

Waziri atuhumiwa kukwapua Sh bilioni 30



MBUNGE wa Meatu, Meshack Opulukwa (Chadema), amemtuhumu Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, kwa kujitengea Sh bilioni 30 kwa ajili ya mradi wa maji katika wilaya yake. Akiuliza swali bungeni jana, Opulukwa alisema fedha hizo zimetengwa mwaka wa fedha 2013/14 na kutaka zigawanywe katika halmashauri zote. “Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inamega fedha hizo, hivyo badala ya kupelekwa katika wilaya hiyo moja zigawanywe katika wilaya nyingine?” alihoji Mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais asiyekuwa na Wizara Maalum, Profesa Mark Mwandosya, alisema hafahamu kama Wilaya ya Mwanga, imetengewa kiasi hicho cha fedha, bali anaufahamu mradi wa maji Mwanga kwa kuwa aliuanzisha yeye wakati akiwa Waziri wa Maji. “Wote tunafahamu matatizo ya maji katika miji ya Mwanga, Same, Korogwa na Olkasment, tulipata fedha kutoka BADEA na Sekta ya Mandeleo ya Maji, bahati nzuri Profesa Maghembe kawa Waziri wa Maji na kaukuta mradi ulioanzishwa na mimi katika wilaya yake,” alisema Profesa Mwandosya.


Awali akijibu swali la msingi la mbunge huyo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Agrey Mwanry, alisema Serikali inatambua tatizo la maji katika kata za Wilaya ya Meatu. Alisema katika mwaka 2011/12, utekelezaji wa mradi wa maji umefanyika katika kijiji cha Mwang’umbi kilichopo katika kata ya Ilamaseko. 

Alisema mwaka 2012/13, shughuli ya usanifu wa mradi mkubwa wa maji katika Kata ya Bukundi Kijiji cha Bukundi, umeshafanyika na kukamilika na ujenzi wa miundombinu utaanza katika mwaka wa fedha 2013/14. “Kupitia fedha za Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo la Meatu, Kijiji cha Mwanyahina kitapelekewa maji kwa kuongeza vituo vya maji viwili.

“Serikali itaendelea kuweka kipaumbele cha utekelezaji wa miradi ya maji katika maeneo mengine yaliyobaki kadri fedha zitakavyopatikana,” alisema Mwanri. Katika swali lake la msingi, Opulukwa alitaka kujua mpango wa Serikali wa kuwapatia maji safi na salama wakazi wa Kata za Mwabuzo, Bukundi, Mwanjolo, Mwamishali, Mwanyahima, Nkoma na Ilamalaseko.

Source: Sanja D. (April 2013). Waziri atuhumiwa kukwapua Sh bilioni 30. Dododma. Retrieved from Mtanzania

No comments: