Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Friday, May 9, 2014

UVCCM yataka Mzee Moyo atoswe CCM


Hassan Nassor Moyo
Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) imesema  imechoshwa na vitendo vya muasisi wa chama hicho, Hassan Nassor Moyo, kwa madai ya kukisaliti na kukidhoofisha chama hicho.  Akizungumza na waandishi wa habari  jana, Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka, aliwataka viongozi wakuu wa CCM kuchukua hatua za  kinidhamu na  kumnyang’anya kadi ya uanachama muasisi huyo.  Moyo ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano ambayo ilihusika wakati wa kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na ni mtetezi wa muundo wa serikali tatu.

     Shaka alisema kwa muda mrefu Mzee Moyo  amekuwa akikihujumu CCM bila ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu, na kwamba hali hiyo  linakidhoofisha chama hicho na kukivunjia hadhi mbele ya wananchi, hivyo wakati umefika kwa muasisi huyo kufukuzwa CCM.  ‘CCM kina mtaji wa wanachama, viongozi na waasisi wengi, si maskini, heri wabaki wachache kuliko kuendelea kubaki na wanachama wasaliti na wakorofi,” lisema Shaka.  Shaka alisema Moyo amekuwa akitumia mwavuli wa uanachama wa CCM kukivuruga na kukisaliti chama hicho kupitia Kamati ya Maridhiano ambayo alisema haikuundwa kwa mujibu wa sheria wala Katiba ya Zanzibar na kwamba Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, alishasema  hadharani kwamba kamati hiyo haitambui. 

    “Hii ni kamati ya upekepeke inayomzunguka na kumyumbisha  Rais Shein, haikuundwa kisheria, haina hadidu za rejea, haifahamiki kazi zake, kwanini ipande jukwaa la CUF na kuliogopa la CCM?” alihoji Shaka. Mzee Moyo alipoulizwa, alisema hashughulishwi na maneno yao na kuwa ni mwanachama wa CCM, ana haki ya kutoa maoni na anaona Serikali tatu ndizo zinazofaa.


Suleiman R. / IPP Media/Nipashe

No comments: