Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Monday, April 15, 2013

Maelezo ya Tundu Lissu baada ya kutoka mahakamani ambapo kesi ya Lwakatare iliendeshwa kwenye Chamber ya Mahakama





Lissu: Tusikilizane!! Naomba tusilizane

Naomba kwa niaba ya timu Lwakatare niwashukuru wote mliofika hapa kutuunga mkono na kumuunga mkono Kamanda wetu Wilfred Muganyizi Lwakatare. Kama tulivyosema wakati kesi hii inafunguliwa ya kwamba Lwakatare atapata utetezi wote unaostahili. Atapata utetezi wote utakaothibitisha kwamba hana hatia yoyote. Tumetoka kusikiliza maombi tuliyoleta Mahakama Kuu kuomba Mahakama kufuta mashauri yaliyofunguliwa dhidi Wilfred Lwakatare. 

Na niseme tu kwamba sisemi kesi itaamuliwaje, ila naomba niseme hoja ambazo tumezizungumza mbele ya Jaji muda mfupi uliopita. Wilfred Lwakatare alishitakiwa tarehe 18 na siku hiyo hiyo tukatoa hoja za kisheria kwamba hayo mashtaka hayakuwa na mashiko, na upande wa washtaki wakajibu hoja zetu, na mahakama ikaweka tareheya kutoa uamuzi wake juu ya hoja zetu. Lakini badala ya kuiruhusu Mahakama itoe uamuzi, Waendesha mashtaka upande wa serikali kesho yake wakafuta hati ya mashtaka waliyofungua tarehe 18, dakika hiyo hiyo wakamkamata, dakika iliyofuta wakamfungulia mashtaka ya aina hiyohiyo wakayapeleka kwa Hakimu mwingine; Na kwetu sisi huo ni mfano wa wazi wa matumizi mabaya ya mamlaka ya Mwendesha mashtaka wa serikali wa mamlaka ya kufuta mashtaka. Sheria zetu zinasema DPP anapofuta mashtaka lazima afanye hivyo 

1. Kwa lengo la kutenda haki
2. Kuzuia matumizi mabaya ya mfumo wa Mahakama
3. Kwa manufaa ya Umma

Kufuta mashtaka na kuyafungua yaleyale hakuna lengo la kutenda haki, kuzuia matumizi mabaya ya mfumo wa Mahakama wala manufaa ya Umma, kwasababu hiyo basi tumeiomba Mahakama Kuu iyafutilie mbali mashtaka dhidi ya Lwakatare. Lakini kuna jambo lingine; Kama mlivyoona Wilfred Lwakatare ametoka hapa akiwa na pingu mkononi, ameshtakiwa kwa makosa ya ugaidi, Sheria yetu ya ugaidi inasema mtu anayeshtakiwa kwa kosa la kutenda mkutano wa kigaidi, huo mkutano wa kigaidi unatakiwa uwe na watu watatu au zaidi. Lwakatare ameshtakiwa na mtu anaitwa Joseph Ludovick Lwezaura; walikuwa wawili. Mkutano wa kigaidi sheria inasema uwe na watu watatu au zaidi, “Hakukuwa na Mkutano wa kigaidi”. Na sheria hiyohiyo inasema kwamba mashtaka ya kigaidi lazima hati ya mashtaka ionyeshe lengo la kigaidi, hati ya mashtaka dhidi ya Lwakatare haionyeshi lengo la kigaidi. Kwa sababu hizo tumeiomba Mahakama Kuu ifute mashtaka ya Kisutu, Wilfred Lwakatare arudi kwenye familia yake na arudi kwenye Chama chake tuendeleze mapambano. Nawashukuruni sana.

No comments: