Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, November 5, 2013

USHAURI WA SAUTI YA HEKIMA KWA VYAMA VYA SIASA

Joseph Golliama
Nia na Lengo la kila chama cha siasa ni kushika Dola ili kiweze kujenga Taifa na kusimamia Ujenzi wa Taifa na kufanya wananchi wa makundi yote wapate maisha Bora na Taifa Zima lipate ustawi na maendeleo endelevu, katika kupambana kufanikisha nia na lengo la kushika Dola kila chama kina jukumu la kuhakikisha kinatumia makosa ya serikali ya chama kilichopo madarakani kuwahahakikishia wananchi kama chenyewe kitapewa lidhaa ya kushika dola basi kitafanya mazuri kwa manufaa ya Taifa kuliko serikali iliyopo madarakani. mambo muhimu ambayo kila chama kinapaswa kuyatazama na kuyakosoa kwa serikali iliyopo madarakani ni haya

1. Serikali iliyopo madarakani inapaswa kuhakikisha Taifa linakuwa na Sauti moja ya kuisikiliza na kama Taifa halina Sauti moja ya kuisikiliza hilo ni jambo la kuihoji serikali iliyopo madarani kwani ni wajibu wake. Inapofika wakati wananchi kama hawajui sauti ya kuisikiliza na wanajiuliza hivi tuisikilize sauti ya viongozi wa dini zetu au tusikilize sauti ya viongozi wa vyama vyetu au tusikilize sauti ya viongozi wa makabila yetu au tuisikilize sauti ya serikali hii inaonyesha Taifa linatatizo kubwa haliijui ni sauti ipi ya kuisikiliza.

2. Serikali iliyopo madarakani inapaswa kuhakikisha Taifa linakuwa na mwelekeo mmoja wa kuufuata na kama Taifa halina mwelekeo mmoja wa kuufuata hilo ni jambo la kuihoji Serikali iliyopo madarakani kwani ni wajibu wake.Taifa lisilo na mwelekeo mmoja ni Taifa lililo njia panda lisilojua kwa kwenda

3. Serikali iliyopo madarakani inapaswa kuhakikisha Taifa linakuwa na Muafaka wa kitaifa wa ujenzi wake yaani muafaka wa makundi yote ya wananchi wa aina ya Taifa tunalotaka kulijenga litakalohakikishia makundi yote ya wananchi ustawi na maendeleo endelevu, muafaka wa ujenzi wa Taifa ndio pekee uwezao kuyafanya makundi yote ya wananchi kuwa na amani katikati yao kama haupo amani miongoni mwa makundi hayo inakuwa adimu.ili kuepuka Taifa kugawanyika kwa misingi ya makundi ya wananchi ni lazima pawepo muafaka wa makundi yote wa ujenzi wa Taifa laasivyo Taifa litagawanyika kwa misingi ya Dini,vyama vya siasa,matabaka ya maisha,makabila,jinsia,rika nk

4. Serikali iliyopo madarakani inapaswa kuhakikisha Taifa linakuwa na Umoja wa upendo ndani yake, umoja ni ile hali ya makundi ya wananchi kupendana na kuthaminiana na kujaliana hivyo serikali inawajibu wa kuwaongoza wananchi kuacha tabia zinazihatarisha umoja wao na umoja wa Taifa kwa ujumla wake,tabia hizi zinapaswa kupigwa vita na serikali ndani ya Taifa ili umoja wa Taifa uimalike, tabia za makundi mbalimbali kuwa na chuki,uadui,fitina,faraka,uzushi,ugomvi,ufisadi,ulevi,uchu,Wivu,ujambazi,Uwizi,tamaa mbaya, usengenyaji, manung'uniko,ushoga,uuaji,ubakaji,uonevu,ukatili,ujeuri,uchokozi, uzembe,uzinzi,uasherati,umalaya,ugaidi,uchafu,uchawi,roho mbaya,ulawiti,hasira,

5. Serikali iliyopo madarani inapaswa kuhakikisha Taifa linakuwa na mawasiliao ya haki ndani yake, mawasiliano ni ile hali ya makundi ya wananchi kuaminiana na kila kundi kuona kundi lingine lina haki ndani ya Taifa, hivyo serikali inapaswa kujenga mawasiliano kwa kuongoza makundi yote ya wananchi kubomoa katikati yao tabia za kukataana,kuhukumiana,ukabila,unyonyaji,dharau,udini,udhehebu,uzuluraji,ubinafsi,madeni,kisasi,umaskini,ujinga,laana,magonjwa,kupenda fedha,kupenda mali,kupenda anasa,kupenda sifa,ubahiri,Rushwa, ukimbizi wa aina zote,kukata tamaa,kujikweza, kukosa shukrani,Dhuluma,Talaka zisizo za msingi,Vita, upendeleo,Ukanda,umaeneo,Uchama, na kila kisicho haki serikali inapaswa kuongoza wananchi kukikataa na kukiacha

Nguvu zote na mamlaka zote ambazo serikali inazo inapaswa kuzitumia kufanya hayo mambo matano na kusimamia Taifa kuhakikisha milele linabaki kuwa na Sauti moja ya kuisikiliza linakuwa na mwelekeo mmoja wa kuufuata, linakuwa na amani, umoja wa upendo na mawasiliano ya haki hapo TAIFA letu litaanza kusonga mbele kuelekea ustawi na maendeleo endelevu

Kama serikali iliyopo madarakani haifanya hayo vyama vya siasa vinapaswa viitumie hali hiyo ya serikali kuwa dhaifu katika kutimiza maslahi ya TAIFA Kuwahakikishia wananchi kwamba wao wakipewa nafasi ya kuunda serikali watatimiza hayo kwa kutumia nguvu na mamlaka ya raslimali za Taifa letu

Ushauri 1; Chama chenye serikali iliyopo madarani kinapaswa kuisimamia serikali kuhakikisha kinafanya haya ninayoyashauri ili kiendelee kupewa fulsa ya kushika dola otherwise ipo siku kitajilaumu kwa kushindwa kutumia fulsa adimu ambayo wananchi walikipa

Ushauri 2; Vyama vinavyotaka kushika Dola angalieni udhaifu wa serikali katika kutumia mambo hayo kwani mkiwahahakikishia wananchi wa makundi yote kuwa mtaunda serikali itakayofanya Taifa letu kuwa na sauti moja ya kuisikiliza, mwelekeo mmoja wa kuufuata, amani, umoja wa upendo na mawasiliano ya haki naamini Mungu atakuwa nanyi na ipo siku kama dhamiri yenu ni ya kweli Mungu atawapa mkitakacho

Nawasilisha mchango wangu wa mawazo kwenu wananchi wenzangu 

Joseph Goliama

No comments: