Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Tuesday, September 3, 2013

Mengi asikitishwa na kauli ya Waziri Muhongo



      MWENYEKITI wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Reginald Mengi, amesema wamesikitishwa na kauli ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa Watanzania hawawezi kufanya uwekezaji katika uchumi wa gesi na mafuta na badala yake wanaweza kuwekeza katika biashara ya machungwa na juisi.

Kauli ya Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kampuni za IPP inatokana na madai yaliyotolewa hivi karibuni na Serikali kuwa uwekezaji wa vitalu vya gesi unahitaji mtaji wa kuanzia Dola milioni 100 za Marekani.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mengi alisema siyo sahihi kwa Profesa Muhongo kusemea uwezo wa Watanzania kushiriki katika uchumi wa gesi na mafuta ni mdogo.



      “Tumesikitishwa na inasikitisha kuona kwamba waziri wa nishati na madini anaona Watanzania waendelee kuwekeza katika uchumi wa machungwa na juisi.

“Kauli aliyoitoa Profesa Muhongo kwa vyombo vya habari inaonyesha wazi kwamba Serikali haina juhudi za makusudi kuhakikisha Watanzania washiriki katika uchumi wa gesi,”alisema.

Alisema ushiriki wa uchumi wa gesi na mafuta hauhitaji rasilimali fedha bali unahitaji ujuzi wa kwenda katika masoko ya mitaji.

“Kwanza naomba ieleweke kuwa sisi hatupingi wawekezaji kutoka nje ya nchi bali tunataka mgeni akija na sisi tunufaike kwa sababu hii ni nchi yetu, hakuna mahali kwingine tutaenda kisha tutasema ni nyumbani kwetu zaidi ya Tanzania.

         

“Hapa ni suala la ujuzi wa biashara na uwekezaji, zaidi ya hapo Watanzania wanaweza kwenda katika masoko ya mitaji na kuwa na utaratibu maalumu utakao wawezsha kushiriki kwa ukamilifu,” alisema Mengi.

Alisema ingawa Profesa Muhongo kukataa kukutana nao kujadili suala hilo kwa madai hana muda, wao hawatakwenda kwa Rais Jakaya Kikwete kutoa malalamiko yao bali watafuata mfumo rasmi wa kuwasiliana naye.

Source: Mtanzania (Sept. 2013).Mengi asikitishwa na kauli ya Waziri Muhongo. Retrieved from Mtanzania

No comments: