Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Thursday, September 5, 2013

Vurugu zagubika bunge la Tanzania.

    
           Bunge la Tanzania kwa mara nyingine limeingia katika mzozo wakati wa mjadala unaoendelea  wa muswaada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba ambao umesusiwa na wabunge ya kambi ya upinzani kwa madai ya kutoshirikisha maoni ya upande mmoja wa muungano yaani Zanzibar. Mzozo huo ulizusha  vurugu kubwa ambapo pia inadaiwa baadhi ya wabunge wa upinzani baada ya kutoka nje walivutana  askari wa bunge na kudiriki kutaka kurushiana ngumi  baada ya Naibu Spika wa Bunge  Job Ndugai, kuamuru kutolewa nje kwa kiongozi wa upinzani bungeni Bw. Freeman Mbowe, na wabunge wa upinzani kuzuia kiongozi huyo kutolewa ukumbini ambapo mbunge wa Mbeya Mjini CHADEMA Joseph Mbilinyi alianza kutolewa nje, kutokana na kuzuia kiongozi wao kutolewa nje ya ukumbi wa bunge.


      Amri hiyo ya naibu spika, ya kumtoa nje bwana Mbowe  ilikuja mara baada ya Kiongozi huyo wa Upinzani bungeni kukataa kutii mamlaka ya kiti ya kukaa chini ili kupisha mjadala wa muswaada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba wa mwaka 2013, uendelee . Kutokea kwa tafrani hiyo kulitokana na mbunge wa Mkoani, Bw. Ali Khamis Seif kuomba muongozo wa spika, akitaka hoja iliyokuwa mbele ya bunge ya kujadili muswada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba iahirishwe, na Naibu Spika kuamua kuitisha kura ambapo wabunge wasiounga mkono mjadala huo uahirishwe wakiwa wengi kutoka chama tawala CCM, walishinda.

        Mbunge wa Iringa Mjini, CHADEMA  Mchungaji Peter Msigwa alifafanua nini hasa kiongozi huyo wa upinzani bungeni alikuwa anataka kusema wakati Naibu Spika wa bunge alipoamuru akae chini, ambapo alisema alitaka kufafanua alichodai upotoshwaji uliofanywa na mwanasheria mkuu wa serikali juu ya muswada huo. Pamoja na tafrani hiyo, Mjadala wa muswada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba uliendelea ambapo muswada huo unapendekeza mambo mbalimbali ikiwemo idadi ya wajumbe wa bunge la katiba na namna ya kuwapata, idadi ya siku za mjadala wa rasimu na mengineyo.

Source: VOA (Sept. 2013).Vurugu zagubika bunge la Tanzania. Retrieved from VOA Sauti ya Amerika

No comments: